Je, nini kilimpoteza mwanamuziki Jim Sullivan baada ya kuimba kuhusu kutekwa na Aliens?

Je, nini kilimpoteza mwanamuziki Jim Sullivan baada ya kuimba kuhusu kutekwa na Aliens?

Da'Vinci

JF-Expert Member
Joined
Dec 1, 2016
Posts
35,812
Reaction score
107,628
Salute Comrades
Intro
Mnamo mwaka 1969 mwanamuziki aitwae Jim Sullivan alirekodi albamu aliyoipa jina la U.F.O, ndani ya albamu hiyo kuna mistari anaimba kua ..aliacha familia yake akawa ametekwa na aliens . Baada ya miaka sita gari lake lilikutwa shambani jangwani kwenye jiji la New Mexico mpaka leo hajapatikana wapi alipo.

Anaitwa James Antony Sullivan kazaliwa August 13 1940 katika eneo la san Diego jijini California marekani. Alikua muimbaji, mtunzi na mpiga gitaa.

Jinsi alivyopotea
Tarehe 4 march 1975 Jim Sullivan aliondoka jijini Los Angeles akielekea Nashville, alikua yeye peke yake ndani ya gari lake aina ya Volkswagen. Siku iliyofuata polisi wa patrol barabarani walimuonya kutokana na uendeshaji wake wa kasi hivyo akaona apumzike kwenye Motel ya La mesa eneo la santa rosa jijini New Mexico, lakini taarifa zingine zinasema hakulala hapo kwenye hiyo hotel, aliacha funguo kwenye mlango wa chumba cha hotel (ndani).

Siku iliyofuata gari lake lilikutwa umbali wa Maili 26 kwenye shamba lililokua linamilikiwa na familia ya Gennetti, na hakuna yoyote aliyemuona akitoka ndani ya hilo gari. Ndani ya gari lake kulikutwa Pesa,gitaa,karatasi, nguo na copy kadhaa za albamu yake. Hakuonekana tena mpaka leo watu wanasema kua labda aliuawa, au alipotea, wengine wanasema kua inawezekana ni kutokana na mambo aliyoimba ndani ya wimbo wa Allien abduction.

Kuna mwili pia ulipatikana maeneo ya shambani uliofanana na jim lakini hakua yeye hivyo mpaka leo hajaonekana wala hajulikani alipo.

Ndugu wana Jf je nanyi mwaona nini kitakua chanzo cha kupotea kwake?
Na kwa masrahi yapi labda mpaka wampoteze?

Msimamo wa mwandishi kuhusu Unidentified Flying Objects (UFO)
Mimi Da'Vinci naamini kua hakuna cha UFOs wala Allien, ni mkakati wa nchi kubwa kubwa kututisha tu wanadamu na kutu Brain wash tu. Ni mambo tu wanayotengeneza ili kuona dunia si sehem salama.
Vitu kama vile..
  • Ozone layer kutoboka
  • Virusi vya ukimwi
  • Kutuaminisha kua kuna mtu aliyewahi tokea anaitwa D.B Cooper wakati hajawahi kuwepo.
  • Kwamba kuna jiwe angani linakuja kwa kasi kuigonga dunia
  • Etc etc
Ahsante
Da'Vinci
 
Kuna mengi tusiyoyajua na wachache ndo wanaojua... haiwezekani mtu apotee na asijulikane alipo ingekua huku africa ningeamini maana wapelelezi wetu hawako makini,,, lkn huko kwa wazungu ni wazi kuna jambo tena kubwa
 
Hapa nilipo ndio namalizia kusoma Protocols of the Elder of Zion.. Wanachojitahidi kufanya wayahudi ni kufanya yale yalioandikwa 1905 kuwa halisi.. Wazungu nao huo ni mkakati wao wa kutuaminisha uongo....
 
Salute Comrades
Intro
Mnamo mwaka 1969 mwanamuziki aitwae Jim Sullivan alirekodi albamu aliyoipa jina la U.F.O, ndani ya albamu hiyo kuna mistari anaimba kua ..aliacha familia yake akawa ametekwa na aliens . Baada ya miaka sita gari lake lilikutwa shambani jangwani kwenye jiji la New Mexico mpaka leo hajapatikana wapi alipo.

