Je, ni zipi faida na hasara za Diapers kwa watoto?

Je, ni zipi faida na hasara za Diapers kwa watoto?

Mtoto akijisaidia haja kubwa abadilishwe hapo hapo hata kama amevaa kwa sekunde 10.

Kuhusu mkojo, inategemea na ubora wa hiyo diaper, hizi fake za mchina na baadhi ya wabongo zinamlowesha na kumuunguza. Lkn nzuri kwa usiku waweza mbadilisha mara moja tu na asipate rashes wala kuchubuka
 
Kaunga na data kwanza mimi huku nimezamia tu. Ila kwa kweli nayajua madhara yake lakini Makampuni yanayozitengeneza wameweka jinsi ya kuzitumia, tatizo ni kina mama wetu, yaani hizo "diapers" ndiyo zimekuwa kimbilio lao.Mtu anakwenda mchepuko anamtwisha mtoto pampers anatokomea zake, masaa nane baadaye ndiyo anakuja kumbadilisha. Hapa sizungumzii mtu madhara ya kimwili lakini pia nazungumzia madhara ya kisaikolojia maana mtoto hana njia ya kujitetea!
 
Last edited by a moderator:
Wakina mama wengi vijana wameamua kuwavalisha watoto wao hizi nepi za kisasa maarufu kama Pampers, ili kuweza pamoja na mambo mengine kufanya kazi zao bila usumbufu wa kuwabadili watoto hao nepi mara kwa mara. Lakini ni sahihi kweli kwa kina mama kuwaacha watoto na hizo Pampers kwa siku nzima bila ya kuwabadilisha?

Maana siku hizi ni rahisi sana kukutana na mtoto wa miaka hata mitatu ananuka kinyesi kwa kuwa tu mama zao wamewazoeza kuwavalisha hizo nepi za kisasa. Wakina mama wamepewa taarifa za kutosha kiasi gani kuhusu madhara yatokanayo na kuwavalisha watoto Pampers kwa muda mrefu?

Mtoto akifikisha miaka miwili nerve system inakuwa imetengemaa, muscle contraction and sphincters are connected to parasympathetic nerve system. Wakati huu mtoto anauwezo wa kutambua anataka kujisaidia haja ndogo au kubwa. Mototo wa miaka mitatu anaenyea pampers anahitaji kuonwa na dactari.
 
UTI at work

Umeonaee na zilivyojaa sasa hivi kuutwa mwanangu ana u.t.i mimi czipendii kivile namfunga wkt wa kutoka na natumia agiiis. Mchana anafunga nappy za kawaida. usiku namlaza free apate mahewaa apumuee
 
Kuvaa diapers for 12 hours without changing them definetly its not right ... Mtoto anatakiwa kuchenjiwa kila muda diaper gets wet, hata kama alibadilishwa after 15 minutes then aka pee yes she / he still needs to be change again.. For 12 hours kwa same diaper without changing , mzazi ajiandae na UTI isiyokwisha .. Thanks .
 
Wadau tubadilishane ufahamu.

Baada ya ugunduzi huu kupata mapokezi mazuri kwa jamii, kwa sasa ni wakati mzuri kujua FAIDA na HASARA zake katika matumizi.

Diapers ni aina ya chupi zilizotengenezwa kwa utaalam wa kipekee kuweza kutumika kwa watoto mpaka wazee ili kuwaepusha na uchafu wa mara kwa mara utakaosababishwa na kutokwa kwa aja ndogo/kubwa pasipo ruhusa yako.

Mimi sijui kilichomo au kilichotengenezea hizo kitu ila napata hofu kutokana na nafsi kutokuwa huru nikizingatia wazazi//walezi wengi wameona kimbilio lao kwa sasa siyo nepi ila hizo chupi/nepi za kisasa.

**hapa naweka moja ya hasara za kijamii zinazotokana na hizo diapers, wananchi wengi wamekuwa wanatupa ovyo hizi kitu ukizingatia haziozi wala kuungua kwa haraka!.

