Je, umewahi kufanya jambo gani la hovyo mpaka ukajutia?

Je, umewahi kufanya jambo gani la hovyo mpaka ukajutia?

MR.NOMA

JF-Expert Member
Joined
Feb 1, 2014
Posts
339
Reaction score
505
Karibuni wakuu, tushirikishane juu ya jambo lolote la hovyo ,ambalo umewahi kulifanya maishani mwako ,hasa kipindi Cha ujana/ utoto na badae ulijutia. Nianze Mimi,; wakati nipo darasa la 2 nikiwahi kufungulia radio ya mzee , nikaweka Kanda ya lackdube nikasililiza mwanzo mwisho. Lakini bahati mbaya tape ilinasa nikashindwa kuitoa ilibidi niivute nikate na baada ya hapo nilijua viboko vitanihusu mzee akirudi home,nikaamua kwenda kuifukia shambani hiyo kanda yote. Mzee aliporudi alitafta akaikosa.Na alisikitika sana maana alipenda sana kuisikiliza. Huwa najuta , ingekuwa Sasa ningeomba msamaha tu na sio kufanya nilichofanya. Lete stori yako unayojutia , tujifunze
 
Kuna sisi ambao hatuna lolote😅😅
 
Kuna siku bwana nimepata kipotabo flani hivi kitaa. Mtoto kazama gheto kwenye Yale Mambo nikavaa mpira kufanya lile zoezi letu la wakubwa. Kuzamisha TU hivi nikagundua kipotabo kile siku nyingi hajafanya zoezi lile. Imebana vyema ile mbaya. nikaenda nikaenda sa nikawa simwagi Wala Nini si unajua mipira Tenaa. Ikanikera nikatoa na kutupa nikapeleka kavukavu. Duh nilipomaliza nikajilaum Sana kvipi sijatumia mpira . But ndo hivyo Tena najuta but mpaka leo hutokea gheto tunaendelea hivyohivyo.
Inatisha.
 
Nikiwa darasa la sita kila siku nilikuwa ninaibiwa vitabu,penseli,pen n.k kuna siku nikaibiwa Jipime ya hisabati, Nikaona siwezi kuwa mnyonge namna hii, Na mimi nikavizia mida ya mapumziko nikasepa na Jipime moja ya maarifa ya jamii ya jamaa mmoja mstaarabu sana, Kwakweli sikuwahi na sikuwa/sina tabia za wizi, Lakini mpaka leo nikikumbuka natamani ningemrudishia jamaa kitabu chake maana wala hakuongea chochote.
 
Nikiwa darasa la sita kila siku nilikuwa ninaibiwa vitabu,penseli,pen n.k kuna siku nikaibiwa Jipime ya hisabati, Nikaona siwezi kuwa mnyonge namna hii, Na mimi nikavizia mida ya mapumziko nikasepa na Jipime moja ya maarifa ya jamii ya jamaa mmoja mstaarabu sana, Kwakweli sikuwahi na sikuwa/sina tabia za wizi, Lakini mpaka leo nikikumbuka natamani ningemrudishia jamaa kitabu chake maana wala hakuongea chochote.
darasa la 7 nilikuta jamaa anaiba vitu vya wengine sikuwahi kusema hata tulipo pigwa kipigo cha mbwa mwizi. yule jamaa kwa kutosema akawa akiiba lazima anipe mgao
baada ya miaka 15 tukaja kukutana kijiji cha swaya mbeya huko ananikumbusha migao ya wizi
 
Jambo lingine ninalokumbuka ,nikiwa kidato Cha 4 usiku,huku kesho yake tukiwa tunaanza mitihani ya taifa niliwahi kuacha kusoma prepo usiku baada ya kufuatwa na washkaji tukasolve paper ya hesabu imevuja eti Kuna mwana anayo basi tulikomaa tukisolve paper fake kuanzia saa 4 usiku mpaka saa 9, by saa 10 ndio nikarudi geto kulala, nikapitiliza badala ya kuamka saa 12 nikaamka saa 1:30 ,nikachelewa chumba Cha mtihani. Na Ile kuingia kwenye paper kumbe sio lenyewe. Nilijuta sana, mpaka Leo siamini kama Kuna mtihani Huwa unavuja Bali ni matapeli tu huwapig pesa watu kwa kuja na paper fake.
 
Kila nilienda pale bar nahisi kutengwa najutia mno. Nilielewa maana ya kuwa amani na kunywa na marafiki kumeishia tangu siku hiyo. Nimejiona bwege kwelikweli.

Emergine hata bar maid hataki kukaa na Wewe??

Hasira ni hasara, najifunza kutokuwa na hasira hata ukinishika tako nawaza nitachukuliaje Hali hiyo.

Nahisi ninaweza kuwekewa kitu cha kuondoa uhai niwapo pale bar.

Marafiki wananitenga nk. Yaani inauma Sana. Uzir Kino bar hapa ni nyingi lkn Kuna Ile ya Wana.
 
Karibuni wakuu, tushirikishane juu ya jambo lolote la hovyo ,ambalo umewahi kulifanya maishani mwako ,hasa kipindi Cha ujana/ utoto na badae ulijutia. Nianze Mimi,; wakati nipo darasa la 2 nikiwahi kufungulia radio ya mzee , nikaweka Kanda ya lackdube nikasililiza mwanzo mwisho. Lakini bahati mbaya tape ilinasa nikashindwa kuitoa ilibidi niivute nikate na baada ya hapo nilijua viboko vitanihusu mzee akirudi home,nikaamua kwenda kuifukia shambani hiyo kanda yote. Mzee aliporudi alitafta akaikosa.Na alisikitika sana maana alipenda sana kuisikiliza. Huwa najuta , ingekuwa Sasa ningeomba msamaha tu na sio kufanya nilichofanya. Lete stori yako unayojutia , tujifunze
Nilikuwa nadate na mdada Fulani akaniambia kanasa ujauzito nikamwambia sijawa tayari kulea mimba tuitoe alikataa nilimlazimisha Sana akakubali kuitoa.
Baada ya mwaka mmoja kupita nikawa nadate na mdada mwingine akasema kashika mimba,nililea toka mimba Hadi kajifungua mtoto. Baadae nimekuja kujua siyo mwanangu. Huwa najuta Sana nasema yawezekana ni Ile laana ya kutoa mimba.
 
Back
Top Bottom