Cute Wife
JF-Expert Member
- Nov 17, 2023
- 1,906
- 5,000
We umewahi kuongea ukweli bana chawa ndugu yake kunguni?🌚🌚Tatizo lenu mtu akiongea ukweli mnasema ni chawa.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
We umewahi kuongea ukweli bana chawa ndugu yake kunguni?🌚🌚Tatizo lenu mtu akiongea ukweli mnasema ni chawa.
hahaha kwamba hawa wa sasa ni special case?Zamani waliwaita wapambe, leo ni machawa...they've been there miaka yote, ila wa sasa wamechangamka sana.
Kawaida unaona ni panic!Ona ulivyopanic sasa Mkuu... asante kwa kunijuza zaidi kuhusu wewe
Uchawa ndio Tunu ya Taifa kwa Sasa. Next Month nitaanza kujiunga Uchawa full combatUsikose kujiunga nasi katika Mjadala wa "Je, 'Uchawa' unakwamisha Uwajibikaji?" Alhamisi hii ya Februari 27, 2025, kuanzia Saa 12 jioni hadi 2 usiku, kupitia Xspaces ya JamiiForums
'Washtue' ndugu, jamaa au marafiki ili wawe sehemu ya Mjadala huu muhimu kwa 'kesho' ya Nchi yetu.
Washiriki watapata fursa ya kutoa maoni au mapendekezo na kuuliza maswali Wazungumzaji wetu
Kushiriki bofya https://jamii.app/KujipendekezaSpace
Khalifa Said
"Uchawa sidhani kama unazorotesha uwajibikaji, ninavyodhani mimi kitu kikubwa kinachodhorotesha uwajibikaji ni uimla, ukatili wa kidola, matumizi ya nguvu kwa polisi na mbinu nyingine za kihuni na za kishenzi zinazotumiwa na waliopa madarakani kuwanyamazisha watu ikiwemo kuwateka"
"Vijana wengi wanajikaribisha kwenye nafasi za Viongozi kwa kuwa wanaona hiyo ndio njia salama ya wao kufanikisha mambo yao mbalimbaliKama tunataka kuondoa hali hiyo tunatakiwa kuweka msingi ambao kila mchango wa Mtu unaweza kuheshimiwa tofauti na ilivyo sasa, mfano Msanii ukiimba nyimbo tofauti na wale waliopo Madarakani inakuwa ngumu kufanikiwa"
Carlos Buto
Carlos amezungumzia kuhusu historia ya Uchawa, ameeleza uchawa haujanza leo katika nchi yetu, uchawa umekuwepo kuanzia kipidni cha mfumo wa chama kimoja lakini kwa hivi sasa unaonekana sana kutokana na uwepo wa mitandao ya kijamii. Ameeleza kuwa mifumo bora ya uchaguzi ndiyo inayoweza kuondoa kadhia hii ya uchawa.
Annastazia Rugambwa
Annastazia ameeleza na kukubali kuwa uchawa ni tatizo kubwa sana na ili kuweza kutatua uongozi wa kiimla inabidi uchawa ukomeshwe. Ameleza pia kutokana na utafiti walioufanya watanzania zaidi ya 53% wanazungumzia kuhusu hali ngumu ya maisha, wengine wameelezea kuhusu ukosefu wa ajira. Ameeleza kuwa Chanzo cha uchawa ni hali ngumu ya maisha, kama wangekuwa na hali nzuri za maisha isingekuwa rahisi kwa wao kufanya uchawa kwani uchawa ni aibu.
Uchawa unawalemaza viongozi, wanaweza wakawa na nia ya kuwasaidia wananchi lakini wanapokutana na uchawa wanasifiwa hivyo kupelekea siku wakihojiwa kuhusu uwajibikaji wao wanakuwa wakali. Amesisitiza kuwa kuna uhusiano mkubwa kati ya uchawa na umasikini.
Ameeleza pia kuwa umasikini ndiyo mtaji wa viongozi na hiyo ndiyo sababu ya wao kutokupambana na umasikini kwa sababu ndiyo mtaji wao. Ameuliza kama umasikini ukiondoka machawa watatoka wapi?
What do you mean by this wordsIt goes without saying….
Asante tena kwa kuendelea kunijuza kuhusu wewe MkuuKawaida unaona ni panic!
Hatuko katika wavelengths zilizo sawa ndo maana [1] umeshangaa jambo ambalo ni dhahiri kabisa na [2] wala sijakujuza chochote kuhusu mimi.
Una tatizo la kusoma na kuelewa. Sijakujuza chochote halafu unatoa shukrani!
Shuleni ulikuwa unapata alama gani wewe? 🤣

yaani unafunguka tuuUnajua principal ya divide and rule?kwa wananchi kuungana pamoja na kuukataa uchawa
my lady,Hadi wewe umekubali, kweli uchawa unawakwaza wengi isipokuwa akina Tlaatlaah, Lucas Mwashambwa, FaizaFoxy Gerson Msigwa Dr. Mwigulu Nchemba, ChoiceVariable na genge lao