Je, Rais wa Yanga Hersi Said anaweza kuwa ni mwanafunzi wangu wa soka?

Je, Rais wa Yanga Hersi Said anaweza kuwa ni mwanafunzi wangu wa soka?

SAYVILLE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
7,895
Reaction score
12,975
Unajua humu ndani tunachukuliana poa sana labda kwa sababu ya hizi ID feki. Kuna madogo ambao wanatakiwa wakupe heshma iliyotukuka ila kwa kuwa tunakutana katika nyuzi za soka tunachukuliana wote hamnazo.

Miaka fulani nikiwa bado bwa mdogo nilishajijengea heshima fulani mitaani ya kusakata kandanda. Kulinganisha na umri wangu, nilikuwa serious sana na mpira. Ndiyo maana huwa nabaki nacheka nikianza kubishana na baadhi ya watu kuhusu mambo ya soka halafu unasikia wananiambia "mpira haujui". Hahaha! Nilikuwa na kitabu changu naweka kumbukumbu za mechi nilizocheza na magoli niliyofunga. Watu tumeanza kufuatilia mipira ya South Amerika huko na Italy kitambo sana na siyo kwenye magazeti, nia kuiba maujuzi na mautundu na kuupeleka uwanjani.

Muda fulani ukafika nikawa kama nimestaafu hivi pamoja na kwamba umri wangu ulikuwa bado mdogo. Pia nikawa kama nimeanza kuwa serious hivi na mambo ya shule.

Mzee mmoja akanifuata akaniambia amenifuatilia kwa muda mrefu na anauelewa umahiri wangu dimbani. Akaniomba nifundishe madogo ambao kiumri hatukuwa tunazidiana sana. Kwa heshma yake nikachukua hilo jukumu. Kulikuwa na watoto wasiopungua 20 nikaanza kuwafundisha A, B na C za soka. Nilikuwa nachukua hadi vitabu vya kufundishia mifumo ya soka nasoma ili kujiongeza, halafu naenda kuwapa madini madogo. Masuala ya "total football" watu tunayajua kitabuni hadi kivitendo. Kitaa nilikuwa legend halafu nilikuwa hata siringi.

Nimefuatilia historia ya hapa na pale ya Rais wa Yanga, Hersi Said. Kwa taarifa nilizopata za alipokuwa anaishi, kuna uwezekano wa asilimia 85 hadi 90 kuwa alikuwa ni miongoni kwa hawa madogo.

Vijana wengi wa maeneo alipokulia huyu Rais wa Yanga nimecheza nao sana mpira. Tulikuwa timu tofauti ila tumekutana katika mechi nyingi za kiushindani na wengi walikuwa washkaji. Majina ya wengi yamenitoka ila baadhi naweza kuwataja hapa ili kuhakiki ninayosema.

Kuna watu unaowaheshimu wanantambua na wananiheshimu.
 
Ni kama mimi nikiwaambia humu nimecheza mechi za chuo dhidi ya kina Ali Mayay Tembele, kuna watoto watapinga! Maana miaka hiyo wakati nacheza dhidi yao mechi za ushindani, wenyewe walikuwa bado wananyonya!

Nikiwaambia nimecheza kombe la Muungano Mufindi miaka hiyo na baadhi ya mastaa waliowahi kucheza ligi kuu, hata hawataamini! Imagine mpaka Wahehe wa kule Iringa walifikia mpaka hatua ya kunizawadia mke (Segito)!!

Nilikuwa nafunga sana magoli enzi zile kabla ya kuhamia kwenye taaluma ya ukocha na baadaye ulinzi wa jadi, niliodumu nao kwa miaka mingi.
 
Ni kama mimi nikiwaambia humu nimecheza mechi za chuo dhidi ya kina Ali Mayay Tembele, kuna watoto watapinga! Maana miaka hiyo wakati nacheza dhidi yao mechi za ushindani, wenyewe walikuwa bado wananyonya!

Nikiwaambia nimecheza kombe la Muungano Mufindi miaka hiyo na baadhi ya mastaa waliowahi kucheza ligi kuu, hata hawataamini! Imagine mpaka Wahehe wa kule Iringa walifikia mpaka hatua ya kunizawadia mke (Segito)!!

Nilikuwa nafunga sana magoli enzi zile kabla ya kuhamia kwenye taaluma ya ukocha na baadaye ulinzi wa jadi, niliodumu nao kwa miaka mingi.
Ubaya watabisha lakini mimi nakufahamu comrade panenka umezipiga sana nakumbuka
 
Shida ya wazee uwa ni hiyo yaani haipiti siku hawajaanza kuwadaganya vijana .

Mara nilikuwa star Mara nilikuwa nyota yaani kikubwa wajioneshe walikuwa na mafanikio ilihali hawana chochote .

Niko umalila kila mzee unayeongea naye hasiti kusema mkuu wa majeshi mstaafu bwana Mboma alikuwa rafiki yake kabla ya kuingia jeshini ilihali historia haioneshi Mboma kusoma Wala kuwepo kwao Santilya umalila kipindi Cha mchakato wa maisha yake .

Ni hapo nawiwa kuwaasa wazee wote kwenye hii nchi waache uongo Mara moja la sivyo tutarudi kule kwenye kuwaita wachawi maana mmezidi kamba bwana
 
Ni kama mimi nikiwaambia humu nimecheza mechi za chuo dhidi ya kina Ali Mayay Tembele, kuna watoto watapinga! Maana miaka hiyo wakati nacheza dhidi yao mechi za ushindani, wenyewe walikuwa bado wananyonya!

