Je, ni ukiukwaji upi wa Haki za Binadamu unaofanyika Tanzania?

Je, ni ukiukwaji upi wa Haki za Binadamu unaofanyika Tanzania?

Chagu wa Malunde

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
8,734
Reaction score
5,750
Ninauliza hili swali ili ndugu zangu kama Watanzania tupate kufahamu hawa jamaa wamarekani ambao huiona nchi yao kama paradiso wametuwekea zuio la kutusua kuingia nchini kwao.

Hapa Tanzania kuna ukiukwaji wa haki za binadamu? Na kama upo ni zipi? Kwa mujibu wa Serikali ya US ni kwamba pamekuwa na uminywaji mkubwa wa demokrasia, uhuru wa kuongea au kutoa maoni, na wamezidi kusema kuwa hata haki ya kuishi nayo inakandamizwa sana (maana yake kuna mauji yanafanyika).

Tanzania sio nchi pekee iliyowekewa zuio la kucheza Green Card Lottery, Nigeria imo pamoja na baadhi ya nchi za Africa na Asia.Ila hapa Tz wamekwenda mbali hadi mmoja wa kiongozi ametajwa kuwa anahusika (labda wana ushahidi)
Jana BBC wameonyesha documentary fupi kama ya dakika 15 ikionyesha jinsi vyombo vya dola nchini Nigeria vinavyowatesa watuhumiwa hadi wakati mwingine kusababisha vifo na ulemavu kwa watuhumiwa.

Hayo yanayofanyika Nigeria hata hapa Tanzania yanafanyika watu na hata baadhi ya watumishi wa vyombo vya dola huyafanya (wakati mwingine kwa kukosa maadili) huenda ikawa sababu ya hawa jamaa kutuweka katika kundi la nchi zilizopigwa ban (zuio). Vitendo hivi vinachafua taswira ya nchi yetu. Nasema hivyo sababu Tanzania ni nchi inayoendeshwa kwa kufuata misingi ya sheria.

Mtu anaiba kuku anapewa kesi ya unyag'anyi wa kutumia siraha.Akitoka humo ndani ana kirema (tortured) na haya mambo yanafanana kabisa na kule Nigeria.

Mimi maoni yangu tunapaswa tujitafakari kama Taifa; justice system yetu iko vipi? Ipo sawa watuhumiwa wanapata haki zao? Watuhumiwa wanateswa mpaka kufa? (Maana kuna minog'ono vijiweni kuwa watu wanapotezwa bila kuwa na hatia)

Tusijikite zaidi katika kuweka hisia zetu kuwa kesi za akina Eric ndio sababu (hizi ni kesi ambazo zipo mahakamani) Ila hatujui kuna wananchi wangapi ambao ndugu zao walipata matatizo wakiwa mikononi mwa vyombo vya dola (nazungumzia watu wasio na uwezo).

Tanzania sasa hivi ni nchi iliyopiga hatua. Kama waliweza kuipa kampuni tenda (jina kapuni) ifunge mitambo ya kutambua alama za vidole kandarasi ambayo mpaka leo ni kitendawili, kwa nini wasinunue lie detectors! Kama nchi za wenzetu.

Mambo ya kutesa na kupiga watuhumiwa yamepitwa na wakati.
 
La uchaguzi serikali za mitaani jibu tosha.. usisumbuke tete. Kweli we uchaguzimdogo umeona ni kawaida kufunga ofisi siku za kurudisha form?
 
Ukishashiba ugali wa awamu ya tano unajifanya maiti zilizokuwa zinaokotwa fukweni hujui, unajifanya akina lisu kupigwa risasi hujui, unajifanya katazo la vyama vya siasa kufanya siasa hujui, unajifanya watoto wa kike kunyimwa kusoma hujui,unajifanya kuwa sheria ya kutakatisha fedha kutumika kuziba watu midomo hujui na pia unajifanya visanga vya uchaguzi wa serekali za mitaa hujui!Unafikiri kila Mtanzania atajifanya kipofu kama wewe? Unakuja hapa kwa mbwembwe kuwa serekali inaongozwa kwa mujibu wa sheria! You are cursed!
 
Ukishashiba ugali wa awamu ya tano unajifanya maiti zilizokuwa zinaokotwa fukweni hujui, unajifanya akina lisu kupigwa risasi hujui, unajifanya katazo la vyama vya siasa kufanya siasa hujui, unajifanya watoto wa kike kunyimwa kusoma hujui na pia unajifanya visanga vya uchaguzi wa serekali za mitaa hujui? Unakuja hapa kwa mbwembwe kuwa serekali inaongozwa kwa mujibu wa sheria! You are cursed!
Jamani nimeuliza swali ili tujuzane. Ugali wa awamu ya tano unatoka wapi? Nigeria napo kulikuwa na uchaguzi? Chad na Mynmar?
 
