Je, Uchawi una mchango wowote katika kukuza Biashara?

Je, Uchawi una mchango wowote katika kukuza Biashara?

Jumong S

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2013
Posts
7,385
Reaction score
10,659
Wiki iliyopita nilitoka Moshi nikaenda kumtembelea classmate wangu pale Arusha. Jamaa ni engineer wa computer. Jumapili baada ya kula Ibada Safi na kwaya kali pale St. Theresa tuli-mount XR 250 na tukaenda kufunga Camera za usalama kwa nyumba mpya ya Tajiri mmoja wa Kanda ya Ziwa. Huyu mjuba kajenga mjumba wa kuishi wa ghorofa mbili. Pale kwake pazuri asee, kama Ikulu ati.

Basi tukiwa tunakomaa na kazi (mie sio mtaalam but nilikua Nampa kampani msela) jamaa alikuja na Range lake kutuletea Vifaa kadhaa. Baada ya kukabidhi alisepa. Basi jamaa yangu akawa ananiongelesha kwa kispanish chetu cha kuunga unga na solotepu. Akanambia huyu mjuba ni mchawi balaa. Pale kwake tulikuta watoto wawili wa kiume mandondocha wanatematema udenda tu.

Jamaa akanambia ni watoto wake wa kuzaa kabisa na ndo wanalinda business zake. Yes, jamaa Ana biashara kubwa ya Hardware na electronics. Nasikia pia Ana Real estate bila kuhesabu biashara nyingine huko kwao! Pale tu nilihesabu magari 4 makali bila kuhesabu maroli ya biashara. Alikua na chale Kadhaa usoni na mikononi. Inasemekana biashara zake kazizindika kwa makafara balaa!

Sasa tujiulize, je, Uchawi una nafasi gani katika kukuza Biashara? Kuna ukweli wowote katika kuinua biashara?

Je, kwa nini tusiusome ktk masomo ya vyuoni kwa maendeleo ya umma?
 
Ngoja nikupe elimu kidogo kuhusu utajiri

Kwanza kuanzia Leo utambue hili, Mungu alipomuumba Adam na Eva aliwapa utajiri wote wa duniani na fahari zake wazimiliki, lakini walipohasi kwa Mungu kwa kumsikiliza shetani, utajiri wote wa duniani ukawa ni Mali ya shetani, wanadamu hatumiliki tena utajiri wa hapa duniani.

Sasa ili kuwa tajiri una options mbili tu
(1) umuombe shetani akupe sehemu ya utajiri anaomiliki, hii inawezekana kama ukikubaliana na masharti yake, na siku ukienda kinyume anakunyang'anya.
(2) umuombe Mungu akupe sehemu ya utajiri alioushikilia Shetani, na hii inawezekana kama utakuwa muombaji sana na mtakatifu haswa, kumyang'anya shetani sehemu ya utajiri wake si rahisi kihivyo.

Usijidanganye kama unaweza kuwa tajiri kwa kufuata seminar za motivation speaker peke yake, utajiri wote anao shetani, ni either uungane naye au upambane kumyang'anya.
 
Ngoja nikupe elimu kidogo kuhusu utajiri
Kwanza kuanzia Leo utambue hili, Mungu alipomuumba Adam na Eva aliwapa utajiri wote wa duniani na fahari zake wazimiliki, lakini walipohasi kwa Mungu kwa kumsikiliza shetani, utajiri wote wa duniani ukawa ni Mali ya shetani, wanadamu hatumiliki tena utajiri wa hapa duniani.
Sasa ili kuwa tajiri una options mbili tu
(1) umuombe shetani akupe sehemu ya utajiri anaomiliki, hii inawezekana kama ukikubaliana na masharti yake, na siku ukienda kinyume anakunyang'anya.
(2) umuombe Mungu akupe sehemu ya utajiri alioushikilia Shetani, na hii inawezekana kama utakuwa muombaji sana na mtakatifu haswa, kumyang'anya shetani sehemu ya utajiri wake si rahisi kihivyo.

Usijidanganye kama unaweza kuwa tajiri kwa kufuata seminar za motivation speaker peke yake, utajiri wote anao shetani, ni either uungane naye au upambane kumyang'anya.
Duh!
 
Mkuu biashara nyingi zimezindikwa na zimepigwa kalilio la kivutia wateja, hakuna biashara mjini zinaenda kwa uzoefu . Mjini kuzito sana , last weekend nilitembelea night club flan hivi chugga nilishangaa nilipoingia mwili ulisisimka sana hata watu niliowakuta hawakuwa wakawaida na cha kushangaza club nzima nilikutana na sura ngeni halafu zinafanana we acha tu.

