Je una uzoefu gani kwenye usafiri wa mabasi?

Je una uzoefu gani kwenye usafiri wa mabasi?

Damaso

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2018
Posts
3,978
Reaction score
6,739
Katika zama hizi za utandawazi, usafiri umekuwa sehemu muhimu ya maisha yetu ya kila siku. Tunaweza kusafiri kwa ndege, treni, basi, gari, pikipiki, au hata kwa miguu. Hata hivyo, pamoja na urahisi huu wote, bado tunakabiliwa na changamoto nyingi, ikiwa ni pamoja na ucheleweshaji, ajali, na huduma mbovu za vyakula.
1734171107456.jpg


Mwaka wa 2020, nilisafiri kutoka Mwanza kuelekea Dar es Salaam kwa basi la Kisesa. Safari hiyo ilikuwa ndefu na yenye changamoto nyingi, na hatimaye nililazimika kushukia Dodoma kutokana na matatizo ya mara kwa mara ya basi hilo. Majanga yalianzia Tinde kwenye mizani, gari lilizima na ikabidi dereva na watu wachache kusaidia kutatua tatizo, ila baada tena tukiwa Tabora gari ikazima kwa mara nyingine.
1734171102300.jpg


Tokea tumeanza safari Nyegezi niliona wazi kuwa Basi hili halipo sawa, sikutaka kumshawishi mtu yoyote kuteremka ila nilitumia ubinadamu kuwaomba niteremke Dodoma ingawa safari iliikuwa ni ya kwenda Dar es Salaam ili tu nisipate karaha zaidi.

Naomba kukualika kushiriki uzoefu wako wa usafiri. Ni nini kilichokuwa kibaya zaidi? Je, uliwahi kusafiri kwa gari iliyokuwa katika hali mbaya? Je, umewahi kukwama barabarani kwa muda mrefu? Je, umewahi kupata ajali ya barabarani?
1734171107456.jpg


Ulipata huduma ya chakula kibaya? Kusimamishwa na maafisa usalama? Unaweza kushare chochote? Hadithi yako inaweza kuwa ya kuchekesha, ya kusikitisha, au hata ya kutisha. Kama Jamii tunaomba kusikia kutoka kwako! Wapo waliopata wachumba, waliopata connection za kazi na kadhalika.
1734171102300.jpg


Kwa kushiriki uzoefu wako wa usafiri, tunaweza kuunganisha pamoja na kujenga jamii yenye uelewa zaidi kuhusu changamoto za usafiri. Tunaweza pia kuhamasisha mabadiliko katika sekta ya usafiri kwa kuwajibisha makampuni ya usafiri na mamlaka husika.

KARIBUNI SANA!
 
Katika zama hizi za utandawazi, usafiri umekuwa sehemu muhimu ya maisha yetu ya kila siku. Tunaweza kusafiri kwa ndege, treni, basi, gari, pikipiki, au hata kwa miguu. Hata hivyo, pamoja na urahisi huu wote, bado tunakabiliwa na changamoto nyingi, ikiwa ni pamoja na ucheleweshaji, ajali, na huduma mbovu za vyakula.
View attachment 3176436

Mwaka wa 2020, nilisafiri kutoka Mwanza kuelekea Dar es Salaam kwa basi la Kisesa. Safari hiyo ilikuwa ndefu na yenye changamoto nyingi, na hatimaye nililazimika kushukia Dodoma kutokana na matatizo ya mara kwa mara ya basi hilo. Majanga yalianzia Tinde kwenye mizani, gari lilizima na ikabidi dereva na watu wachache kusaidia kutatua tatizo, ila baada tena tukiwa Tabora gari ikazima kwa mara nyingine.
View attachment 3176437

Tokea tumeanza safari Nyegezi niliona wazi kuwa Basi hili halipo sawa, sikutaka kumshawishi mtu yoyote kuteremka ila nilitumia ubinadamu kuwaomba niteremke Dodoma ingawa safari iliikuwa ni ya kwenda Dar es Salaam ili tu nisipate karaha zaidi.

