Je, ni sahihi Watoto kushirikishwa katika usuluhishi wa ugomvi wa wazazi?

Je, ni sahihi Watoto kushirikishwa katika usuluhishi wa ugomvi wa wazazi?

mabutu1835

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2018
Posts
909
Reaction score
1,425
Naendelea kushuhudia kuongezeka kwa matukio ya baadhi ya familia watoto hasa wengine wakiwa na miaka 17 wakishirikishwa katika kusuluhisha migogoro ya wazazi wao.

Inawezekana hali hii inatokana na kukosekana kwa watu wazima katika familia au viongozi wa dini wakikosa kuaminiwa na baadhi ya familia.

Kwa mtazamo wangu sioni kama ni sahihi watoto kushirikishwa katika kutafuta suluhu ya wazazi wao. Usuluhishi wa migogoro ya wanandoa inahitaji umri, ukomavu wa akili kuhusu maisha, uzoefu wa masuala ya ndoa, nk.

Kila mmoja atoe mtazamo wake na ushauri ikibidi ili tusaidie vijana wasiogope ndoa kutokana na majeraha ya nafsi walizoshuhudia katika vikao vya kutatua migogoro ya ndoa za wazazi wao.
 
Wakati tupo sekomdari kuna jamaa akasema likizo hii sirudi nyumbani. Tukamuuliza kwanini, akasema Mama na Baba wanataka kuachana lakini Mzee ananisubiri mimi nitoe maamuzi ya Talaka.
Eeenh siendi maamuzi yoyote yatakayofikiwa ntayakubali. Mama na Baba yake walimsubiri kijana wao wa kwanza hakutokea.
Sijui ile kesi iliishaje maana ilikuwa muhula wa mwisho.
 
Taasisi ya ndoa imeshapoteza maana, sikuelewa kwa nini watawa wa kikatoliki walikatazwa ndoa na kutakiwa kuwa waseja, lakini sasa hivi naelewa vizuri.

Ndoa nyingi sasa hivi ni upuuzi mtupu, bora hata wachumba upendo unakuwepo.
 
Binafsi naona ni vyema watoto wakishirikishwa huenda baadhi ya ndoa zikabaki, kwani watoto huwa hawapendi wazazi wao waachane na huwa wanaathirika sana.

Na ni vyema washirikishwe kwenye maamuzi mengi mengi tu yanayohusu familia, hiyo inakuwa kama mbinu ya kumpa uzoefu mtoto wa jinsi ya kuishi na familia yake hapo baadae.
 
Binafsi naona ni vyema watoto wakishirikishwa huenda baadhi ya ndoa zikabaki, kwani watoto huwa hawapendi wazazi wao waachane na huwa wanaathirika sana.

Na ni vyema washirikishwe kwenye maamuzi mengi mengi tu yanayohusu familia, hiyo inakuwa kama mbinu ya kumpa uzoefu mtoto wa jinsi ya kuishi na familia yake hapo baadae.
Naunga mkono hoja.
 
Naendelea kushuhudia kuongezeka kwa matukio ya baadhi ya familia watoto hasa wengine wakiwa na miaka 17 wakishirikishwa katika kusuluhisha migogoro ya wazazi wao.

Inawezekana hali hii inatokana na kukosekana kwa watu wazima katika familia au viongozi wa dini wakikosa kuaminiwa na baadhi ya familia.

Kwa mtazamo wangu sioni kama ni sahihi watoto kushirikishwa katika kutafuta suluhu ya wazazi wao. Usuluhishi wa migogoro ya wanandoa inahitaji umri, ukomavu wa akili kuhusu maisha, uzoefu wa masuala ya ndoa, nk.

Kila mmoja atoe mtazamo wake na ushauri ikibidi ili tusaidie vijana wasiogope ndoa kutokana na majeraha ya nafsi walizoshuhudia katika vikao vya kutatua migogoro ya ndoa za wazazi wao.
Inategemea na ukomavu wa mtoto aisee
 
Kwa kweli sio sahihi,mtoto wa kiume unaskia mama yako amechepuka huko au baba yako anamfua mingumi mama yako huko chumbani ….then na wew unatakiwq kua msuluhishi!! Kwa kweli mimi siwezi sana sana nitatoka na chuki na dharau juu yao.
 
Back
Top Bottom