Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 53,857
- 121,995
Wanabodi,
Wanabodi, Ijumaa ya leo nimepata fursa ya kuendelea na zile makala zangu za kwa Maslahi ya Taifa, leo nikiulizia kuhusu msimamo wa rais Magufuli kutosafiri nje hata kwa zile safari zenye maslahi makubwa kwa taifa, jee msimamo huo una Maslahi kwa Taifa?
Bandiko hili ni la swali moja kuu, kuwa Tanzania tumedhamiria kujenga Tanzania ya Viwanda, Jee tunaweza kuijenga hiyo Tanzania ya Viwanda bila kutegemea mitaji ya FDI kutoka nchi za nje zikiwemo nchi za Mabeberu?. Namna mzuri ya kuhamasisha FDI ni kupitia kwenye ziara za nje za rais, tuliona kwa JK, tukaona kwa Kagame na sasa tunaona kwa Uhuru, jee rais wetu Magufuli aendelee tuu kujifungia ndani tukitumai hizi FDI zitatufuata zenyewe?
Msimamo wa Rais wetu Dr. John Pombe Joseph Magufuli , JPM, wa kutosafiri nje una maslahi kwa taifa kwenye hili, hivyo kama tunategemea FDI kutoka nje, lazima rais Magufuli akubali kutoka awafuate ili kuvutia FDI zao au azidi kushikilia msimamo, tukomae nao, kwa hoja ya mgonjwa ndio hufuata mganga, kama wana shida waje?.
Kwa wavivu wa kusoma makitu marefu, tuishie hapa, wengine tuendeleeni.
Tena kwa sasa bara zima ka Africa tuko kwenye kukamilisha kusaini African Continental Free Trade Area (AfCFTA) Agreement, lakini sisikii Tanzania tunajipangaje. Hivyo Kenya akisaini FTA na Marekani, then njia ya bidhaa za Africa Mashariki kuingia Marekani ni kupitia Kenya.
Hitimisho, kwa vile nimesema mengi humu, naomba kumalizia na lile swali la msingi la hoja hii kwa Maslahi ya Taifa, kuhusu msimamo wa rais Magufuli kutosafiri nje hata kwa zile safari zenye maslahi makubwa kwa taifa, jee msimamo huo una Maslahi kwa Taifa?.
Kwa kuwa Tanzania tumedhamiria kujenga Tanzania ya Viwanda, Jee tunaweza kuijenga hiyo Tanzania ya Viwanda bila kutegemea mitaji ya FDI kutoka nchi za nje zikiwemo nchi za Mabeberu, kuna umuhimu kwa rais wetu kusafiri nchi katika ziara za kimkakati ili kuvutia FDI?.
Kwa wale wa swala, Ijumaa Kareem
Kwa sisi wengine, Furahi Dei Njema
Paskali
Wanabodi, Ijumaa ya leo nimepata fursa ya kuendelea na zile makala zangu za kwa Maslahi ya Taifa, leo nikiulizia kuhusu msimamo wa rais Magufuli kutosafiri nje hata kwa zile safari zenye maslahi makubwa kwa taifa, jee msimamo huo una Maslahi kwa Taifa?
Bandiko hili ni la swali moja kuu, kuwa Tanzania tumedhamiria kujenga Tanzania ya Viwanda, Jee tunaweza kuijenga hiyo Tanzania ya Viwanda bila kutegemea mitaji ya FDI kutoka nchi za nje zikiwemo nchi za Mabeberu?. Namna mzuri ya kuhamasisha FDI ni kupitia kwenye ziara za nje za rais, tuliona kwa JK, tukaona kwa Kagame na sasa tunaona kwa Uhuru, jee rais wetu Magufuli aendelee tuu kujifungia ndani tukitumai hizi FDI zitatufuata zenyewe?
Msimamo wa Rais wetu Dr. John Pombe Joseph Magufuli , JPM, wa kutosafiri nje una maslahi kwa taifa kwenye hili, hivyo kama tunategemea FDI kutoka nje, lazima rais Magufuli akubali kutoka awafuate ili kuvutia FDI zao au azidi kushikilia msimamo, tukomae nao, kwa hoja ya mgonjwa ndio hufuata mganga, kama wana shida waje?.
Kwa wavivu wa kusoma makitu marefu, tuishie hapa, wengine tuendeleeni.