Nafasi ni yako mdau kutoa faida na hasara tofauti na hiyo yangu.

Nawasilisha.
 
Wazazi sasa hivi wamekwa 'mateja' wa karatasi za nailoni zenye spongi kwa ndani maarufu kwa jina la pampasi kuwavalisha watoto wao badala ya kutumia vile vitaulo vyembamba vinavyojulikana kama nepi. Pampars ndiyo brand ya kwanza kuingiza bidhaa hizi zilizochukua nafasi ya matumizi ya nepi tulizozizoea, ingawa sasa hivi ziko kampuni nyingine zenye bidhaa kama hizi lakini watu huwa wanaziita zote pampasi hata kama brand yao sio Pampars, sawa na ilivyo kwa bidhaa za Shell, Kiwi, PANADOL, Mobil.

Madhumuni ya wazazi na walezi kuzipenda bidhaa hizi ni ule uwezo wake wa kuzuia mikojo na kinyesi toka kwa mtoto kisisambae nje na kuchafua sehemu nyingine za mazingira yanayomzunguuka mtoto. Hivyo mtoto ana uwezo wa kukaa na mkojo na kinyezi chake kwenye "pampasi" kwa muda mrefu sana usiku, safarini, au wakati walezi wanafanya kazi nyingine.
Pamoja na uzuri wa bidhaa hizi kwa walezi lakini zinasababisha kasoro kubwa na mbaya za kiafya kwa watoto. Ndani ya kinyesi wako bacteria na fungus wengi ambao wanasababisha ugongwa wa UTI and fangasi kwenye mfumo wa mkojo unayojumuisha kibofu cha mkojo na mafigo. Mtoto mwenye UTI anakuwa anahangaika ama kulia sana wakati wa kukojoa, anakojoa mkojo "mchafu" wenye vitu kama usaha na utando fulani (turbid), harufu na kupata homa kali isiyotibika kwa dawa za malaria. UTI isipotibiwa vizuri na haraka inasababisha uharibifu mkubwa wa figo za mtoto na mtoto kuonyesha dalili za kuvimba miguu na hatimaye mwili mzima kisha kifo.

KInachofanyika pale ni kwamba kinyesi na mikojo inapokuwepo pamoja kwenye pampasi kwa muda mrefu vinatawanyika hadi kugusa njia ya mkojo na kuwafanya bacteria walioko kwenye kinyesi (enterobacteria) wapate muda wa kutosha kuweza kupandisha juu kwenye kibofu na mafigo kupitia tundu la kukojolea na mirija inayosafirisha mkojo. Tofauti na nepi za kawaida ambazo kwa vyovyote vile mtoto huwa hakai na kinyesi chake kwa muda mrefu hivyo kupunguza muda wa bacteria kuweza kujisogeza hadi kwenye kibofu bila kufagiliwa (flushed) na mkojo mwingine wa mtoto.

Tatizo la UTI ni kubwa sana kwa watoto wenye jinsia ya kike kuliko jinsia ya kiume kutokana na maumbile ya jinsia ya kike kuweza kuruhu kinyezi kingi kibaki ukeni na kwa muda mrefu pamoja na umbali ufupi sana wa njia ya kufika kwenye kibofu ukilinganisha na mwanaume. Lile "bomba" la mwanaume huwa linairefusha safari ya bacteria kukifikia kibofu cha mtoto wa kiume. Mtoto wa kiume aliyetahiriwa mapema ana uwezekano mkubwa pia wa kujikinga na maambukizi ya UTI kuliko wenzao ambao hawajatahiriwa.

