Je, Ukubwa wa Nchi yetu Tanzania ni kikwazo katika kuwafikia na kuwahudumia wananchi?

Sahihi
 
Kikwazo ni chadema na vibaraka.
Mkuu kivipi? To be fair fafanua vizuri! Uliowataja hapo juu hawakusanyi kodi, hawaandai bajeti ya serikali na hawapo Bungeni kwa sasa. Ni miaka 60 sasa hawajawahi kushika dola wala serikali, wanakuwaje kikwazo?
 
Kumanage population kubwa hili ichochee maendeleo ni kazi kubwa inayoitaji miaka mingi sana .
Kwa akili ya haraka haraka unaweza ukasema population kubwa ndio yenye kuchangia Kodi nyingi hivo maendeleo yatachochewa haraka sana .
Lakini kwa jinsi nionavyo population kubwa ndiyo yenye kutumia Kodi nyingi na kuchochea umaskini wa haraka sana, nawasikia wakubwa wangu wanasema enzi za Nyerere Kuna favour nyingi walikuwa wakizipata Sasa awazipati, kwenye elimu uko, mahospitalini uko Sasa akuna Nini tafsiri yake kipindi kile ilikuwa ni raisi kufanya yote hayo kulingana na hile population.
Saizi ni kazi kubwa sana mfano hii population ya zaidi ya mil 61 tafuta takwimu ujue ni wangapi kweli wanalipa Kodi kwa ajili ya maendeleo ya nchi Yao utachoka na hapo ndo utajua panya wengi awachimbi mshimo na hii population kubwa ni mzingo inanyonya watu wachache na hivyo tutachelewa kufika malengo .
Nb; Ni mtizamo wangu
 

Mkuu nakuunga mkono! πŸ‘πŸ‘
 
Tatizo sio ukubwa, tatizo ni viongozi kuwa wabinafsi na wabadhilifu wa mali za umma.
Kila Mwaka CAG anatoa taarifa yake huku akifichua ubadhirifu mkubwa sana wa fedha za umma, fedha ambazo kama zisingefanyiwa ufisadi zilinufaisha taifa kwa namna nzuri na kupunguza au kuondoa kabisa kero mbalimbali ndani ya taifa hili
 
Somehow but with brain,Nchi hii ni ndogo sana
 
Tatizo si ukubwa wa nchi, wala idadi ya watu...hivi vimekuwa visingizio vya wachache wenye uvivu wa kufikiri. Tatizo letu ni kurundika kila kitu, kila jambo, kila makusanyo, nk. kwa serikali kuu(mfuko mkuu/hazina). Na hiki ndiyo kinatoa mwanya kwa wapigaji. Kwanza nchi ingegawanywa katika kanda za kiuchumi (Economic Zone); na siyo hizi za kisiasa. Kwa rasilimali zilizopo hapa nchini, kila kanda (angalau ziwe 5) inazo raslimali za kutosha kuendeleza maeneo hayo, kuanzia kilimo, mifugo, uvuvi, madini, utalii, nk. Mapato yote yakusanywe katika kanda na kuhudumia maendeleo ya kanda husika. Asilimia kidogo sana ya makusanyo ipelekwe hazina kuu kwa shughuli za utawala..hapo tutapunguza upigaji. Na huku kwenye kanda viongozi wote wachaguliwe na wananchi na kudhibitiwa na wananchi wenyewe. HEBU TUJARIBU MUUNDO HUU TOFAUTI, TUONE KAMA KUNA SHULE ITAKOSA MADAWATI AU MATUNDU YA VYOO!
 
Tuangazie katika ngazi ya familia!!

Ikiwa kuzaa sana Kwa maskini, ni sababu kuu ya Umaskini wa Watanzania wengi wa KIPATO Cha chini, sasa kwanini matajiri pia hawana watoto wengi pamoja na kumiliki ukwasi wa kutosha kuwahudumia?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…