Tena nashauri, baada ya Uchaguzi Mkuu ujao, yule kijana "pendwa" asipogombea ubunge popote, rais amteue tuu awe Mbunge wa kuteuliwa amfanye deputy wa MFA, na ataandamana nae UNGA, halafu tupimane ubavu na kubwa la mabeberu, nani zaidi kati ya Hapa Kazi akiongozana na Dogo Janja na Pempei na Kubwa Jinga!.Kwa miaka ya hivi karibuni nchi ya Marekani na vibaraka wake EU zimekuwa zikituchokoa sana kwenye mambo yutu ya ndani kutaka kutuingilia, wanatumia visingizio vya democracy, na human rights, kwa kutaka kulazimisha democratic modal yao ndio iwe imposed to all, na human rights records zao ndio ziwe standards to all, tumewagomea
Sisi tuna democracy modal yetu ambayo ni Tanzanian Democracy ambayo ni part of African Democracy, ambapo inaruhusu uchaguzi wa vyama vingi vingi kufanyika, halafu chama kimoja kikashinda kwa 99.9% na uchaguzi huo bado ukahesabika ni uchaguzi huru na wa haki kama ilivyokuwa kwa uchaguzi wa serikali za mitaa, ambapo CCM imeshinda kwa ushindi wa kishindo cha asilimia 99.9% na uchaguzi ulikuwa huru na wa haki kwa mujibu wa ile kanuni ya "the end justifies the means" ambapo modal hiyo pia ndio tutakayo itumia kwenye uchaguzi Mkuu ujao. Kwa mabeberu na vibaraka wao hawaamini na sasa kwenye Uchanguzi Mkuu wanataka kutuingilia. Wanaoamua ni wananchi, wanaopiga kura ni wananchi, kama wananchi wenyewe ndio ndio wameamua kwa hiyari yao wenyewe na uhuru bila shinikizo, wamekichagua chama kimoja kwa kukipa ushindi wa asilimia 99.9%, nani anaweza kuwabishia?. Kama kwa sheria yetu kukijitokeza mgombea mmoja tuu anatangazwa ni mshindi halali, kama wapinzani waliamua kutumia demokrasia yao ya kutoshiri, hiyo nayo ni demokrasia na ndio demokrasia yetu wasituingilie!.
Hata kwenye human rights records, pia tuna modals zetu, baadhi ya tabia za kizungu kwetu ni uchafu, hawawezi kutulazimisha, sasa wamefikia kumzuia mmoja wa viongozi wetu kuingia nchini kwao kwa kukataa uchafu wao, wakidhani wanatukomoa, tutawaonyesha!.
Hata suala la watu wanaopotea katika mazingira ya kutatanisha na ile miili iliyokuwa inaopolewa kwenye mito na fukwe, Jeshi letu safi la polisi lenye uwezo mkubwa, halina hata haja ya kubaini kwa kutumia DNA, limebaini ile ni miili ya wakimbizi wa kutoka nje ambao wamekufa kwa njaa na kukosa hewa ili wasibainike wanaamua kuwazika marehemu wao kwenye maji wasionekane.
Na tukio kama lile shambulio la mwanasiasa pale Dodoma, wale ni watu wasiojulikana na wako mahali kote duniani, tena Marekani ndio taifa linaloongoza kwa unsolved murder mysteries sasa wanashangaa ni kwa Tanzania?. Au kuzuia wazururaji kwa kisingizio cha kufanya maandanano, na kuzuia wapiga uvivu na wakaa bure kwa kusingizio cha kuhudhuria mikutano ya hadhara ya kisiasa?. Tanzania ya sasa ni Tanzania ya hapa kazi tuu, hii ndio Tanzania yetu, hii ndio demokrasia yetu na viwango hivyo vya human rights records ndio viwango vyetu wasituingilie.
Adhabu za Utotoni.
Nakumbuka tukiwa wadogo, mtoto akifanya kosa la kustahili adhabu mbadala, anaadhibiwa kupitia kwa mtoto mwingine ambaye ataletewa zawadi yeye atanyimwa. Huu ukaribu wa nchi beberu ya Marekani na our next door Kenya, unanitia mashaka!, sio kwamba mabeberu hawa baada ya kutushindwa kutuingilia sasa wanataka kutuzunguka na kutuchapa fimbo za kiuchumi na ki lbiashara kupitia kwa jirani yetu wa Kenya?.
Tangu kuingia madarakani kwa serikali ya awamu ya tano, rais Magufuli na serikali yake ya awamu ya tano, anafanya kazi nzuri kwa kubadili sheria za uwekezaji ili rasilimali zetu zitufaidie wenyewe na kuimarisha ukusanyaji mapato, kufufua uchumi kwa kununua ndege, kujenga miundombinu kama SGR na miradi ya kimkakati kama Stigler kwa fedha za ndani, hivyo sasa mabeberu wanatuonea wivu jinsi tunavyoendelea bila kuwategemea wao.
Kwa vile tumedhamiria kujenga Tanzania ya viwanda ili kuipeleka Tanzania kuwa nchi ya uchumi wa kati katika safari ya kuwa donor country kwa kutumia fedha zetu wenyewe za ndani na kujazilizia kwa mikopo, jee Tanzania tunaweza kujenga Tanzania ya Viwanda bila Kutegemea mitaji na fedha za FDI za kutoka kwa Mabeberu wakiongozwa na kubwa la mabeberu Marekani?.
