OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 53,868
- 121,001
Anaandika Wakili msomi Jonh Mallya,
Ni usiku wa manane. Lengai Ole Sabaya amelaza kichogo chake kwenye kiganja. Mwili wake ameulaza juu ya sakafu baridi akitazama dari la chumba cha mahabusu ambacho taa zake hazizimwi usiku-kucha.
Kelele za wenyeji zinamghasi, lakini hazimtoi kwenye lindi la mawazo, majuto na masikitiko. Anakumbuka alivyokua analala mahoteli makubwa bila kulipa. Anajua leo na siku nyingi zijazo hatolipia mahali pa kulala. Atalala bure.
Lakini wasiwasi wa kulawitiwa, kupigwa na wababe wa jela, kupewa adhabu na askari magereza na hofu ya kukutwa na hatia au kuongezewa mashtaka vinamnyima raha.
Anajuta na haoni tumaini mbele yake. Anamkumbuka mwendazake. Anatamani ajiunge nae, lakini hana fursa ya kufanya hivyo. Anajuta kwanini alizaliwa, lakini hawezi kulaumu wazazi wake. Anajuta kuteuliwa, lakini anajua kuna wenzake waliteuliwa na hawakufanya mabaya aliyofanya yeye.
Anajisikia dhalili. Amevaa sweta, lakini anahisi baridi. Yuko na watu wengi lakini anajihisi mpweke!
Anakumbuka mazungumzo yake na Godbless Lema, alivyomwambia aliyekuteua sio Mungu. Anatamani siku ijirudie aukubali ule ushauri wa Lema, lakini haiwezekani tena. Anajipa moyo huenda atashinda vita hii, lakini akitafakari haoni mwanga. Dunia nzima inajua ubaya wake.
Amechoka kulala kwa mgongo, anajaribu kugeuka alale kwa ubavu, lakini mtu wa pembeni yake ni mnene na anakoroma kwa nguvu. Anatamani apate angalau konyagi ndogo imsaidie kulala, lakini Kisongo ni gereza lenye ulinzi mkali. Hawezi kupata huduma hiyo kwa sasa.
Anawakumbuka viongozi waliokua marafiki zake. Anajipa moyo huenda wakamsaidia. Lakini anakumbuka nao wanatafuta uteuzi, hivyo hawawezi kusimama upande wake kwa sasa.
Anafumba macho kuzuia machozi. Anatamani apate usingizi alale ili mawazo yakatishwe, lakini wapi!
Anasikitika tena. Anailaani siku Mwendazake alipokufa. Anailaani siku aliyoenda Takukuru kwa wito wa barua. Analaani ndugu zake ambao hawakumshauri aache ubaya. Analaani marafiki zake waliokua wanamsifia na kumuita jembe.
Anainua mkono kutazama muda, lakini hakuna saa mkononi. Anakumbuka yuko jela na huko saa, mkanda na viatu haviruhusiwi.
Anajisonya kimoyomoyo,
Anajitukana, anajilaani.!
My Take
Sabaya ana kesi ya uhujumu uchumi,ubakaji na matumizi mabaya ya madaraka aliyofanya kipindi cha utawala wa Magufuli. Alifanya yote haya huku Wilaya na Mkoa ukiwa na vyombo vya ulinzi na usalama ikiwemo TISS. Walikuwa wapi?
Haya, Chadema walipiga kelele, Mbowe alipiga kelele, Lema akaonya. Mitandao ya kijamii ikaweka mambo hadharani. Lakini Rais aliyemteua hakufanya chochote. Akasema wewe chapa kazi.
Swali: Je Sabaya alipewa kibali cha kuhujumu uchumi?
Ni usiku wa manane. Lengai Ole Sabaya amelaza kichogo chake kwenye kiganja. Mwili wake ameulaza juu ya sakafu baridi akitazama dari la chumba cha mahabusu ambacho taa zake hazizimwi usiku-kucha.
Kelele za wenyeji zinamghasi, lakini hazimtoi kwenye lindi la mawazo, majuto na masikitiko. Anakumbuka alivyokua analala mahoteli makubwa bila kulipa. Anajua leo na siku nyingi zijazo hatolipia mahali pa kulala. Atalala bure.
Lakini wasiwasi wa kulawitiwa, kupigwa na wababe wa jela, kupewa adhabu na askari magereza na hofu ya kukutwa na hatia au kuongezewa mashtaka vinamnyima raha.
Anajuta na haoni tumaini mbele yake. Anamkumbuka mwendazake. Anatamani ajiunge nae, lakini hana fursa ya kufanya hivyo. Anajuta kwanini alizaliwa, lakini hawezi kulaumu wazazi wake. Anajuta kuteuliwa, lakini anajua kuna wenzake waliteuliwa na hawakufanya mabaya aliyofanya yeye.
Anajisikia dhalili. Amevaa sweta, lakini anahisi baridi. Yuko na watu wengi lakini anajihisi mpweke!
Anakumbuka mazungumzo yake na Godbless Lema, alivyomwambia aliyekuteua sio Mungu. Anatamani siku ijirudie aukubali ule ushauri wa Lema, lakini haiwezekani tena. Anajipa moyo huenda atashinda vita hii, lakini akitafakari haoni mwanga. Dunia nzima inajua ubaya wake.
Amechoka kulala kwa mgongo, anajaribu kugeuka alale kwa ubavu, lakini mtu wa pembeni yake ni mnene na anakoroma kwa nguvu. Anatamani apate angalau konyagi ndogo imsaidie kulala, lakini Kisongo ni gereza lenye ulinzi mkali. Hawezi kupata huduma hiyo kwa sasa.
Anawakumbuka viongozi waliokua marafiki zake. Anajipa moyo huenda wakamsaidia. Lakini anakumbuka nao wanatafuta uteuzi, hivyo hawawezi kusimama upande wake kwa sasa.
Anafumba macho kuzuia machozi. Anatamani apate usingizi alale ili mawazo yakatishwe, lakini wapi!
Anasikitika tena. Anailaani siku Mwendazake alipokufa. Anailaani siku aliyoenda Takukuru kwa wito wa barua. Analaani ndugu zake ambao hawakumshauri aache ubaya. Analaani marafiki zake waliokua wanamsifia na kumuita jembe.
Anainua mkono kutazama muda, lakini hakuna saa mkononi. Anakumbuka yuko jela na huko saa, mkanda na viatu haviruhusiwi.
Anajisonya kimoyomoyo,
Anajitukana, anajilaani.!
My Take
Sabaya ana kesi ya uhujumu uchumi,ubakaji na matumizi mabaya ya madaraka aliyofanya kipindi cha utawala wa Magufuli. Alifanya yote haya huku Wilaya na Mkoa ukiwa na vyombo vya ulinzi na usalama ikiwemo TISS. Walikuwa wapi?
Haya, Chadema walipiga kelele, Mbowe alipiga kelele, Lema akaonya. Mitandao ya kijamii ikaweka mambo hadharani. Lakini Rais aliyemteua hakufanya chochote. Akasema wewe chapa kazi.
Swali: Je Sabaya alipewa kibali cha kuhujumu uchumi?