Je, umeshawahi kufuta namba ya mtu kwenye simu yako na ukarudi kuihifadhi tena baadaye?

Je, umeshawahi kufuta namba ya mtu kwenye simu yako na ukarudi kuihifadhi tena baadaye?

Raymanu KE

JF-Expert Member
Joined
Jan 20, 2022
Posts
8,611
Reaction score
16,118
Waslaam wakuu,

Kuna hili suala ambalo limenitokea mara kadha naomba kuwashirikisha, sijui huwa linawatokea na nyie ama ni mimi pekee yangu tu. Kuna muda ambao una rafiki yako ama mpenzi wako huwa mnaaminia sana, ila ikatokea siku mkaahidiana mambo fulani ila mmoja wenu haswa rafiki/mpenzi wako akayeyusha dili.

Baada ya hiyo ukakasirika sana ukaamua kufuta na namba yake kwenye simu yako, ukaapa kamwe hutokaa umtafute na wala yeye asikutafute tena. Yaani uhusiano uishi hivyo.

Kwa mfano, kama mpenzi wako alikuahidi kwamba atakutembelea kwenye maskani yako jamaa ukaboycott kila kitu ili umsubiri aje, siku inaisha hajatimba gheto na ukimtafuta kwenye simu hapatikani kabisa. Sasa hasira zinakujaa unaamua kukata mawasiliano naye kwa kufuta namba zake kwenye simu yako.

Sasa baada ya wewe kuifuta namba yake muda mfupi baada unaona anakupigia simu pamoja na kututumia ujumbe eti anataka aje. Jamaa unajikuta umeihifadhi namba yake Ttna kwa tabasamu.😂

Kisa cha pili una mshikaji wako mnaelewana sana, siku moja unamuomba akupige tafu na pesa kiasi fulani, hapa tunafikiria ulishamfanyiaga na pesa ndiyo maana unamuomba. Sasa jamaa anakupigia kalenda kwamba atakutumia kama muamala kwenye simu unasikilizia.

Siku inafika umetegea sana ila jamaa hajiongezi na ukipiga simu hapokei wala kujibu ujumbe. Unaona umepigwa fix. Unakasirika unafuta namba yake kwenye simu yako ukaapa kamwe hutokaa umtafute tena. Baada ya siku moja unaona muamala unaingia kwenye simu yako, tena ni maradufu ya ile pesa uliomuomba. Jamaa unabaki kutabasamu na kuhifadhi namba ya jamaa kwenye simu. 😂

Je, wewe ushawahi kufuta namba ya mtu kwenye simu yako na ukarudi kuihifadhi tena?
 
Kujirudi kwa aliyekukosea ni jambo zuri ikimaanisha kaelewa makosa yake, na huyo ndye rafik&mpenzi wa kweli, na hupaswi kutomthameh wala kumbeza.

Lkn kuna hawa wasiojutia makosa yao, hawa ndio kuwapotezea mazima.

Haya mambo ni mengi sana, kuna hawa rafiki tunaweka nao ahadi lkn wanachukulia powa, mim kuna huyu nimempuuza na nimemuweka kwenye list ya watu nitakaowaondoa maishan, haiwezekan rafiki uweke nae ahadi akapuuza na simu zako anazipuuza, sio kwamba haoni, bali anakuchukulia powa, watu kama hawa unatakiwa kuwapa muda na kuwaweka kwenye pending mode kama watabadirika na wasipobadirika waondoe maishan, futa kumbukumbu zao including namba mpaka picha.

Maisha yana mambo mengi tuchoshane na hali ya maisha na bado watu watuchoshe? Hii sio powa....NEXT THEM
 
Nilikiwaga na number za Angelina Jolie baada ya kukutana nae Facebook. Nikamtongoza akanikubalia nikamuomba picha zake akawa ananitumia. Nikamuomba picha ya k nione akanitumia ila kajifunika na pazia. Sasa kuona vile nikaamua kufuta umber zake imepita kama miezi minne kanitafuta akanitumia picha nikafurahi na kutabasamu. Ila sikujua kumbe ana Bwana anaitwa Brad Pitt si akagundua demu ananitumia picha mwamba akazingua kinyama akaniblock kila Kona. Dah nilikuja kupoteza number zake ile simu yangu ya Nokia mawasiliano yake yakapotea ila sijabadilisha namba namsubiria anicheki mana Kuna mtu kanambia eti Ange Kaachana na Brad. Ila dah alikuw anatamani nimzalishe mtoto mmoja wa kiume. Nakumbuka Ange wangu, nakumbuka nilikuwa nimekusave Ange utamu😔
 
Mimi naongoza kwa kufuta namba za watu hafu sijutii wala nini. Cos sipendi sana kua na ukaribu na watu

Lakini pia hua sipendi ujipendekeza, mimi nakutext maraka kadhaa wewe upo kimya lazima niifute namba yako.
 
Back
Top Bottom