Tetesi: Je, Rais Magufuli anaondoa mifumo ya kitaasisi na kuweka mifumo-watu?

Tetesi: Je, Rais Magufuli anaondoa mifumo ya kitaasisi na kuweka mifumo-watu?

CWR2016

JF-Expert Member
Joined
Dec 14, 2017
Posts
2,773
Reaction score
6,349
Habari wana JF...

Kuna mambo yanaendelea ktk nchi hii ni makubwa na ya ajabu.
Yasiposemwa huko mbele hatutaweza kupona kama Taifa.

Mnaweza mkachagua kunyamaza ila gharama ya kuja kurekebisha haya mambo ikawa kubwa sana.

Mabadiliko ya kisheria yanayoendelea Tz tena kwa "Hati za dharura" yanaondoa kabisa mifumo ya kitaasisi na kuotesha mifumo-watu.

Moja, Sheria ya Vyama vya siasa ikamfanya Mtu mmoja aitwaye "Msajili wa Vyama vya Siasa" kuwa mwamuzi wa kila kitu juu ya masuala yote ya vyama kuanzia madai hadi jinai.
Yani leo kwa sheria ile "Msajili" anaweza kuamua chochote juu ya chama na hata ikiwa ni kwa hisia tu.
Kwa wenye busara huko nyuma, makosa yote yalipelekwa ktk mahakama ambapo ushahidi pasi na shaka pande zote ulihitajika ili kuhukumu.
Leo "Msajili" tu anatosha kusema, mfano, 'Ktk kikao cheni mlimualika mgeni bila ruhusa yangu, nawafungia kufanya vikao miezi sita'.
Ule mfumo mpana wa kimahakama, umemezwa na mtu-MSAJILI.

Mbili, Ipo sheria pendekezwa (muswada) sasa ya vyama vya kijamii na asasi za kiraia. Na kwenyewe kuna Mtu msajili ambae anakuwa ktk Wizara ya Mambo ya ndani amepewa manguvu ya kuamua kwa uoni/utashi wake.

Yani huyu msajili akihisi kuna jinai anakufutilia mbali. Ni HISIA tu, au hata akiambiwa tu. ANAFUTA.
Haina kubisha. Ndio ana mamlaka hayo. Si mahakama wala nini. Ni Yeye Mtu-Msajili.

Na hawa wote ni Wateule wa Rais. Na Yeye Rais anaweza kuwatengua wkt wowote.
Nadhani mnauona mfumo mtu hapo.

Tatu, hii ndio funga kazi. Upo muswada unaopendekeza kuanzishwa kwa "Ofisi ya kushughulikia Malalamiko ya walipa kodi" chini ya Wizara ya Fedha.

Huu ni mfumo-mtu. Kama wabunge wetu wana akili wasipitishe hiki kitu. Kiufupi, mfumo wa kushughulikia malalamiko na madai ya kikodi upo mpaka sasa tena kisheria kabisa. Ambacho wabunge wangeweza fanya ni kuuboresha. Mfano kuangalia gharama na urahisi wa kila mfanyabiashara kuufikia.

Unaachaje mfumo wa kisheria wa kusuluhisha mapingamizi na malalamiko ya kodi!!!!, unaenda kuweka dawati kwenye wizara eti lishughulikie malalamiko ya wafanyabiashara Tanzania nzima?!!

Je, ni lini mfanyabiashara ataenda kulalamika wizarani??. Je, ule mfumo wa TRA kushtakiwa kwenye mabaraza na bodi za rufani za kodi, hadi Mahakama ya Rufaa unakufa??

Sasa atawekwa mtu (mfumo-mtu) pale Wizarani na atasikiliza vilio vya wafanyabiashara na kuamua.
Je, wasipokubaliana hapo, wanaenda wapi??
Kiufupi TRA inaenda kumezwa, Bodi na Mabaraza ya Rufani za kodi vinenda kumezwa pia.
Sasa kodi itakadiriwa na kulipwa pale kwenye dawati la Wizara ya Fedha. Simple!

