Je, PSSSF wameingia kwenye mkondo wa Siasa au hawana pesa?

Mung Chris

JF-Expert Member
Joined
Sep 12, 2017
Posts
3,391
Reaction score
3,849
Nauliza swali hilo ni kwa sababu ndugu yangu aliwasilisha nyaraka za kustaafu miezi 3 kabla ya kustaafu rasmi na walizipokea wakasema kila kitu kimekamilika.

Sasa ameshastaafu ana miezi 5 sasa ukizingatia ofisi ya waziri ili tetea sana swala la wastaafu kulipwa pia Rais alisisitiza walipwe haraka.

Sasa swali linakuja; je, ilikuwa ni siasa tu majukwaani au kuwaonyesha wastaaafu kuwa wamebadilka kwa maneno na sio vitendo au ofisi kwa sasa haina fedha kwa ajili ya wataafu kwa sasa.

Hata simu hajapigiwa kuwa labda kuna mabadiliko au kuna kitu unatakiwa urekebishe.

Sijaelewa kabisa
 
Suala ni ufuatiliaji tu. Bongo urasimu umeshamiri kila idara
 
Website yao tu imedukuliwa..hakuna secured connection
 
Toa rushwa mkuu vinginevyo mtakesha! Hiyo taasisi inaongoza kwa kuomba rushwa!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…