Je ni sahihi wanafunzi wa shule za msingi za serikali kupewa chakula wale tu waliolipia pesa ya chakula na wengine kuzunguka zunguka tu nje?

Kama chakula kinanunuliwa na hakitoshi kuwapa wote unataka waliochangia wapewe nusu ? Kuna options mbili:
Wafanye research Yesu alibadilisha vipi mkate na kuwa mikate (which is impossible) au watu wapate means ya kupata disposable income ili waweze kumudu mahitaji yao (pamoja na kuwapatia watoto wao chakula mavazi na malazi)
 
Upumbavu mkubwa ulioko hapa nchini ni kuwadekeza wazazi kuhusu elimu. Yaani hoja ya chakula mzazi analalamika Kwamba Hana kipato....KAZI KUFINUKA NA KUJAZA WATOTO Ila linapokuja suala la kulea na kusomesha umasikini unakuwa kichaka.

Ingekuwa vyema elimu ilipiwe tena gharama kubwa,then huduma ya afya itolewe bure.

Kitu pekee ambacho huja bila kupangwa ni magonjwa na yanaweza kukuta huna hata senti lakini kusomesha ukishajua umekojoa ndani....jiandae.
 
Ifike wakati tuishi kibepali tu, huna hela hakuna kula.

Umaskini sio wakuendekeza sana
Huko kwa mabepari halisi Marekani na Ulaya watoto wote shuleni wanapewa chakula kwa gharama za serikali.
 
Wazazi ndo changamoto hapo.
Ubishi wa kijinga na kufata mkumbo, kila mchango anahisi anaibiwa.

Mwalimu akuibie nini hasa kama sio kuwaonea tu hawa watumishi wa umma.
Chakula cha wanafunzi mashuleni inapaswa kuwa wajibu wa serikali.
 
Haya mambo ya kutokuchangia mnayaweza sana. Waswahili, huwa hamtaki kuchangia kabisa ingawa ni mtoto wako
Ila sadaka wanatoa sana wwkifikiri pepo yao
Charity begins at home jamani ila wengi hawaelewi
Mwalimu atasemwa kwa kila mabaya
Hata Ulaya wazazi hawachangii chakula kwenye shule za umma, ni wajibu wa serikali kuwapa wanafunzi chakula bora chenye virutubisho.
 
Shida kubwa iko hapa, kuna matanzania yanazaa kama nguruwe wakati uwezo duni, yanaishia kutesa watoto kwa lishe duni huduma zingine mbovu mixer vipigo vya stress za maisha
Ni huzuni....
 
Ni wajibu wa serikali kuwapa wanafunzi chakula mashuleni, pia ni wajibu wa serikali kuhamasisha uzazi wa mpango kwa raia wa nchi.
 
Ni wajibu wa serikali kuwapa wanafunzi chakula mashuleni, pia ni wajibu wa serikali kuhamasisha uzazi wa mpango kwa raia wa nchi.
πŸ‘πŸ»πŸ‘πŸ»πŸ‘πŸ»
 
ni wajibu wa serikali kuhamasisha uzazi wa mpango kwa raia wa nchi.
Ni wajibu wako ww na mm pia mkuu..mm Nina mmoja na sioni dalili ya kuongeza ,mkuu ww uko na wangapi
 
Nikijibu swali lako, ni sahihi kutopewa chakula sababu hawajalipia, haitakua sawa kwa waliolipia.
Njia itakayoleta uniformity kama unavyotaka ni utaratibu wa serikali kagawa chakula mashuleni, ila hata wakisema watoto waje na vyakula kutoka nyumbani bado kutakua na malalamiko na kutia huruma kutokana na chakula watakavyokua wanakuja navyo.
Pia, mahindi na masomo haviendi kabisa πŸ˜…
 
Nilikuwa na mengi ya kusema lakin hayatakuwa na msaada acha nibaki nayo tu
 
Wazazi ndo changamoto hapo.
Ubishi wa kijinga na kufata mkumbo, kila mchango anahisi anaibiwa.

Mwalimu akuibie nini hasa kama sio kuwaonea tu hawa watumishi wa umma.
Mimi binafsi sioni kosa la wazazi maana hawana uelewa na mchakato wa kujifunza na kupata elimu
Mitaani tuna walimu waliosoma hadi level ya degree lakini hawafanyi tafiti za kutosha ili kupata suluhisho la haya yote badala yake mipango mingi hasa shule za vijijini inapangwa kwa mihemko hasa na wanasiasa wa vijijini wasiokuwa na ujuzi wowote mwisho wa siku uungwaji wa mkono unakuwa mdogo maana mengi yanakuwa ya kisiasa na lazima kuwepo na utofauti wa kisiasa na hata wazazi wanaweza wakakataa kusapot kwa sababu za utofauti wa kiitikadi za siasa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…