Je, ulishawahi kukutana na kitu cha kutisha usiku? Pita hapa tupeane uzoefu

sista angu alichelewa kurudi na mme wake..nyumba wakaniachia mimi niiangalie....basi bwana nkawa najikaza nsilale...nkikaza hadi saa sita usiku.wananiambia tu kwa simu tupo njiiani tunarudi
kutoka nje niingize baadhi ya vitu nakutana na paka mweusi tiii sijawahi ona...halafu macho yake makali yanawaka..
nkiangalia nyumba nyingine majirani wote wamelala..nkajipa ujasiri nimfukuze atakuwa paka wa kawaida tu..nkirusha kistu wapii.pakaa ndo kwanza hatikisiki ananikazia macho.....nkirusha jiwe na mikwara shhh...paka kaganda
badala ya paka kukimbia nkajikuta mi ndo natimua mbiokrud ndani..mlango nkaubana na funguo kabisa..taa nkazima..maana nlihisi ka kuna mtu ananichungulia dirishani.
 
Mwaka 1998 nilikuwa Mpanda mjini maeneo ya City nasubiri barmed afunge nitoke nae, makazi Kawajense,baada ya kusubiri kwa muda majira ya 5 demu akaniambia nisubiri kidogo.
Ili kupata uhakika nikamwambia anipe kitu chake nikaenacho, akanipa jacket lake.
Nikakaa mpaka saa 6 nasubiri kwa nje, nilipoingia ndani nikamuulizia nikaambiwa ametoka kama dk20 hivi nikazunguka kila kona sikukuona.

Nikaona hii noma nikaondoka zangu na jacket lake,kufika maeneo ya soko kuu nikaona polisi kwa mbali,nikaona hapa nimeisha nikala kona kumbe walikuwa wameniona.

Wakaanza kunifuata nikapiga kona za kutosha nikajikuta niko maeneo ya tajiri mmoja alikuwa anaitwa Tarimo, nikakutana na kundi la mbwa ikawa nafukuzwa na mbwa napolisi kwa pamoja, polisi walivyoona mbwa wakarudi nikapita barabara inayoelekea hosptali ya wilaya.
Nilichoka kupita maelezo, nafika shule ya Msakila nakutana na watu wako doria wakaniambia nisimame nikaona sasa hapa kama kufa nife siyo kwenda polisi nikaanza mbio tena,nilipofika nyumbani nilivyoingia ndani sikuamini,nikakoma kutembea usiku.
Na sintasahau kabisa ile siku, kwanza barmed alivyo niachia jacket lake na nilivyokoswa koswa kunyea debe kwa ajili yake.
.
 
Ha ha ha haaaaaaaah!
 
Duh..[emoji23] [emoji23]
Mbona hujamalizia kisa chako!
 
hahah mkuu inaonekana uyo mtoto kuna mdau alimbeba kwa dau la juu zaid yako,,ila ulijitahdi kuzitimua mbio asee,,polisi,mbwa na sungusungu wote umekalisha [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
mkuu huyo ndama wa mguu m1 hakuwaungia kweli?? najarib kufikiria mngekutana na mama ake angekuaje
 
Muzee ww ni shida! kumbe ww nawe ni muzee wa dawa za kisunni kama Mzizimkavu!
 
babu we ni suka au
 
Kubwa lao ni rafiki yangu moja alivyonielezea kisa cha yeye kuacha udaktar.