Kipindi nipo mwanza niliwahi kuwa na mwenyeji alinisimulia mambo mengi kuhusu biashara na nguvu za Giza zinavyotumika . Duniani ni mapito tu kila mtu ashinde mechi zake kwa juhudi au kubebwa.Mjini kuzito sana , nenda kwa mfano hapa Arusha , soko kuu, Kilombero au maduka ya stendi ndogo Kama uko vizuri na Kinga za jadi utaona mengi . Wamama wa Kilombero ni nomana hata wale wauza matunda Kilombero .
 
Wiki iliyopita nilitoka Moshi nikaenda kumtembelea classmate wangu pale Arusha. Jamaa ni engineer wa computer. Jpili baada ya kula Ibada Safi na kwaya kali pale St. Theresa tuli-mount XR 250 na tukaenda kufunga Camera za usalama kwa nyumba mpya ya Tajiri mmoja wa Kanda ya Ziwa. Huyu mjuba kajenga mjumba wa kuishi wa ghorofa mbili. Pale kwake pazuri asee, kama Ikulu ati.
Je, kwa nini tusiusome ktk masomo ya vyuoni kwa maendeleo ya umma?

Kuna elimu zimefichwa haiwezekani kuziweka katika masomo ya vyuoni

Lakini elimu hizo ukizitaka utazipata Kwa manufaa yako maana wengine wanaweza wasizihitaji
 
Ngoja nikupe elimu kidogo kuhusu utajiri
Kwanza kuanzia Leo utambue hili, Mungu alipomuumba Adam na Eva aliwapa utajiri wote wa duniani na fahari zake wazimiliki, lakini walipohasi kwa Mungu kwa kumsikiliza shetani, utajiri wote wa duniani ukawa ni Mali ya shetani, wanadamu hatumiliki tena utajiri wa hapa duniani.
Sasa ili kuwa tajiri una options mbili tu
(1) umuombe shetani akupe sehemu ya utajiri anaomiliki, hii inawezekana kama ukikubaliana na masharti yake, na siku ukienda kinyume anakunyang'anya.
(2) umuombe Mungu akupe sehemu ya utajiri alioushikilia Shetani, na hii inawezekana kama utakuwa muombaji sana na mtakatifu haswa, kumyang'anya shetani sehemu ya utajiri wake si rahisi kihivyo.

Usijidanganye kama unaweza kuwa tajiri kwa kufuata seminar za motivation speaker peke yake, utajiri wote anao shetani, ni either uungane naye au upambane kumyang'anya.
Tatizo connection Ni ngum kupata walio wengi wangekua kwa Lucifer
 
Siamini hivyo vitu, mganga sasa nyumba ya nyasi na watoto viriba tumbo huku wake zake wanne wakiwa hawana nuru kabisa.
Hakuna kitu unachomiliki katika hii dunia, wewe ni mpitaji tu, unaakodisha Mali za shetani ukifa unamuachia au umnyang' anye kwa msaada wa Mungu ila ukifa unamuachia Mungu vitu vyake.
Hapa duniani unakuja mtupu unaondoka mtupu.
Hivi unajua hata huu mwili tunaazima tu, ila tukifa tunauacha hapa duniani.
 
Hakuna kitu unachomiliki katika hii dunia, wewe ni mpitaji tu, unaakodisha Mali za shetani ukifa unamuachia au umnyang' anye kwa msaada wa Mungu ila ukifa unamuachia Mungu vitu vyake.
Hapa duniani unakuja mtupu unaondoka mtupu.
Hivi unajua hata huu mwili tunaazima tu, ila tukifa tunauacha hapa duniani.
Hili ni suala la Imani na kama imekuingia basi hakuna shida mm nipo poa kabisa wala sina shida. Mm naishi kwa Imani ya mtaji wa masikini ni nguvu zake mwenyewe ila siyo za giza
 
Ujatembea ukaona dunia ilivyo umezoea kuona dunia kwa sura ya nje tu
Nimeishi kigoma, pangani, tanga mjini, sumbawanga, namanyere, lyambamfipa, shinyanga, bariadi huko wanasema kuna mlango wa kuzimu, pemba na mafia kote huko nk nk lakini sijawahi kukwamishwa jambo langu kwa namna yoyote ile ya kichawi labdq figisu tu za kuchongeana kwenye majukumu. Mm siamini katika utajiri ni nguvu za shetani bali naamini utajiri ni katika juhudi na mawazo yetu katika kufanya kazi.
 
Hakuna uchawi, juhudi binafsi katika utafutaji ndio daraja litaloweza kukufikisha kwenye point ya utajiri

Africa tuko kwenye rank za juu kabisa katika mabara yenye imani za kishirikina, lakini hatujaweza kutoa hata mchawi mmoja kwenye top 10 ya mabilionea

Swali la kizushi kwa wewe unayeamini uchawi

Utachukua reaction ganu siku ambayo umemuajiri mtu akuuzie duka lako halafu baada ya siku kadhaa akaja kukuambia ule mtaji wote umesombwa na wachawi kupitia chuma ulete??
 