Anaitwa James Antony Sullivan kazaliwa August 13 1940 katika eneo la san Diego jijini California marekani. Alikua muimbaji, mtunzi na mpiga gitaa.

Jinsi alivyopotea
Tarehe 4 march 1975 Jim Sullivan aliondoka jijini Los Angeles akielekea Nashville, alikua yeye peke yake ndani ya gari lake aina ya Volkswagen. Siku iliyofuata polisi wa patrol barabarani walimuonya kutokana na uendeshaji wake wa kasi hivyo akaona apumzike kwenye Motel ya La mesa eneo la santa rosa jijini New Mexico, lakini taarifa zingine zinasema hakulala hapo kwenye hiyo hotel, aliacha funguo kwenye mlango wa chumba cha hotel (ndani).

Siku iliyofuata gari lake lilikutwa umbali wa Maili 26 kwenye shamba lililokua linamilikiwa na familia ya Gennetti, na hakuna yoyote aliyemuona akitoka ndani ya hilo gari. Ndani ya gari lake kulikutwa Pesa,gitaa,karatasi, nguo na copy kadhaa za albamu yake. Hakuonekana tena mpaka leo watu wanasema kua labda aliuawa, au alipotea, wengine wanasema kua inawezekana ni kutokana na mambo aliyoimba ndani ya wimbo wa Allien abduction.

Kuna mwili pia ulipatikana maeneo ya shambani uliofanana na jim lakini hakua yeye hivyo mpaka leo hajaonekana wala hajulikani alipo.

Ndugu wana Jf je nanyi mwaona nini kitakua chanzo cha kupotea kwake?
Na kwa masrahi yapi labda mpaka wampoteze?

Msimamo wa mwandishi kuhusu Unidentified Flying Objects (UFO)
Mimi Da'Vinci naamini kua hakuna cha UFOs wala Allien, ni mkakati wa nchi kubwa kubwa kututisha tu wanadamu na kutu Brain wash tu. Ni mambo tu wanayotengeneza ili kuona dunia si sehem salama.
Vitu kama vile..
  • Ozone layer kutoboka
  • Virusi vya ukimwi
  • Kutuaminisha kua kuna mtu aliyewahi tokea anaitwa D.B Cooper wakati hajawahi kuwepo.
  • Kwamba kuna jiwe angani linakuja kwa kasi kuigonga dunia
  • Etc etc
Ahsante
Da'Vinci
mkuu heshima kwako kaka mkubwa..[emoji4] [emoji4]

Lakini mkuu kumbuka kuwa kifo cha huyu jamaa kimeleta utata mwingi sana kwa sababu aliwahi kuhukumiwa kifungo cha maisha kutokana na kesi ya kumuua mke wake wa pili na kupelekea Hatimaye kushtakiwa na mauaji ya mke wake mwaka 1998, alikimbilia Costa Rica, kisha Panama, Venezuela na hatimaye kwenda Thailand, ambapo alikamatwa mwaka 2002.

Alirejeshwa Atlanta kwa kesi, alihukumiwa mwaka 2006 na kuhukumiwa maisha ya gerezani.

Alikuwa na mwendesha mashtaka David Boone ambaye alikuwa anamtetea kwani inasemekana alifarakana na huyo mke wake wa pili.

Mke wake aliamua kumshitaki klkwani aliamini kuwa endapo kesi itafika mahakamani basi sehemu ya mali za Sullivan atapewa huyo mwanamke kwani alidai taraka.

Ndipo bwana James akamua kumtafuta jangili mmoja anaitwa Phillip Harwood na kumpa kiasi cha , $25,000 kumuua mke wake Lita Sullivan alipofungua mlango wa nyumba yake ya mji wa Atlanta ..


Lakini kutoka na kesi hiyo kuunguruma mahakamani kwani ilikuwa ni lazima James Sullivan ahukumiwe kifungo cha maisha lakini wakili wake alimtetea ambapo ilipelekea kukamatwa kwa yule jangili aliyelipwa pesa ndefu na kufungwa miaka 20 .