Nilimuona rais jirani yetu, Uhuru Kenyatta akifanya ziara ya Marekani, na baada ya ziara ile, leo kuna kitu nimekisoma kuhusu matokeo ya ziara hiyo. Nimekisoma hapa
Corporate Council on Africa
www.corporatecouncilonafrica.com
Tusemezane ukweli jameni, haya makusanyo yetu ya ndani, kweli yanaweza kutosha kugharimia miradi yote mikubwa hii ya kimkakati, tukawalipa watu wetu nyongeza zao stahiki za mishara, na bado tukaservice deni la nje?. Mbona naona kama bado tunakopa?!.
Tukubali tukatae, japo naunga mkono msimamo wa rais Magufuli kutokusafiri nje kwa safari zisizo na manufaa, lakini sio kila safari ya ng'ambo ni kutalii!, safari nyingine ni safari za kimkakati, hivyo jee lazima tufike mahali Rais Magufuli alazimishwe kusafiri nje, safari za kimkakati?.
Kati ya nchi zote za Africa Mashariki, Tanzania ndio inayoongoza kwa fursa, the most advantageous kutawala uchumi wa Africa Mashariki kuanzia vivutio vya utalii, bandari, usafirishaji, madini, gesi, mafuta yako njiani, hivi hii Kenya inayokumbatiwa hivi na mabeberu, ina nini?!, kila uchao Kenya inastrugle kutupiga bao!. Shuhudieni jinsi rais Uhuru Kenyatta alivyotupiga bao kwa kulamba bingo ya kubwa la mabeberu, Marekani kwa kusaini FTA kati ya Kenya na Marekani.
Ili Tanzania ya viwanda ilete manufaa makubwa ni lazima viwanda hivyo vizalishe bidhaa for export markets ili vituingizie fedha za mabeberu ambayo ni dola ya Marekani, jee sisi Tanzania tuna juhudi zozote kukuza biashara ya nje?.
Wakati sisi tukihangaika kujenga viwanda, Uhuru Kenyatta yeye anahangaikia masoko ya kimataifa, sasa kwa vile tayari tunayo EAC Custom Union, na tuna soko la EAC, SADC na Comesa, hii FTA ya Kenya na Marekani itaifanya Kenya kuwa ndio hub ya international export trade kwa soko la Marekani ambalo ndilo soko kubwa kuliko masoko yote duniani.
Japo Tanzania tuko kwenye soko la AGOA, Tanzania hatujawahi ku utilize fursa za soko hili to the fullest compared to Kenya na Uganda, hivyo hii FTA ya Kenya na Marekani ndio itaifanya Kenya kuwa ndio soko kuu la bidhaa na mazao kutoka Tanzania, hata huku kuandimika kwa nyanya, wafanyabiashara wa Kenya, wananunua nyanya zote zikiwa shambani!, hivyo nyanya zimeadimika, hiyo FTA ikiwa kwenye full fledge Tanzania tutakuwa na hali gani?.
Kwa nini Tanzania tupigwe bao kama hili la kisigino, wakati all it takes ni kwa rais wetu kuacha kujifungia ndani, atoke tuu kidogo hapo nje avuke bahari na kujichanganya na marais wenzake wa Africa na duniani akiwemo rais kubwa la mabeberu, zaidi ya faida za kiuchumi za ziara za kimkakati, safari za nje zina faida ya ziada ya exposure hivyo inapunguza...
Tena kwa sasa bara zima ka Africa tuko kwenye kukamilisha kusaini African Continental Free Trade Area (AfCFTA) Agreement, lakini sisikii Tanzania tunajipangaje. Hivyo Kenya akisaini FTA na Marekani, then njia ya bidhaa za Africa Mashariki kuingia Marekani ni kupitia Kenya.
Hitimisho, kwa vile nimesema mengi humu, naomba kumalizia na lile swali la msingi la hoja hii kwa Maslahi ya Taifa, kuhusu msimamo wa rais Magufuli kutosafiri nje hata kwa zile safari zenye maslahi makubwa kwa taifa, jee msimamo huo una Maslahi kwa Taifa?.
Kwa kuwa Tanzania tumedhamiria kujenga Tanzania ya Viwanda, Jee tunaweza kuijenga hiyo Tanzania ya Viwanda bila kutegemea mitaji ya FDI kutoka nchi za nje zikiwemo nchi za Mabeberu, kuna umuhimu kwa rais wetu kusafiri nchi katika ziara za kimkakati ili kuvutia FDI?.
Kwa wale wa swala, Ijumaa Kareem
Kwa sisi wengine, Furahi Dei Njema
Paskali