Wazazi pampasi ni janga sio ufahari, mkojo na kinyesi HUWA vina tindikali (acid) ambayo ikigusana na ngozi ya mtoto inasababisha kuunguza ngozi ya matako, mapaja na sehemu za siri za mtoto na kuonekana zimechubuka na kuwa nyekundu, hivyo kusababisha watoto wengi wapate mapele, majipu na fangasi kwenye ngozi mara kwa mara NA KUWAFANYA WAZAZI WANAPOZE HELA Na muda wao mwingi kununua pampasi, kununua matibabu ya watoto wao na kutumia muda mwingi wa kufanya vitu vingine kupeleka watoto dawani. Kama huwezi kuachana kabisa na matumizi ya pampasi basi Hakikisha kuwa unaibadilisha kila mara, yaani mara 3 kwa usiku kucha na mara 5 kwa mchana kutwa.
 
kavulata: sikio la kufa hakisikii dawa. Bandiko lako halitapata wachangiaji wengi kwa kuwaihusu watu au tukio na hata udaku.

Pampasi ni janga kama ilivyo matumizi mabaya ya "fridge" ambazo zimefanywa kuhifadhi vyakula viporo kwa kuamini haviharibiki. Mathalani maharage yanapikwa ya wiki na kuhifadhiwa kwenye "fridge" kumbe baada ya saa 6 hugeuka kuwa sumu guvu.

Akina mama kueni waangalifu na makini kwa afya ya familia
 
Ukweli hata mm huwa nawasiwasi sana na hizi mambo......inawezekana hata ikawa inaathiri mfumo wa uzazi kwa watoto maana wazungu wabaya sana
 
Ukweli hata mm huwa nawasiwasi sana na hizi mambo......inawezekana hata ikawa inaathiri mfumo wa uzazi kwa watoto maana wazungu wabaya sana
Wazungu sio wabaya. Kwao ''diapers'' zinatumika lakini kwa umakini. Sio kama huku kwetu unakuta mama anamvalisha mtoto anashinda nayo. Halfu hali ya hewa ya kwao ni tofauti na ya kwetu. Unakuta sehemu kama Dar joto ni kali lakini mtoto anavaa diaper masaa 24! Halfu quality ya diapers zao ni nzurii. BTW mwanzisha uzi kavulata asante sana. Umetoa elimu nzuri sana. Mimi nashauri kwa wenye watoto wadogo WASITUMIE kabisa hizi diapers. Kwanza nyingi zitatengenezwa na wachina uchochoroni hivyo hazina quality nzuri na zinakuwa contaminated. Pili mazingira ya kwetu hasa sehemu kama Dar ni ya joto sana. Nilikuwa na jirani yangu mtoto wake alikuwa haishi kuugua UTI. Alikuwa hajagundua kama ni kwa sababu ya diapers anazotumia. Siku alipogundua na kuacha mtoto wake hajaugua tena.
 
Nilikwisha weka bandiko humu kuhusu chanzo kikuu cha UTI nikitegemea dada zetu wa JF wangelitia maanani, lakini hadithi ni ile ile ya "sikio la kufa... ".

UTI kwa watoto ni matumizi yasiyo sahihi ya "pampers" (muda mrefu imechafuka kwa kinyesi na mkojo)na kwa watu wazima (hasa kina mama) ni kujitawaza kwa maji kusiko sahihi - nyuma mbele badala ya mbele nyuma, hivyo maji ya kinyesi kuingia njia ya mkojo.

WanaJF dada mko wapi, au tuwataje kwa majina ndo mtwambie "practice" zenu au za marafiki/majirani zenu. Ukimya ni dhahiri mmeguswa.
 