Lakini James alifungwa kifungo cha nje kwani wakili wake alimtetea kuwa alikuwa bado ana mawazo juu ya kifo cha mke wake hivyo hangeweza kuvumilia maisha ya gerezani ,.

kutokana na kuwa na mawazo ya kufiwa na mke wake au sijui alikuwa anafanya unafiki ndo akawa na mawazo ya hapa na pale na kupelekwa kujiua yeye mwenyewe shambani huko bila kumhusisha mtu..


shida ilikuwa ...... ni wapi mwili wake ulipotelea,..

Baadhi ya documentary zinasema kifo chake kinahusishwa na FBI waliokuwa wanamsaka kwa kuwa alikuwa na makosa mengi sana ikiwemo la kuimba nyimbo ambazo zilikuwa zinawapa hofu kubwa watu( Alliens and UFO) na kukimbiza gari hasa nyakati za usiku kwa kasi sana ..japo alipewa onyo lakini hakuiacha tabia ile..


Lkini pia inasemekana kuwa familia ya marehemu Lita ndo ilipanga njama za kulipiza kisasi kwa kumuua binti yao..hivyo na wao wakaamua kumpoteza bila ushahidi


Lakini documentary zingine zinasema jamaa aliuliwa na FBI kwani alianza kuzungumzia mambo ya mental abduction yaliyokuwa yanafanywa na Aliens kwa viongozi wastaafu katika serikali ya marekani kuhofia kutoa siri za uhusiano wa seeikali ya marekani na Viumbe toka sayari za mbali( Aliens)..


Lakini ushahidi mwingine unasema kuwa ilikuwa ni hofu yake ya kuogopa kifungo cha maisha hivo aliamua kujiua kwa kuwa alikuwa mkiwa aliyejaa hofu na roho ilikuwa inamsuta kwa kumuua mkewe...

Mpaka leo bado FBI wanaendelea na uchunguzi sijui watapata jawabu juu ya kupotea kwake..



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna mengi tusiyoyajua na wachache ndo wanaojua... haiwezekani mtu apotee na asijulikane alipo ingekua huku africa ningeamini maana wapelelezi wetu hawako makini,,, lkn huko kwa wazungu ni wawazi kuna jambo tena kubwa
Naam kiongozi ndio maana mimi hua naamini kua hakuna kitu kinachoitwa D.B. Cooper bali ni character tu kwenye story waliyotunga na kutuaminisha kua lilitokea.
Db cooper ni kama madenge he's never existed
 
Hapa nilipo ndio namalizia kusoma Protocols of the Elder of Zion.. Wanachojitahidi kufanya wayahudi ni kufanya yale yalioandikwa 1905 kuwa halisi.. Wazungu nao huo ni mkakati wao wa kutuaminisha uongo....
Naam kiongozi ni kua macho tu tunatishwa tu ili tuamini dunia si mahali salama. Ila si kweli mambo hayo yanatengenezwa tu
 
mkuu heshima kwako kaka mkubwa..[emoji4] [emoji4]

Lakini mkuu kumbuka kuwa kifo cha huyu jamaa kimeleta utata mwingi sana kwa sababu aliwahi kuhukumiwa kifungo cha maisha kutokana na kesi ya kumuua mke wake wa pili na kupelekea Hatimaye kushtakiwa na mauaji ya mke wake mwaka 1998, alikimbilia Costa Rica, kisha Panama, Venezuela na hatimaye kwenda Thailand, ambapo alikamatwa mwaka 2002.

Alirejeshwa Atlanta kwa kesi, alihukumiwa mwaka 2006 na kuhukumiwa maisha ya gerezani.

Alikuwa na mwendesha mashtaka David Boone ambaye alikuwa anamtetea kwani inasemekana alifarakana na huyo mke wake wa pili.

Mke wake aliamua kumshitaki klkwani aliamini kuwa endapo kesi itafika mahakamani basi sehemu ya mali za Sullivan atapewa huyo mwanamke kwani alidai taraka.

Ndipo bwana James akamua kumtafuta jangili mmoja anaitwa Phillip Harwood na kumpa kiasi cha , $25,000 kumuua mke wake Lita Sullivan alipofungua mlango wa nyumba yake ya mji wa Atlanta ..


Lakini kutoka na kesi hiyo kuunguruma mahakamani kwani ilikuwa ni lazima James Sullivan ahukumiwe kifungo cha maisha lakini wakili wake alimtetea ambapo ilipelekea kukamatwa kwa yule jangili aliyelipwa pesa ndefu na kufungwa miaka 20 .

