Je, ni wakati sasa Simba Sports Club kutafuta free kick specialist au waliopo wana uwezo huo?

kuna wakat SSC sajili zake sizielewi unataka kusema Africa nzima yupo Chama tu na team zote dunian haiwez kuuza mchezaji au wachezaji muhimu bila ya kupata mbadala wake walivyoondoka Chama na mwenzake hela ilikuwepo mm nilitegemea walete wabada plus forward mmoja matata pale mbele
 
Kabisa tena,kuna free kick nyingi zenye kuzaa matunda lakini akuna fundi wa izo mambo.

Nakumbuka Roberto Calos na David Beckham kwenye free kick tano basi angalau tatu lazima wakuumize.
Kwa hapa Africa now nani specialist wa freekick? Na je utamnunua mchezaji ili tu akusaidie freekicks ukiwa timamu kweli? Maana mabao ya freekicks ni machache mno duniani imagine Messi na ubora wake hajafikisha mabao 65 tu ya freekick wakati ana mabao 700 hivi ya carrier yake
 
Morison alifunga kwa freekick dhidi ya Red Arrows
Na duniani hakuna timu inanunua mchezaji wa kupiga freekicks tu kama ipo itaje
 
Huyo mtaalamu unayemsema kashapiga freekicks ngapi hadi sasa na kafunga magoli mangapi?
 
Morison alifunga kwa freekick dhidi ya Red Arrows
Na duniani hakuna timu inanunua mchezaji wa kupiga freekicks tu kama ipo itaje
sio kununua kwa ajili ya free kick pekee hapana ukichunguza asilimia kubwa ya wachezaji wanaojua kupiga hiyo mipira hata uwanjan sio vilaza kama unavyosema
 
Kwa hivyo Simba imnunue nani specialist wa freekicks? Na je mchezaji yupi wa timu yoyote hapa bongo amefunga magoli 10 ya freekicks kwa mwaka kama kweli ni ishu muhimu kihivyo? Hao hao waliopo wafanye mazoezi ya freekicks tu hakuna mchezaji ambaye akipewa kupiga freekicks unahesabu 99% ni kufunga kama yupo mtajeni hapa kwa waliopo now
 
na ndiyo maana nikauliza je wanunue au waliopo wanafaa ukirejea kwenye kichwa habar utaona
 
na ndiyo maana nikauliza je wanunue au waliopo wanafaa ukirejea kwenye kichwa habar utaona
Waliopo wanafaa , Morison amefunga kwa freekick , Mwenda anajua kufunga kwa Freekicks , Wawa vilevile nadhani tu tatizo ni uwekezaji wa makocha kuamua kuipa time ya kutosha sension ya set pieces na hadi sasa naona improvement kubwa hasa kwenye kona jambo ambalo lilikuwa tatizo sana nyakati za nyuma.Huwezi kutegemea kikosi hiki ambacho kinajaribu kuundwa upya kupata kikosi bora zaidi kikupe kila kitu 100%
Na by the way sisi tulio na kaujuzi kadogo tu ka mpira tunaamini hakuna timu iliyokamilika 100% kila timu ina udhaifu wake kazi ni kuugundua na kuutumia vema tu.
 
umenena vyema kabisa inabidi wawekeze kwenye hili swala nalo walipe uzito wake
 
Cm,, c,,, on x h. P x X,,,, p x x r zzz., and.,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…