Kwa nini mifumo-watu inapendwa sana na JPM kuliko Taasisi?

Endeleeni kutafakari...
 
Dingilai jiwe anatuonesha ubovu wa katiba yetu wacha ayavurunde bt ataingia tu kwenye kumi na nane za watanzania then watamnyonyoa kisha tutarekebisha makosa yetu alafu tutaanza safari ndefu ya kuikimbiza Brazil kiuchumi
 
Wako busy wanasherekea ndege na SGR. Zitakapo kosa wa kusafirishwa hawa hawa wataongozana barabarani kung'oa.
Tatizo letu wa Afrika tuko reactive sana. Tunasubiri mpaka yatukute ndo kelele zianze.
Mfano, Kikotoo- Kabla ya sheria kupitishwa kuna watu humu walisema sheria itakuwa na madhara, hawakuungwa mkono. Walipoambiwa sasa inaanza kazi kelele zikaanza. Tayari mamilioni yamepotea kwenye vikao yangetumika kwenye mambo mengine. Halafu inaonekana mmefanyiwa huruma wakati ni stahiki yenu

Sheria ya bodi ya mikopo- hapa kuna vijana 3 tu walienda mahakamani sijui na wao yaliwapata wapi. Sasa imeanza kutekelezwa mwaka wa pili kelele zinaanza. Wengi tunapuuza.

Kwa uzoefu wangu hii sheria itapita.
Tena watakaolalamika baadaye ni watumishi wa serikali wakiona hizo NGO zimefungwa na wao posho za blah blah wanakosa. Sasa watakaa kimya.

Ya wanasiasa, 2020 tu tuwasikia wakikatwa wakaanza kutapatapa.
Wakati sasa wanapiga kelele za ndiyo

Kwa tabia hii tuendako si salama.
Hapo juu Ethiopia pamoja na ndege na reli bora umaskini umewang'ang'ania kwa kuendekeza haya mambo.
 
Aendee zaidi ya hapa ili akili zikae sawa.

Wenye akili na uwezo wa kuona mbali walionya tangu 2016/2017 ila wajinga wengi hawakuelewa sasa wacha waelewe kwa vitendo.
Ashafikisha Taasisi na Taifa pabaya. Anazimeza Taasisi zote halafu watu wanajifanya hawaoni. Hakuna nchi ilifanikiwa kwa mfumo-watu.
 
Nasema hivi na bado tutulie kimya dawa iingine kunako.................... wakati tunaambiwa tumejengee UKUTA mliona wana siasa ni wachochezi wakati mnaambiwa tuna rais wa ajabu haijawahi tokea mliona ametumwa na mabeberu, wakati tunaambiwa akimaliza na sisi atakuja kwenu mliona kama huyu hajui asemalo matokeo yake akazawadiwa risasi..... Na bado tulipoambiwa nchi kapewa mshamba hatu
 
Nasema hivi na bado tutulie kimya dawa iingine kunako.................... wakati tunaambiwa tumejengee UKUTA mliona wana siasa ni wachochezi wakati mnaambiwa tuna rais wa ajabu haijawahi tokea mliona ametumwa na mabeberu, wakati tunaambiwa akimaliza na sisi atakuja kwenu mliona kama huyu hajui asemalo matokeo yake akazawadiwa risasi..... Na bado tulipoambiwa nchi kapewa mshamba hatu
Naogopa sana maana hata zile taasisi kubwa/nzito zimeanza kufungwa kamba. Tuamke, tukatae kabla hatujavunja ukuta
 
Je, ni lini mfanyabiashara ataenda kulalamika wizarani??. Je, ule mfumo wa TRA kushtakiwa kwenye mabaraza na bodi za rufani za kodi, hadi Mahakama ya Rufaa unakufa??

Sasa atawekwa mtu (mfumo-mtu) pale Wizarani na atasikiliza vilio vya wafanyabiashara na kuamua.
Je, wasipokubaliana hapo, wanaenda wapi??

Kiufupi TRA inaenda kumezwa, Bodi na Mabaraza ya Rufani za kodi vinenda kumezwa pia.
Sasa kodi itakadiriwa na kulipwa pale kwenye dawati la Wizara ya Fedha. Simple!

