Je ni sahihi wanafunzi wa shule za msingi za serikali kupewa chakula wale tu waliolipia pesa ya chakula na wengine kuzunguka zunguka tu nje?

Je ni sahihi wanafunzi wa shule za msingi za serikali kupewa chakula wale tu waliolipia pesa ya chakula na wengine kuzunguka zunguka tu nje?

realMamy

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2024
Posts
3,925
Reaction score
8,853
Hii ni kwa baadhi ya Shule za Msingi zinazofanya hivyo.

Hii inatisha sana kwa sababu watoto hutia huruma wakati wengine wakiwa nje na mawazo Mengi sana.
Niliwahi kufanya utafiti kidogo wa kuwauliza watoto kuwa wanafikiri ni kwa nini wazazi hawawalipii Chakula? Majibu yao yalikuwa tofauti tofauti.

Wengi wao walieleza kuwa wazazi Hawana kipato cha kutosha.

Wengine walisema wazazi wao wenyewe wakiwa nyumbani wanakula milo yote mitatu lakini wanashindwa kuwalipia pesa kidogo ya Chakula.

Wengine walisema baba zao wanajua ratiba zote za Mechi za mipira lakini hawajui kama watoto hawapati chakula cha mchana Shuleni.

Walieleza kuwa wanajisikia vibaya sana kwa sababu wanashindwa kuelewa hata masomo darasani kwa kuwa na njaa.

Kama Inawezekana basi ule mfumo wa zamani wa kulima mahindi shuleni urudi ili watoto wote wapate chakula Shuleni.

Hii inaumiza sana Serikali tunaomba mlifanyie kazi.

Kama tunaweza kutoa msaada wa mahindi nchi za Jirani basi Tusaidie na watoto wetu.

Wanafunzi wana njaa sana.

PIA SOMA
- Mtoto wako (aliye shule ya kutwa) anapata chakula shuleni? Kwa kiwango gani mzazi/mlezi unahusika katika kufanikisha hilo?
 
Sasa aleje kitu ambacho hajachangia.

Mtoto afundishwe hajala kwa sababu vitu huwa vina gharama na lazima vigharimiwe. Hii itamsaidia asiwe mwizi ukubwani. Itumike kama motisha na sio mshangao.
 
Haya mambo ya kutokuchangia mnayaweza sana. Waswahili, huwa hamtaki kuchangia kabisa ingawa ni mtoto wako

Ila sadaka wanatoa sana wwkifikiri pepo yao

Charity begins at home jamani ila wengi hawaelewi

Mwalimu atasemwa kwa kila mabaya
 
Mtu unazaa ovyo bila mpangilio watt 6, unakaa nyumba ya kupanga au kwako kipato n full kuunga unga, hapo lazima watoto wasile shule na kaptula na viatu vyote vina matobo, begi zuri mtoto anayaonaga Kwa wenzake ,nauli ya kwenda shule shida mtt anagombana na makondakta Kila cku mpk wamemkariri.

Aiseee tuzae Kwa mpngo waalimu tunawaonea Bure nao pia wanachangamoto zao njee ya huo uwalimu..
 
Hii Hoja yako "Kama Inawezekana basi ule mfumo wa zamani wa kulima mahindi shuleni urudi ili watoto wote wapate chakula Shuleni"

Inaweza kuwa applicable kwa shule za Mikoani zenye maeneo makubwa ya Kilimo. Je, huko mjini watafanyaje?
Labda ungesema mzazi ambaye hakulipia chakula kwa mtoto wake achukuliwe hatua e.g.

Kushtakiwa Ofisi ya Kata, kufunguliwa mashtaka Mahakamani(Polisi wahusike) lakini isiwe kumrudisha mtoto nyumbani (Kumfukuza shule).

Huku kwetu Mzazi analazimika kuleta mahindi, maharage na mafuta.Tofauti ya hapo anapelekwa mahakamani sawa kama yule anayeshindwa kumpeleka mtoto shule.
 
Back
Top Bottom