Je, ulishawahi kukutana na kitu cha kutisha usiku? Pita hapa tupeane uzoefu

Huyo ndama wa mguu mmoja alikuwa amesimamaje!?

Sent from my HTC Desire 816 dual sim using JamiiForums mobile app
 
Hahaha...basi poa mkuu!
 
Ha ha ha kwa tusi ulilotoa lazma waseme we mkorofi
 
Usiombe kukutana na kibwengo ni msumbufu
 
Nakumbuka ilikuwa amri kila jpili nyumba nzima hasa watoto kwenda kanisani hasa ya kwanza. Siku hyo Mimi na wadogo zangu tulidamka saa10 pasipo kujua na kuanza kujiandaa kama dk20 tukawa tayari tunajiandaa kuondoka, pembeni ya nyumba yetu alikuwepo mama muuza samaki alisemekana anatumia nguvu za Giza( mchawi) ile tunapita kwenye kona inayotenganisha kwake na kwetu mara paap!! Nikamuona kazungukwa na moto mkubwa sana na yupo uchi kama anaoga. Nilimkazia macho sana akapayuka piteni haraka.. Sijui kama wadogo zangu waliliona hilo, Sikuuliza Kitu wala kusema mpaka nilipokuja kusema badae sana
 
Ilikuwa Ifakara, maeneo ya Viwanja 60, nikiwa Form 2, siku 1 nikawa nasafiri kwenda DSM. Ili kupanda treni TAZARA, ilikuwa kuna basi tunapanda (mf wa daladala) kutoka Viwanja 60 mpk Kibaoni ilipo station ya TAZARA.

ili kubana matumizi kwa akili za kitoto, classmate wangu akanambia atanfata home kwa baiskeli yake na kunipeleka station.

Treni ilikuwa inapita alfajir kutokea Mbeya, so ili kuiwahi mshkaji alikuja home kama Saa 7 (enzi hizo IFAKARA ni kijiji) na kwa wastani baiskeli ingetuchukua masaa 2-3!

Safari ilianza powa. Humo njiani vijiji VYOTE kimyaaaaa, miti, misitu na mashamba ya mpunga!

Tulikuwa tunapokezana kuendesha kila Mmoja anapochoka! Ikafika zamu yangu kuendesha! Nikaendesha kama dk 20 hv - kukawa na observation flani tunaziona!

1. Mimi nikawa nafeel Kitu flani mf wa vile mtu analiskia tumbo wkt ndege inashuka ama kupaa!

2. Mshkaji akanambia anahisi kama vile tunaendesha baiskeli ktk barabara ya lami, alikuwa haisi kami yale makorongo ya mashimo (IFAKARA lami bado)

3. Ajabu ya Mungu, kila mtu alipatwa na woga lakini hakuna aliemuambia mwenzake! Binafsi nikaanza kuona MWENDOKASI wa baiskeli umekuwa juu sana, zaidi ya Mara 3 ya mwendo wa kawaida!

4. Mshkaji ghafla akanambia anahisi tairi za baiskeli hazigusi ardhi! Kweli kuangalia chini.... Tukaona Kitu mf wa pumba za mpunga!

5. Kilichofuata, ile baiskeli ilikuwa inafanya kama vampire! Ni sawa niseme ikiruka Morocco inatua Victoria! Ikiruka tena inatua Science! Ikiruka science inatua Makongo! Ikiruka Makongo inatua GOIG! Ikiruka GOIG inatua Mbuyuni! Cha kushangaza ile baiskeli ilikuwa ikitua haitoi wala hatuhisi kishindo km vile ikianguka Nazi ama embe!

6. Tulipiga kimya. Nikaacha kunyonga pedal na mshkaji nae akawa kimyaaaa! Nikahisi amelala lkn nikawa naogopa kumuita!

Tulifika station ndani ya kama dk 45 tu! Tulifika pasi na uchovu! Baiskeli ilikuwa Ok tu! Mshkaji nlikaa nae station mpk treni ilipokuja! Alirudi town baada ya jua kuchomoza!

Tangu Hapo tuliacha rasmi kuendesha baiskeli usiku!
 
Bibi yako alikurahisishia safari uwahi kufika..
 
Nakumbukaga wale walikua wanaitwa vigozo walikua wanatabia ya kupoteza watu walikua wanaishi milimani sasa utakuta kuna ukungu mwingi mliman harafu ukiwa unatembea unamona MTU mbele yako kisha unatembea haraka haraka ili safar yenu iwe moja babu unaenda kunyofolewa macho
 
Naskia umemnunulia diamond kikuku cha kuvaa mguuni
 
Sijawahi kutana na mizoga ya aina hiyo maishani mwangu japo kuna wakati fulani tukiwa vijana tulikuwa tukiamka usiku na kwenda maporini kusaka wachawi na mara zote hizo sikufanikiwa kuwapata.
 
Nilisha wai kukutana na mzuka weeee sitak hata kukumbuka
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…