Nikiwaambia nimecheza kombe la Muungano Mufindi miaka hiyo na baadhi ya mastaa waliowahi kucheza ligi kuu, hata hawataamini! Imagine mpaka Wahehe wa kule Iringa walifikia mpaka hatua ya kunizawadia mke (Segito)!!

Nilikuwa nafunga sana magoli enzi zile kabla ya kuhamia kwenye taaluma ya ukocha na baadaye ulinzi wa jadi, niliodumu nao kwa miaka mingi.
Ali mayayi nilikua nae chuo,alikua rais wetu mwaka wa pili,kumbe umesoma kipindi hicho!?.. anyway mi nilichelewa tu kufika chuo,mayai asingenikuta japo kwangu ni mkubwa
 
Ali mayayi nilikua nae chuo,alikua rais wetu mwaka wa pili,kumbe umesoma kipindi hicho!?.. anyway mi nilichelewa tu kufika chuo,mayai asingenikuta japo kwangu ni mkubwa
Nilikuwa najiendeleza tu mkurugenzi ili kuongeza kidogo maarifa kichwani. Ndiyo tukawa tunakutana kwenye mechi za kirafiki, na pia mashindano ya chuo. Kama unavyofahamu elimu haina mwisho.
 
Shida ya wazee uwa ni hiyo yaani haipiti siku hawajaanza kuwadaganya vijana .

Mara nilikuwa star Mara nilikuwa nyota yaani kikubwa wajioneshe walikuwa na mafanikio ilihali hawana chochote .

Niko umalila kila mzee unayeongea naye hasiti kusema mkuu wa majeshi mstaafu bwana Mboma alikuwa rafiki yake kabla ya kuingia jeshini ilihali historia haioneshi Mboma kusoma Wala kuwepo kwao Santilya umalila kipindi Cha mchakato wa maisha yake .

Ni hapo nawiwa kuwaasa wazee wote kwenye hii nchi waache uongo Mara moja la sivyo tutarudi kule kwenye kuwaita wachawi maana mmezidi kamba bwana
Nikae nitunge stori ya namna hii ili iweje? Kwa ajili ya kupata likes? Miaka kama 4 iliyopita nilianza harakati za kumtafuta yule mzee maana alikuwa anatupiga sana picha nikaambiwa alishafariki.

Kwani Mboma ndiyo nani? Unadhani kila aliyesoma na Mboma alitoboa au alikuja kuwa maarufu hadi ushangae ukikutana na mzee huko Umalila anayesema alisoma naye? Nadhani maisha haujayajua bado.

Watu tuna historia zetu, zingine dunia inajua zingine tunaishi nazo mioyoni, zingine bado tunazisuka labda kuna siku utasoma vitabu vyetu. Hizi ID fake zisikuchanganye.
 
Unajua humu ndani tunachukuliana poa sana labda kwa sababu ya hizi ID feki. Kuna madogo ambao wanatakiwa wakupe heshma iliyotukuka ila kwa kuwa tunakutana katika nyuzi za soka tunachukuliana wote hamnazo.

Miaka fulani nikiwa bado bwa mdogo nilishajijengea heshima fulani mitaani ya kusakata kandanda. Kulinganisha na umri wangu, nilikuwa serious sana na mpira. Ndiyo maana huwa nabaki nacheka nikianza kubishana na baadhi ya watu kuhusu mambo ya soka halafu unasikia wananiambia "mpira haujui". Hahaha! Nilikuwa na kitabu changu naweka kumbukumbu za mechi nilizocheza na magoli niliyofunga. Watu tumeanza kufuatilia mipira ya South Amerika huko na Italy kitambo sana na siyo kwenye magazeti, nia kuiba maujuzi na mautundu na kuupeleka uwanjani.

Muda fulani ukafika nikawa kama nimestaafu hivi pamoja na kwamba umri wangu ulikuwa bado mdogo. Pia nikawa kama nimeanza kuwa serious hivi na mambo ya shule.

Mzee mmoja akanifuata akaniambia amenifuatilia kwa muda mrefu na anauelewa umahiri wangu dimbani. Akaniomba nifundishe madogo ambao kiumri hatukuwa tunazidiana sana. Kwa heshma yake nikachukua hilo jukumu. Kulikuwa na watoto wasiopungua 20 nikaanza kuwafundisha A, B na C za soka. Nilikuwa nachukua hadi vitabu vya kufundishia mifumo ya soka nasoma ili kujiongeza, halafu naenda kuwapa madini madogo. Masuala ya "total football" watu tunayajua kitabuni hadi kivitendo. Kitaa nilikuwa legend halafu nilikuwa hata siringi.

Nimefuatilia historia ya hapa na pale ya Rais wa Yanga, Hersi Said. Kwa taarifa nilizopata za alipokuwa anaishi, kuna uwezekano wa asilimia 85 hadi 90 kuwa alikuwa ni miongoni kwa hawa madogo.

Vijana wengi wa maeneo alipokulia huyu Rais wa Yanga nimecheza nao sana mpira. Tulikuwa timu tofauti ila tumekutana katika mechi nyingi za kiushindani na wengi walikuwa washkaji. Majina ya wengi yamenitoka ila baadhi naweza kuwataja hapa ili kuhakiki ninayosema.

Kuna watu unaowaheshimu wanantambua na wananiheshimu.
Teh teh, uwe unatrain wanafunzi 20 halafu usiwajue majina? Kama huyo Hersi ulimfundisha usingebabaika kusema inawezekana alikuwa mwanafunzi wako!!
Kiufupi hata mpira huujui!
 
Back
Top Bottom