Je, tukemee udini, ukanda na ukabila au? Je, neno Sukuma Gang si neno la kibaguzi? Mnaonaje tukiungana kukemea ubaguzi wowote kwa jina lolote?

Huyo fisadi mwenyewe asingekua Rais kama sio kufariki kwa Mwalimu, mtazamo wa Nyerere ulikua ni pamoja na kumkataa huyo chekibobu tapeli
 
Tatizo la Ubaguzi wa Ukanda na Ukabila lilianza kipindi cha mwenda zake huyu ndo chanzo cha haya yote ku exaggerates watu wa kabila lake tu ndo wanaojua na kuwapa fursa ya ajira na ndo hv hv kwa Bibiye na hata Rais Mwingine ajaye yani amin kwamba yanayoendelea yaliasisiwa na Jiwe na kamwe hayatakaa yaishe Hii dhambi itatafuna hili Taifa
 
Naungana na mleta mada.

Binafsi sijawahi kulitumua hilo neno iwe positively au negatively. Watumiaji wa neno hili wanasema haliashirii kabila bali itikadi. Lakini hata kama linaashiria itikadi, uwepo wa neno linalotaja kabila, tayari umeleta hisia za ukabila.

Makosa au wema wa mtu usihusishwe na kabila lake, labda kama tendo lililofanywa na mhusika ni sehemu ya mila, tamaduni na desturi za kabila lake. Kama mtu hafai, basi atajwe yeye kwa sifa zake mbaya kuwa hafai.

Siku za huko nyuma, nilipokuwa nafanya masomo yangu ya shahada ya kwanza pale UD, kulikuwa na kawaida watu wa mkoa fulani au wilaya fulani kuwa na aina fulani ya umoja. Baadaye wengine walienda mbali zaidi na kufanya umoja huo kuashiria kabila.

Mathalani, tunajua wakazi wengi wa wilaya ya Kibosho ni wakibosho, Mwanga ni wapare, Bariadi ni wasukuma wanaojiita wanyantuzu, sasa wakatokea baadhi ya wanachuo, kwa mfano badala ya kuwa na umoja wa watu watokao Kibosho, wakataka kuwepo umoja wa wakibosho, au badala ya umoja wa wanachuo watokao Bariadi, wangetaka uwepo umoja wa wanyantuzu, n.k.

Chuo kilipiga marufuku. Kwa sababu moja tu kwamba hata kama wakazi wengi wa Kibosho ni wakibosho, ni ubaguzi kuwa na umoja wa Wakibosho kwa sababu itaashiria kwamba kama kuna wanyamwezi wanaoishi Kibosho hawatakuwa na sifa ya kuwemo kwenye umoja huo, sawa na kama ukiwa unatoka Bariadi lakini wewe siyo mnyantuzu, utakuwa huna sifa ya kuwepo kwenye umoja wa wanyantuzu.

Tujiepushena fikra zinazoibua hisia za ubaguzi wa kilabila. Makabila yetu yabakie kwenye utani wetu wa asili lakini siyo kututenga kwa lolote.

Kama mtu ana viashiria vya ubaguzi wa aina yoyote hafai kuwa kiongozi.
 
Bibi tozo yeye ni mdini wa waziwazi
 
Kuna usemi wa kiswahili unasema (watendewao.....)
Nchi hii hasa kule Zanzibar Muarabu anaonekana kama ni dosari. Akigombea Uongozi mtu mwenye asili ya Kiarabu utasikia ataleta Utumwa na kuwarudisha waarabu.Kwa kauli hii inamkosesha kuungwa mkono na kupoteza haki yake.
Nakumbuka Dr.Salim Ahmed Salim alipotaka kugombea Uraisi kule ZNZ
Pia nakumbuka. Wawekezaji wakiwa waarabu nchi hii inaonekana kama Dhambi.
na mambo yafananyo na hili.
Huu mbona Tuliunyamazia?
 
Makabila ya kishamba kwa ukabila wahaya, wachaga , wasukuma na wanyakyusa ndo kwa sana ushamba mzigo...
 
Sukumagang ni ITIKADI iliyoasisiwa na Lucifer JPM kwa manufaa ya wasukuma ukiwemo wewe Paskali Njalah Mayala, na kwa faida yako hilo vuguvugu la Sukumagang bila Mungu kuingilia ugomvi lingetupeleka pabaya kama taifa!

Wasukuma kama hilo ni tatizo fanyeni kazi ya kulifuta maana hata wewe hujawahi kulishutumu huko nyuma!
 
Minja ila nyinyi ule ubaguzi wenu wa enzi za Mramba waziri wa Fedha,wizara yote 80% Wachaga,Kitillya C.General TRA 80% Wachaga,Kimei CRDB,80% Wachaga huioni? Ukiamua kukemea ukabila kemea kweli kweli na uanze na kutoa boriti kwenye jicho lako kwanza.Makabila mengine walau wanaweza kuongea kuhusu ukabila lakini siyo Wachaga maana tuna mifano halisi pia.
 
Very objective comment
 
Mafisadi yanajali basi kanda ya ziwa ina majimbo mangapi?

Miaka miwili ya Magufuli mmbunge aliekwenda ni Kalemani peke yake hata huyo Mpina mnaemwita ‘sukuma gang’ ajafika.

Waanzilishi la hilo neno ni genge la wahuni tu, lakini humo ndani mwao likitokea fisadi wanaloelewana nalo awatojali dini wala kabila lake; mradi yao yaende watalipa tu nchi.

Sukuma gang ni Twitter na JF tu ndio wanayo promote hiyo dhana mafisadi yanajua hakuna kitu kama icho mtaani.

Yupo msukuma mmoja ana nafasi serikalini nyuma ya pazia jamaa ukimtajia Magufuli anaweza tapika ataki ata kulisikia hilo jina sijui aliwafanya nini serikalini.
 
Ukiacha Kigogo ambaye naye kipindi hicho alikuwa anatumiwa na chama hiki, dhana hii imebuniwa na kuwa propagated na chama kinachojiita kikuu cha uponzani Tanzania.

Mbinu yao ni ile ile, kutumia vijana ambao wengi wao wanajulikana walau kwa nick names kwa njia ya makala na meseji kwenye social media, JF ikiongoza.

Kwa sababu ni mabingwa wa kutumia mbinu chafu hasa wakishindwa kwa hoja, mnakumbuka story za kutunga za utekaji na mauaji! Hawaoni shida kutumia dhana ya ukabila.

Ndiyo maana sikushangaa sana kiongozi wao alivyotembelea Arusha hivi karibuni, aliwaita watu wa kabila lake mkoani hapa na kufanya nao mkutano wa siri. Imagine kiongozi wa kisiasa unaenda mkoa fulani alafu unaita watu wa kabila lako tu kisiri na kuendeleza ajenda za kisiasa, za kitaifa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…