Bila picha inaweza isieleweke
IMG_20200210_222217_640.JPG
images (4).jpeg
images (3).jpeg
images (2).jpeg
images (1).jpeg
images.jpeg
 
Ukishashiba ugali wa awamu ya tano unajifanya maiti zilizokuwa zinaokotwa fukweni hujui, unajifanya akina lisu kupigwa risasi hujui, unajifanya katazo la vyama vya siasa kufanya siasa hujui, unajifanya watoto wa kike kunyimwa kusoma hujui,unajifanya kuwa sheria ya kutakatisha fedha kutumika kuziba watu midomo hujui na pia unajifanya visanga vya uchaguzi wa serekali za mitaa hujui!Unafikiri kila Mtanzania atajifanya kipofu kama wewe? Unakuja hapa kwa mbwembwe kuwa serekali inaongozwa kwa mujibu wa sheria! You are cursed!
Watu mnaokariri kama wewe zamani walikuwa wanaitwa bendera fuata upepo. Miaka ile ya nyuma 1995 kurudi nyuma mpaka tunapata uhuru waliopata mimba walikuwa wanasoma? Kutakatisha pesa suala likienda mahakamani hutakiwi hata kuhoji (mahakama ni chombo huru) wacha kesi ziishe upate majibu.
 
La uchaguzi serikali za mitaani jibu tosha.. usisumbuke tete. Kweli we uchaguzimdogo umeona ni kawaida kufunga ofisi siku za kurudisha form?

Naongezea Risasi kwa yule mbunge, Azori, zile maiti ufukweni,
 
Bwana tundu antipas mughwai lisu alipigwa risasi 36 hakuna hata wakusingiziwa alokamatwa.

Ndug alphonso mawazo aliuwawa karibu kabisa na kituo cha polisi hajakamatwa hata mdudu

Ndg.Erick kabendera mwandishi wa habari anashikiliwa kwa ml. Alikuwa anafanya biashara gani?.

Bi. Akwilin akilina aliuwa na police waliopo mahakamani ni wengine

Magazeti tuliokuwa tunasoma yamefungiwa nk

Watu walinyanyaswa na kuuliwa huko rufiji, mafia na kilwa. Yaani serikali ilipeleka jeshi kwenda kupambana na raiya? Nakumbuka mateso yale ya pale nyamisati unapekuliwa kama unaenda ughaibuni! Namlaani sana huyu bwana


Sent using jamii forums mobile app
 
Ukishashiba ugali wa awamu ya tano unajifanya maiti zilizokuwa zinaokotwa fukweni hujui, unajifanya akina lisu kupigwa risasi hujui, unajifanya katazo la vyama vya siasa kufanya siasa hujui, unajifanya watoto wa kike kunyimwa kusoma hujui,unajifanya kuwa sheria ya kutakatisha fedha kutumika kuziba watu midomo hujui na pia unajifanya visanga vya uchaguzi wa serekali za mitaa hujui!Unafikiri kila Mtanzania atajifanya kipofu kama wewe? Unakuja hapa kwa mbwembwe kuwa serekali inaongozwa kwa mujibu wa sheria! You are cursed!
Tatizo ni kujibu hoja kwa kusoma kichwa cha habari, na kuwa na mahaba ya kisiasa kwa kila suala hata ambalo halihusiani na mahaba ya Chama flan( Pole sana)
 
Watu mnaokariri kama wewe zamani walikuwa wanaitwa bendera fuata upepo. Miaka ile ya nyuma 1995 kurudi nyuma mpaka tunapata uhuru waliopata mimba walikuwa wanasoma? Kutakatisha pesa suala likienda mahakamani hutakiwi hata kuhoji (mahakama ni chombo huru) wacha kesi ziishe upate majibu.
Mkuu nafikiri unakosea sana unapojaribu kuweka mambo yaliyokua yanafanyika miaka ya 95 kurudi nyuma na sasa.Maisha yamebadirika mno, technologia imekua sana..watu wanauqezo wa kufuatilia mambo katika real time kabisa, watu wanauwezo wa kuhoji siku hizi sababu ya uwepo wa urahisi wa kupata taarifa za uhakika...

Tukirudi kwenye mada pendwa..binafsi napigilia mstari na kukazia manani yaliyosema na kiongozi wa Tanganyika law Society juzi wakati wa kufunga maadhimisho ya wiki ya sheria..kitu kama icho...