Lakini James alifungwa kifungo cha nje kwani wakili wake alimtetea kuwa alikuwa bado ana mawazo juu ya kifo cha mke wake hivyo hangeweza kuvumilia maisha ya gerezani ,.

kutokana na kuwa na mawazo ya kufiwa na mke wake au sijui alikuwa anafanya unafiki ndo akawa na mawazo ya hapa na pale na kupelekwa kujiua yeye mwenyewe shambani huko bila kumhusisha mtu..


shida ilikuwa ...... ni wapi mwili wake ulipotelea,..

Baadhi ya documentary zinasema kifo chake kinahusishwa na FBI waliokuwa wanamsaka kwa kuwa alikuwa na makosa mengi sana ikiwemo la kuimba nyimbo ambazo zilikuwa zinawapa hofu kubwa watu( Alliens and UFO) na kukimbiza gari hasa nyakati za usiku kwa kasi sana ..japo alipewa onyo lakini hakuiacha tabia ile..


Lkini pia inasemekana kuwa familia ya marehemu Lita ndo ilipanga njama za kulipiza kisasi kwa kumuua binti yao..hivyo na wao wakaamua kumpoteza bila ushahidi


Lakini documentary zingine zinasema jamaa aliuliwa na FBI kwani alianza kuzungumzia mambo ya mental abduction yaliyokuwa yanafanywa na Aliens kwa viongozi wastaafu katika serikali ya marekani kuhofia kutoa siri za uhusiano wa seeikali ya marekani na Viumbe toka sayari za mbali( Aliens)..


Lakini ushahidi mwingine unasema kuwa ilikuwa ni hofu yake ya kuogopa kifungo cha maisha hivo aliamua kujiua kwa kuwa alikuwa mkiwa aliyejaa hofu na roho ilikuwa inamsuta kwa kumuua mkewe...

Mpaka leo bado FBI wanaendelea na uchunguzi sijui watapata jawabu juu ya kupotea kwake..



Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu umeandika story nzuri lakini nashindwa kufaham kama unamzungumzia Jim Sullivan kutokana na miaka hiyo. Yeye katoweka toka mwaka 1975 au mimi ndio sijaelewa
 
Wamarekani ni wabaya sana kuhusu propoganda kwa raia wake. Ukibahatika kuishi huko na ukaitrakti na watu wa kawaida ndio utalijua hilo. Wako ambao hatakuandika baadhi ya maneno ya lugha yao ni shida tupu. Hawajui kinacho endelea huko duniani nje ya marekani yao. Wameamimishwa kuwa USA ndio kila kitu. Utawaonea huruma kwa kweli. Kiufumbi ni mazombi flani kuhusu habari za dunia nje ya USA.
 
Wamarekani ni wabaya sana kuhusu propoganda kwa raia wake. Ukibahatika kuishi huko na ukaitrakti na watu wa kawsuda ndio utalijua hilo. Wako ambao hatakuandika baadhi ya maneno ya lugha yao ni shida tupu. Hawajui kinacho endelea huko duniani nje ya marekani yao. Wameamimishwa kuwa USA ndio kila kitu. Utawaonea huruma kwa kweli. Kiufumbi ni mazombi flani kuhusu habari za dunia nje ya USA.
Ni kweli haya unenayo???
Kuna ushahidi??
 
Kipimo/point tunachotumia ili kutambua kuwa kuna viumbe wenye ufahamu zaidi yetu

Si matukio ya ajabu ajabu yanayo endelea kutokea kwa watu duniani

Ila ni juu ya umaana kwa ujumla wa maisha

Yanayo onekana yana mitindo mingi yenye kustaajabisha.!

Lakini yasiyo na kusudi lenye mvuto

Inaonekana ainabinadamu inaishi kiutamaduni Tu

Yenye kudhihirisha ufahamu mchanga Mno katika welewa

Kulinganisha na utambuzi ambao kiumbe anao kuweza kusababu vitu_ni hilo Tu linalo tuchochea kuwa na shaka

NB:
Ni kwamba ufahamu wa viumbe umebaka umaana/kusudi la maisha kwa ujumla_Hilo tu

That why we say there is another hiden inteligent race than us

Who are capable for those dam things around

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom