[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] nilikuwa cr mwaka wa kwaza nikawa nawapelekesha yaani sitaki ujinga wala shobo na kiburi cha asili [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] mwaka wa pili wakati wa kuchagua cr wakanikataa kwakishindo [emoji23][emoji23][emoji23] ndipo atakoea rafik yangu akasema ujue watu wanakukubali sana sema hujui gombea urais jaman nilijawa na kichwa balaa [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Nikaenda kuchukua fomu mimi huyu kuaza kupiga kampeni siku ya siku kufika nilipata kula 7 wakawa wananiita 7up [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Nikaja ludishwa ucr mwaka wa tatu kwa figisu figisu [emoji23][emoji23][emoji23] nikawa na kiburi rais akanitoa class wakagoma kuchagua mwingine wakawa bado wananitaka ase [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] nikapita tena kwa kishindo
Jinga sana umenifurahisha sana japo pole pia mwamba .
Nilikuwa nikikaa na wazee kwenye kahawa natoa mapoint pasipokujua nayachota jf
Basi bana wakasema wewe unafaa kuwa kiongozi miaka ikakata na muda ukaenda .
Basi siku ya siku nafuatwa na wazee wa rika la babu yangu na baba yangu eti wanataka nigombee ubunge kupitia chama cha mapinduzi .
Hapo ndipo nikajua shetani ni msaliti maana bichwa lilinijaa nikasema duh kumbe nakubalika hivi [emoji3]
Basi bwana nikawa nawaza hapa nikope mzigo wa kutosha benki alafu nitangaze nia alafu mambo ya kazi niyaweke pending [emoji16]
Duh hapa ndipo nilijua watumishi wa serikali ni wanafiki sana yaani wote ofisini ni full kunisifia yaani wewe unafaa na lazima upite ukifeli basi lazima kuna teuzi utakula .
Kweli bichwa langu likafuata maneno yao nikagombea kwenye uchaguzi ndani ya chama duh nikaambulia kura 2(mbili) [emoji23]
Huku na mzee Magu akadai kama uliacha kazi kwenda kwenye kugombea ubaki huko huko [emoji848]
Basi bwana wapambe wote wakanitenga na ndugu wakaanza kunitenga eti nimeacha kazi kwenda kwenye siasa .
Nilihonga wajumbe vichenji ila mzigo wenyewe nilikuwa nao bado .
Basi stress na kutrngwa na jamii nikaamua kuwa mtu wa bar na pia nikawa nafanya matanuzi ya kufuru oyaaaa binadamu sio watu acha waanze kunirudia mara ooh wanasikia kuna kitengo nimekula [emoji3]
Mimi sina habari ni mwendo wa kuitumbua hela ya mkopo dah stress zinaonhezeka japo wao wanadhani mimi nina maisha kumbe ni mkopo na pia wanadhani nina kitengo nishakula .
Dah Mungu mwema nilikuja kurudishwa kazini kwa mbinde baada ya kuhonga sana na kujinyenyekeza sana .
Ule ujinga siwezi sahau mpaka leo nipo nalipa madeni ya benki taratibu huku namlaani Magufuli na wajumbe pamoja na wanafiki wote walionijaza ujinga .
Mitanzania ni minafiki sana [emoji57]