Vyombo vyetu vya ulinzi na usalama haviko rafiki na watawaliwa..na hili sio suala la askari mmoja mmoj Hapana bali ni suala la kimfumo na sheria pamoja na MENTALITY inayopandikizwa....Vyombo vyetu vya ulinzi na usalama vimerithi mabaki ya Mkoloni ambae lengo laka halikua kufundisha ama kuonya...hapana....Jeshi la mkoloni lililenga kwenye kuleta hofu kubwa..sisi tumerithi sheria hizo hizo...matokeo yake ndo tuonavyo...Wati hawaruhusiwi kuhoji, watu wanawekwa ndani, wengine wanapotezwa etc..
Na hili suala linaenda hadi kwa viongozi ambao wanakua kama mkoloni tu...kutoa amri na kutekelezwa etc...Watu wamekua kama wafalme, wanaogopwa....


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu nafikiri unakosea sana unapojaribu kuweka mambo yaliyokua yanafanyika miaka ya 95 kurudi nyuma na sasa.Maisha yamebadirika mno, technologia imekua sana..watu wanauqezo wa kufuatilia mambo katika real time kabisa, watu wanauwezo wa kuhoji siku hizi sababu ya uwepo wa urahisi wa kupata taarifa za uhakika...

Tukirudi kwenye mada pendwa..binafsi napigilia mstari na kukazia manani yaliyosema na kiongozi wa Tanganyika law Society juzi wakati wa kufunga maadhimisho ya wiki ya sheria..kitu kama icho...

Vyombo vyetu vya ulinzi na usalama haviko rafiki na watawaliwa..na hili sio suala la askari mmoja mmoj Hapana bali ni suala la kimfumo na sheria pamoja na MENTALITY inayopandikizwa....Vyombo vyetu vya ulinzi na usalama vimerithi mabaki ya Mkoloni ambae lengo laka halikua kufundisha ama kuonya...hapana....Jeshi la mkoloni lililenga kwenye kuleta hofu kubwa..sisi tumerithi sheria hizo hizo...matokeo yake ndo tuonavyo...Wati hawaruhusiwi kuhoji, watu wanawekwa ndani, wengine wanapotezwa etc..
Na hili suala linaenda hadi kwa viongozi ambao wanakua kama mkoloni tu...kutoa amri na kutekelezwa etc...Watu wamekua kama wafalme, wanaogopwa....


Sent using Jamii Forums mobile app
Sawa kabisa. Ila hatukujenga shule zetu ili watoto wetu wawe na maadili mabovu kama kuanza ngono wakiwa wadogo na kuleta uwepo wa mimba za utotoni.
Ndio maana serikali inataka hao ambao labda kwa bahati mbaya au kwa makusudi walipata mimba wawe namna nyingine ya kuendelea na masomo.
Pia ni kweli kuna umuhimu wa kubadili sheria ambazo ziliachwa na wakoloni ambazo hazina manufaa kwa utoaji haki kwa miaka hii; Hilo halitasaidia kama kuna watumishi wa vyombo vya dola ambao hawana maadili. Sababu hata nchi zilizo endelea wapo wapo ambao hawana maadili (pamoja na kuwa na sheria nzuri) wapo wanaoua hata kutesa. Usa imekuwa ikikumbwa na mauji ya watu weusi toka wa maafisa wa polisi wasio na maadili.
 
Kwa nini NYUMBU wasahaulike kupelekwa kwenye zoo ya ikulu

Sent using Jamii Forums mobile app
nilidhani ungeuliza kwanni hawajapelekwa ikulu ya Chamwino?
nilidhani ungeuliza ule uhayawani mliofanyiana jana pale lumumba mmeufyata kwa wastaafu.
nlilijua ungeuliza aliyejenga uwanja wa chatto ni nani na tenda ilitangazwa wapi na je ile pesa ilipitishwa na bunge lipi?
nlihisi ungekwenda mbali na kuhoji mkandarasi anayejenga daraja la mto mara ni nani mbona kazi haziish na pesa anapewa?
hoji tena zilipo trilion 1.5 zilizomtoa assad CAG
Hoji hoji aliyemuua AZORY, MAWAZO NA BEN SANANE? Hoji aliyemminia risasi ndugu lisu yupo wapi?
hoji kidogo tenda za kununua midege ilitangazwa wapi? pesa ilipitishwa na bunge lipi?
hoji hoji ndugu hoji mv bagamoyo ilipo? hoji hoji hoji utajibiwa
hoji hoji kama waweza hoja na sio viroja
 
Back
Top Bottom