MWATANI
Member
- Feb 14, 2014
- 45
- 44
Salaam Wana JamiiForums,
Naanza andiko hili fupi kwa marejeo ya usemi usemao " Myonge Myongeni lakini haki yake mpeni" ni usemi wenye maana Pana kimantiki, Sasa ni miaka miwili ya Rais Samia tangu ashike hatamu ya uongozi wa nchi, amefanya mengi hata ambayo wahafidhina ndani ya CCM na nje ya chama hawakutarijia.
Demokrasia na mifumo ya utawala Bora imeshika Kasi, uhuru wa maoni, na uhusiano chanya wa kidiplomasia unavutia na kufungua fursa za kiuchumi, Vyama shindani au upinzani wanapumua katika siasa za uwiano sawia.
Aidha Rais Samia ni binadamu inawezekana anayo mapungufu yake kama walivyo binadamu na watawala wengineo, lakini hadi sasa Rais Samia anastahili kupewa alama za utendaji bora zisizopungua 95% Kwa uongozi uliotukuka na wenye dira ya kitaifa na kimataifa. Je, anastahili kutambuliwa Kwa uongozi Bora na kupewa tuzo ya Mo Ibrahim?
Nawasilisha.
Naanza andiko hili fupi kwa marejeo ya usemi usemao " Myonge Myongeni lakini haki yake mpeni" ni usemi wenye maana Pana kimantiki, Sasa ni miaka miwili ya Rais Samia tangu ashike hatamu ya uongozi wa nchi, amefanya mengi hata ambayo wahafidhina ndani ya CCM na nje ya chama hawakutarijia.
Demokrasia na mifumo ya utawala Bora imeshika Kasi, uhuru wa maoni, na uhusiano chanya wa kidiplomasia unavutia na kufungua fursa za kiuchumi, Vyama shindani au upinzani wanapumua katika siasa za uwiano sawia.
Aidha Rais Samia ni binadamu inawezekana anayo mapungufu yake kama walivyo binadamu na watawala wengineo, lakini hadi sasa Rais Samia anastahili kupewa alama za utendaji bora zisizopungua 95% Kwa uongozi uliotukuka na wenye dira ya kitaifa na kimataifa. Je, anastahili kutambuliwa Kwa uongozi Bora na kupewa tuzo ya Mo Ibrahim?
Nawasilisha.