Kwa nini mifumo-watu inapendwa sana na JPM kuliko Taasisi?

Endeleeni kutafakari...

Siyo dalili njema!
Ikiunganisha na mswada wa dharura uliopo Bungeni kwa sasa unaweza kuona picha ukutani!
 
Naogopa sana maana hata zile taasisi kubwa/nzito zimeanza kufungwa kamba. Tuamke, tukatae kabla hatujavunja ukuta


Kabisa watu mtamwelewa pia Mange Kimambi tuko kwenye giza nzito sana hatujui tutajinasua kwa namna gani................. ni shida isiyokuwa na kipimo kwa kweli. Na tutakuwa Zimbabwe watakuwa na nafuu najua mashirika yamefungwa sio moja kwanza walianza kwa kuwanyima vibali vya kufanya kazi nchini kwenye sekta binafs hata wale wakujitolea ...
 
Kabisa watu mtamwelewa pia Mange Kimambi tuko kwenye giza nzito sana hatujui tutajinasua kwa namna gani................. ni shida isiyokuwa na kipimo kwa kweli. Na tutakuwa Zimbabwe watakuwa na nafuu najua mashirika yamefungwa sio moja kwanza walianza kwa kuwanyima vibali vya kufanya kazi nchini kwenye sekta binafs hata wale wakujitolea ...
Sisi tuna kazi sana mbele.
 
Ukishaona kiongozi anahubiri uzalendo na anahakikisha watu wote wanaamini uzalendo ni matendo yake, na hapo hapo hataki katiba yenye maoni ya watu, tena anaongea hivyo hadharani, hapo ujue kuna balaa kubwa. Matokeo yake hataki katiba mpya, lakini anahakikisha utashi wake ndio unageuzwa kuwa sheria na watu wako kimya, katika mazingira hayo ujue siku wananchi watataka kutoka kwenye hizo sheria basi damu lazima imwagike.
 
KaZijua akili za waTz kuwa hawawezi lolote ndio maana anafanya yale ayaonayo na bunge letu si la kuhoji hasa kwa wengi hivyo tutarajie mengi zaidi
 
hiyo ni moja ya sifa za authoritarianism, ana hulka ya udikteta na kiongozi mbovu!
 
Wabunge ndio wawakilishi wetu wakishaamua kunengua na kuitikia kila wimbo "ndiyooo...." huku wanaopinga upuuzi wakiitwa wasaliti na kufukuzwa bungeni...
Kazi tunayo...
 
Serikali ya Ccm ni Ovu, dhaifu na ya hovyo kuwahi kutokea toka tupate uhuru?

"Mith 28:1 "Waovu hukimbia ingawa hakuna yeyote anayewakimbiza, lakini waadilifu wana ujasiri kama simba"

Serikali ya Ccm chini ya Magufuli

1.Imeshindwa kuwawezesha wakulima kupata pembejeo kwa bei nafuu na kuwapatia masoko ya uhakika wa mazao yao.

2.Wafanyabiashara wamebanwa na kodi za kubambikiziwa

3.Hakuna ajira mpya

4.Wafanyakazi wamebanwa hakuna nyongeza ya mshahara

5. Vyama vya siasa vimebanwa kufanya siasa

6. Watu wanatekwa na kuuawa hakuna mtu aliyekamatwa walakushutumiwa

7. Manunuzi yote yanafanywa na raisi mwenyewe

8 Serikali imejitoa OPEC

9. Miswaada zaidi ya kumi imepelekwa Bungeni ndani ya kipindi cha miaka mitatu tu miswaada hiyo imelenga:

1 Kubana uhuru wa kutoa maoni
2 Kutisha watu
3 Kuzuia Vyama vya upinzani kufanya siasa
4 Kuzuia uwazi katika uendeshaji wa serikali

Narudia tena kuuliza swali je serikali ya Ccm chini ya Magufuli ni Ovu, dhaifu na ya hovyo kuwahi kutokea?
 
Back
Top Bottom