Hakuna uchawi, juhudi binafsi katika utafutaji ndio daraja litaloweza kukufikisha kwenye point ya utajiri

Africa tuko kwenye rank za juu kabisa katika mabara yenye imani za kishirikina, lakini hatujaweza kutoa hata mchawi mmoja kwenye top 10 ya mabilionea

Swali la kizushi kwa wewe unayeamini uchawi

Utachukua reaction ganu siku ambayo umemuajiri mtu akuuzie duka lako halafu baada ya siku kadhaa akaja kukuambia ule mtaji wote umesombwa na wachawi kupitia chuma ulete??
sahihi kabisa mkuu, wengi wetu hasa sisi wakuona giza lishatanda na hakuna namna tunaweza ishi maisha yale ya ndoto zetu hujifariji kwa imani hizi za kishirikina.
 
Sizungumzii kwa wengine, ila kwangu binafsi.

Nafanya biashara ya kifedha (za mtandao na benki). Mwaka 2018 nilipigwa tukio na wakulungwa wakaondoka na 28+ Million cash, simu na mashine za benki.

Nilimpigia simu mama yangu kumueleze maswaibu yaliyonipata. Alishangaa sana nimesurvive vipi zaidi ya miaka 5 bila kuzindika eneo langu la biashara.

Akanitaka niende nyumbani kwa mwitikio wa haraka. Baada ya kuandika maelezo polisi, jioni nikazama nyumbani.

Akanipeleka kwa mzee mmoja. Wala siyo mchawi, ila ni mtaalamu wa kuzindika.

Kuzindika siyo uchawi. Nikampeleka mjini. Akafanya yake akarudi.

Nimeshakosa majaribio matatu ya kuvamiwa.

Na ripoti zote nazipata kutoka polisi. Wakivamia na kukamatwa, wakihojiwa wanasema walipanga kuja kuniibia. Ila mikakati yao inafeli.

Zindiko ni muhimu sana.
 
Sizungumzii kwa wengine, ila kwangu binafsi.

Nafanya biashara ya kifedha (za mtandao na benki). Mwaka 2018 nilipigwa tukio na wakulungwa wakaondoka na 28+ Million cash, simu na mashine za benki.

Nilimpigia simu mama yangu kumueleze maswaibu yaliyonipata. Alishangaa sana nimesurvive vipi zaidi ya miaka 5 bila kuzindika eneo langu la biashara.

Akanitaka niende nyumbani kwa mwitikio wa haraka. Baada ya kuandika maelezo polisi, jioni nikazama nyumbani.

Akanipeleka kwa mzee mmoja. Wala siyo mchawi, ila ni mtaalamu wa kuzindika.

Kuzindika siyo uchawi. Nikampeleka mjini. Akafanya yake akarudi.

Nimeshakosa majaribio matatu ya kuvamiwa.

Na ripoti zote nazipata kutoka polisi. Wakivamia na kukamatwa, wakihojiwa wanasema walipanga kuja kuniibia. Ila mikakati yao inafeli.

Zindiko ni muhimu sana.
Huu ushahidi bado haujitoshelezi mkuu, mm nilifikiri baada ya ripoti kufika kwa mtaalamu pesa zikarudi katika mazingira ambayo na wewe ya kuliacha katika wakati mgumu bila kuelewa nini kilitokea.
 
Ngoja nikupe elimu kidogo kuhusu utajiri
Kwanza kuanzia Leo utambue hili, Mungu alipomuumba Adam na Eva aliwapa utajiri wote wa duniani na fahari zake wazimiliki, lakini walipohasi kwa Mungu kwa kumsikiliza shetani, utajiri wote wa duniani ukawa ni Mali ya shetani, wanadamu hatumiliki tena utajiri wa hapa duniani.
Sasa ili kuwa tajiri una options mbili tu
(1) umuombe shetani akupe sehemu ya utajiri anaomiliki, hii inawezekana kama ukikubaliana na masharti yake, na siku ukienda kinyume anakunyang'anya.
(2) umuombe Mungu akupe sehemu ya utajiri alioushikilia Shetani, na hii inawezekana kama utakuwa muombaji sana na mtakatifu haswa, kumyang'anya shetani sehemu ya utajiri wake si rahisi kihivyo.

Usijidanganye kama unaweza kuwa tajiri kwa kufuata seminar za motivation speaker peke yake, utajiri wote anao shetani, ni either uungane naye au upambane kumyang'anya.
Waliotoboa bila kuamini number moja na mbili ni viumbe vya ajabu?
 
Back
Top Bottom