Huyu rafikia yangu akiwa doctor ktk nchi moja ya ng'ambo,siku moja akiwa ktk zamu ya kikazi, wakaletwa majeruhi wengi kutoka ktk ajali ya treni ya umeme, sasa,yeye na wasidizi wake wakaanza kuwapitia wale majeruhi walioumia sana. Akiwa ktk pilikapilka zake pale amewahudumia mpk akachoka na kusikitikia wale majeruhi akaamua kwenda kupumzika kidogo ktk chumba chake akiwa pale,mara ghafla mlango ukafunguliwa hamad tena ghafla anaona MAJERUHI KAINGIA NA KIWILIWILI CHA KICHWA CHAKE KASHIKILIA MKONONI,KILE KIWILIWILI CHA KICHWA AKISEMA "DOCTOR PLEASE NIUMGIE KICHWA CHANGU KWANI NATAKA NIWAHI KWANI KESHO NI SIKU HARUSI YANGU NA MCHUMBA WANGU YEYE AKUUMIA ILA KANIAGIZA NISIPOENDA KUFUNGA NAE NDOA KESHO,NDO MWISHO WA MAHUSIANO YANGU NAE.

LAAAA!!! Yule rafiki yangu dokta alipopata nafasi ya kupenya pale mlango alitimua mbio na kelele za kutosha,yule majeruhi nae mbio nyuma ya doctor.

Laaaa unajua kilichofuata?????...?
Kesho nitamalizia kisa hiki cha kutisha kwani naona4 wino wa kalamu yangu umekwisha na ni usiku sana.
 
Mie bhana nliendaga kwa ndugu zangu uko kijijini sasa tulikua ndugu wengi kidogo, hapakua na option zaidi ya wao ndugu zangu kunipa chumba cha ajabu kidogo, yaan nje ya nyumba yao kulikua na chumba ambacho kilikua hakitumiwi na watu, kilijengwaga kwa ajili ya wafanyakazi wa ng'ombe nk. Sasa hao wafanyakazi walikua ni wakabila flani iv tata kidogo kwa maswala ya ushirikina, walivyoondoka na kurudi kwao watu wakawa wanalalamika kila wakilala icho chumba, sasa mie sikuwai kujua habari hizi na kwa siku ile hapakua na option yoyote zaidi ya mie kupewa icho chumba, sasa sijui ndugu zangu waliniona mie kijana wa mjini mauza uza yatakwama au vp, ila ni vile ndugu wengine walikua watu wazima.

Kimbembe kikaanza usiku wa siku hio, sasa nimelala nahisi mmmmhh humu mbona kama kuna watu wengine tena waziada,basi napuuza mawazo haya tu ila sense zinaniambia kabisa we are more than 3 humu, aargggh nkafungulia RFA sikujali, sasa kimbembe kikaja usiku sanaa nikaanza kuskia watu wanatembea humo ndani, wengine wanapanda hdi juu ya kitanda nlicholala yaan nimelala naskia kabisa kuna mtu imesimama hapa kitandani, asee nliatuka vibaya sanaa, moyo unadunda, presha juu najiuliza naota au live, kumbe live, mara nikaskia mtu anavuta shuka, asee nliongea kwa nguvu "k**mamaaaaaeeeee" nani uyo, nkaskia sauti ya kicheko, nkajiuliza ndan au nje, asee nlisali sala zote, hali ikatulia kidogo, nikalala ila usingizi hauji, yaani nimetetemeka mpaka nimechoka, nimesali sanaa, sasa ukaja kama usingizi iv nikaanza kuota mambo ya ajabu et mule kuna watu watatu wananihoji wew umetoka wap, mbona mkorofi? Nani kakutuma uje chumbani kwetu khaaa nkastuka sasa nimestuka ila ile ndoto naiona kabisa inaendelea nikiwa macho, asee usiku ule ulikua vita vikali sanaa, nikawa macho tu nimefungulia radio kwa saut kubwa tu ila natetemeka haswa,,, kilichofuata kesho yake nikawaeleza ndugu zangu yote ndo wakanipa huu mkanda wa icho chumba na wengine hawakuamin kwamba nimewezaje kulala humo? Nikawamind kimoyo moyo wale ndugu kesho yake mchana tena uyoo nkarudi kwetu mjini,na nikasema niko radhi niue mchawi ila sio mwizi.
 

Jacket lake ulilifanyaje sasa
 
Serikali ingeingia mkataba iwafungie wanafunzi tekinolojia hii ingesaidia sana
 
Reactions: SDG
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…