Je nyumbani kwenu, walipo wazazi au ndugu zako, ni sehemu salama ambayo ukipigwa unaweza kukimbilia na kupata utulivu?

Je nyumbani kwenu, walipo wazazi au ndugu zako, ni sehemu salama ambayo ukipigwa unaweza kukimbilia na kupata utulivu?

Dogoli kinyamkela

JF-Expert Member
Joined
Nov 21, 2024
Posts
618
Reaction score
1,440
Je nyumbani kwenu, walipo wazazi au ndugu zako, ni sehemu salama ambayo ukipigwa unaweza kukimbilia na kupata utulivu kabla ya kurejea tena kwenye mapambano; Au ni heri ufie ugenini kuliko kuthubutu kurudi huko?

Kuna kitu nataka kufundisha kuhusu hili.
 
Somo No1.
Watu wengi kwenye familia zao hawajafundishwa upendo wala kuheshimiana. Kwenye familia kumejaa ugomvi na chuki, wazazi wana watoto wapendwa na wa nyongeza. Kuna watoto hata wafanye jema gani, inaonekana ni kama wanajipendekeza tu. Mzazi anaweza kumdanganya mtoto fulani ili atoe hela kwa ajili ya mtoto mwingine, mf. Mzazi anapiga simu na kudanganya kuwa anaumwa na anahitaji pesa ya matibabu, kumbe ameombwa pesa na mtoto wake mmoja mpendwa.

Familia nyingi watu wanashindana badala ya kusaidiana. Yaani mtu anajipima maendeleo kwa kujilinganisha na ndugu yake, akizidiwa kitu na ndugu yake, anaona kama dunia imemuangukia. Familia kama hii, ni heri kufia ugenini kuliko kukimbilia wakati wa shida maana wanaweza kufanya ukafa kwa msongo wa mawazo.
 
Mimi huwa naamini hivi kuwa nikishindwa ugenini basi siwez kufungwa nyumbani so all I do nikuwekeza ugenini .

Maana ukifungwa ugenini kutoboa nyumbani it is just luck.
 
Somo No.2
Kuna familia zile ambazo ukiwa na changamoto za kiafya wanahangaika upone usije ukafa. Unatakiwa kuishi mbwa wewe ili tuendelee kukuona unavyoteseka.😆😆

Hizi familia unaweza kushangaa, unapokuwa na changamoto ya kuhitaji kuvushwa, yaani ni kama hawakuoni na hata ukisema unalala na njaa wala hakuna anayejali.
 
Somo No.3
Watu wanatakiwa kufundishwa upendo na kuheshimiana kwa utu na siyo kwa vitu. Wazazi wanatakiwa kuwa mfano wa upendo kwa watoto na kila mtu ndani ya familia anatakiwa kufundishwa kuwajibika kwa nafasi yake. Heshima iwekewe mkazo ili kila mtu ajione ni wa muhimu na siyo wa nyongeza ili hata akiwa mbali, awe anakumbuka nyumbani na watu wake.
 
Somo No.4
Kuna watu wanajua kabisa kuwa hawapendwi kwenye familia zao, wanajua kuwa vitu walivyo navyo ndiyo vinapendwa na wazazi na ndugu zao, ikitokea vitu hivyo mfano mali au ajira vikaondoka basi na ule uhusiano na familia pia unakuwa ndiyo mwisho. Watu wa aina hii mara nyingi, wakiwa na shida, huona ni salama kukimbilia kwa marafiki kuliko nyumbani.
 
Somo No.5
Familia yoyote inayohitaji kuwa na msingi imara ni lazima iwe na uongozi unaoheshimiwa na unaojuheshimu. Kama ni baba ni lazima ajijengee heshima kwa watoto wake ili apate mamlaka ya kimaadili (moral authority) ya kuwafundisha watoto wake kuheshimiana. Upendo ufundishwe kwa vitendo, kila mtu afundishwe kuona thamani ya wenzake na kuvumilia madhaifu yao. Shida ya mwanafamilia isichukuliwe kwa mzaha, hata kama amekosea ni lazima atolewe kwenye shida kwanza halafu lawama itafuata baadae. Ieleweke kwamba heshima ya mwanafamilia ni heshima ya familia nzima kwa hiyo mwanafamilia anayejaribu kutafuta njia ya kuleta heshima, ni lazima asaidiwe na kila mtu kwa kila kilichopo.
 
Somo No.6
Kama umetoka kwenye familia isiyo na misingi, watu hawaheshimiani wala kupendana, watu wanashindana badala ya kusaidiana. Kama unahisi familia inakutumia kama kifaa kwa manufaa binafsi na hakuna anayejali kuhusu wewe, fanya hivi. Kwanza elewa kwamba, iwapo familia yako hawapendani, hiyo ni dalili kwamba watoto wako hawatakuwa na sehemu ya kukimbilia ikitokea haupo. Jitahidi kuhakikisha unatafuta mwenza anayetokea familia yenye hali tofauti na unayotoka wewe. Watoto wako wana haki ya kuonja ladha ya upendo angalau toka upande mmoja. Iwapo hawatawahi kuona upendo wa kindugu pande zote, hawataamini katika heshima, upendo na ushirikiano.

Usifanye makosa katika uchaguzi wa mwenza kwa sababu tayari una majeraha ya familia ulipotokea, ukiumizwa tena kwenye ndoa utakosa ladha na maana nzima ya maisha. Uchaguzi mzuri wa mwenza utakupa utulivu wa kuanzisha himaya mpya utakayoijenga kwa misingi yako na kufuta kumbukumbu za maumivu uliyopitia kwenye familia uliyotokea na utawafanya watoto wako na wajukuu kuishi katika misingi mizuri uliyoikosa.
Mwisho WA SoMo🙏🏽
 
Hawa majambazi wa CCM wanaoua waTANZANIA wenzao kila siku unadhani wanatoka familia zenye upendo, heshima na amani au ni kutoka familia za crooks ?
 
Back
Top Bottom