Wazungu sio wabaya. Kwao ''diapers'' zinatumika lakini kwa umakini. Sio kama huku kwetu unakuta mama anamvalisha mtoto anashinda nayo. Halfu hali ya hewa ya kwao ni tofauti na ya kwetu. Unakuta sehemu kama Dar joto ni kali lakini mtoto anavaa diaper masaa 24! Halfu quality ya diapers zao ni nzurii. BTW mwanzisha uzi kavulata asante sana. Umetoa elimu nzuri sana. Mimi nashauri kwa wenye watoto wadogo WASITUMIE kabisa hizi diapers. Kwanza nyingi zitatengenezwa na wachina uchochoroni hivyo hazina quality nzuri na zinakuwa contaminated. Pili mazingira ya kwetu hasa sehemu kama Dar ni ya joto sana. Nilikuwa na jirani yangu mtoto wake alikuwa haishi kuugua UTI. Alikuwa hajagundua kama ni kwa sababu ya diapers anazotumia. Siku alipogundua na kuacha mtoto wake hajaugua tena.
Shida pia uchumi wa wazazi haumudu kutumia diapers, hivyo ikifika jioni saa 12 utawaona wazazi wakimiminika madukani kwenda kununua piece moja tu ya diaper ambayo atamvalisha mtoto wake hiyohiyo moja usiku kucha illi yeye asisumbuke kuammshwa na mikojo na kinyesi cha mtoto wake. Hivyo mpaka asubuhi unakuta pampasi imetuna na kurura kwa mikojo na mavi ya mtoto ya usiku kucha, jamani jamani wazaziiiii, acheni kuwaaua watoto wenu kwa mikono yenu wenyewe na ushamba wenu
 
Umofa kwenu!!!!!!

Wakuu mbalimbali nimetatizwa na elimu tata juu ya hizi nepi za kizungu kwa kina la ''pambasi''

Mama mmoja amenikuta niko na mama yoyoo tunambadilisha dogo ''pampasi'' akasema msinichukie jamani lkn mnielewe, mnamuharibu mtoto wenu mzuri wa kiume.Kuwa hizo zinamadhara, mala mtoto atakuja kuwa hanithi etc.
Pia kuna kakilipu kanatembea mitandaoni kakionyesha hiyo makitu ikiwa inatoa funza.

Tuliheshimu maoni yake lakini hatukiyatekeleza kwa wema tu maana ratiba ya huyu dogo kuvaa papasi ni kwenye matukio tu ila siku zote anakula nepi.



wazazi mbalimbali na wajuvi wa mambo haya karibu tutoane tongotongo za maisha.
Kuuliza ni Akili.
 
Karne ya 21 na watu bado wana imani potofu kiasi hiki???

Ama kweli kumshinda adui ‘ujinga’ ni vita ngumu sana!!!
mkuu mama kaoshwa ubongo na mume wake kuwa huyo mume '' hiyo kitu kaifanyia ile wasomi wanaita TAFITI''.
mkuu hili ni tatizo pana, maana wengi wanahizi imani kichinichini. Wengine wanapinga hata mayumizi ya ''wipes'' eti nazo zinamadhara.

Weka elimu mkuu tukomboe jamii, nataka nimtakase ubongo huyo mbaba aliyemuosha ubongo mke wake, ila hakoswa nondo na ushawishi wa kutosha, maana huyo jamaa akiamini kitu unahitaji ushahidi na maelezo mazito kumsaidia aamini.
 
Mngemuuliza Pampas zimetengenezwa kwa materials zipi na madhara yake yanasababishwa na nini na kwanini?
Pamoja na hayo, kwa sababu za kiuchumi, na flexibility pampas siyo kitu cha kushindia kwa mtoto.
Pia Pampas inaweza kumchelewesha mtoto kujitambua kwenye kwenda haja. Inabidi ajisaidie kwenye nguo ili hata ninyi mstuke mapema na kumbadirisha au hata yeye aanze kukereka mapema.
Pampas zinalemaza or ku slow down watoto katika kujitambua pia zinalemaza wazazi/waangalizi
 
Scientifically, kila kitu kina madhara. Huwezi acha kutumia kisa assumptions.

Sent using Jamii Forums mobile app
duu!!!
Tatizo ni Je madhara yapo katika '' scientifically tolerable zone''.
Mfano Unahitaji makreti hamsini ya soda ili ulewe, lkn mtu anakuambia ukinywa ''fanta'' utalewa zaidi ya mtu aliyekunywa '' chupa kumi za konyagi''.
 
Back
Top Bottom