Naomba kukualika kushiriki uzoefu wako wa usafiri. Ni nini kilichokuwa kibaya zaidi? Je, uliwahi kusafiri kwa gari iliyokuwa katika hali mbaya? Je, umewahi kukwama barabarani kwa muda mrefu? Je, umewahi kupata ajali ya barabarani?
View attachment 3176436

Ulipata huduma ya chakula kibaya? Kusimamishwa na maafisa usalama? Unaweza kushare chochote? Hadithi yako inaweza kuwa ya kuchekesha, ya kusikitisha, au hata ya kutisha. Kama Jamii tunaomba kusikia kutoka kwako! Wapo waliopata wachumba, waliopata connection za kazi na kadhalika.
View attachment 3176437

Kwa kushiriki uzoefu wako wa usafiri, tunaweza kuunganisha pamoja na kujenga jamii yenye uelewa zaidi kuhusu changamoto za usafiri. Tunaweza pia kuhamasisha mabadiliko katika sekta ya usafiri kwa kuwajibisha makampuni ya usafiri na mamlaka husika.

KARIBUNI SANA!
Wacha tuu!Damoso.
 
Katika zama hizi za utandawazi, usafiri umekuwa sehemu muhimu ya maisha yetu ya kila siku. Tunaweza kusafiri kwa ndege, treni, basi, gari, pikipiki,
Mimi siku moja nilisafiri kutoka Rombo kwenda Mwanza miaka kadhaa iliyopita.
Kuna magari yalikuwa yanaunganisha Rombo Hadi Mwanza.
Sasa bana kufika njia panda Himo kijana mmoja km wa miaka 18-25 akaingia akawa amekaa siti ya mbele yangu upande wa kushoto,abiria wakaendelea kuingia km kawa .Tulipofika Arusha akaingia mmama mmoja na kapu lake na watu wengine wakaingia safari ikaendelea.Tulipotoka Arusha Yule kijana akatoa pafyumu akaanza kupulizia kabegi kake kadogo alikokuwa amekaweka kwenye carrier ndani.
Mimi nikawa namtazama na sikuekewa chochote.
Hakusema na mtu yooyote akawa baada ya muda analipulizia .
Eee bwaneeee,kufika makuyuni gari ikapelekwa kituo Cha piolisi ,tukaambiwq Ni ukaguzi kwani inasemekana kuwa tumebeba dawa za kulevya,kufumba na kufumbua lile kapu la Yule mama nikalikuta karibu na miguu yangu,pembeni ya abiria mwenzangu.
Polisi wakaingia ndani,wakaanza kunusa mabegi yote yaliyokuwa ndani.
Wakalichukua like begi la kijana na kuuliza Hilo Ni la Nani,kijana akakaa kimya,na watu wote tutakaaa kimya,wakalichukua wakashuka nalo.
Walipofika pale kwenye siti yangu,wakachukua kapu kutuelekeza mwenye kapu,Mimi na abiria aliyekuwa jirani tushuke tuambatane nao.
Tukaingizwa pale kaunta ya polisi,wakatuhoji kidogo Mimi nikasema hili kapu sii langu na sijui kilichomo.
Wakamwambia mama mwenye kapu abaki,Mimi na jirani tukaambiwa tuingie kwa gari.
Gari ikaanza safari Tena,Sasa Yule kijana akaanza kupiga simu mfululizo,anamwambia wa kwenye simu kuwa mzigo umeshushwa makuyuni kituo Cha piolisi.
Baadae kijana akampigia mtu mwingine na kumwambia kuwa mzigo umeshushwa Ila bosi kamwambia asiwe na wasiwasi aendelee na safari kwani mzigo utawekwa kwenye gari nyingine na yeye itabidi ashuke babati ili aupokee.
Kijana akawa very relaxed na alivyofika babati akashuka ,kilichoendelea sijui.
Ila kwa ujumla nilishtuka sàna,Yule mama alikuwa anataka kuniingiza matatizoni,kusogeza kapu upande wa miguu yetu.
Nikajifunza kuwa makini Sana kwenye safari,huko Kuna mengi Mambo mengi na unaweza pata msala kizembe kabisa.
 
Mimi siku moja nilisafiri kutoka Rombo kwenda Mwanza miaka kadhaa iliyopita.
Kuna magari yalikuwa yanaunganisha Rombo Hadi Mwanza.
Sasa bana kufika njia panda Himo kijana mmoja km wa miaka 18-25 akaingia akawa amekaa siti ya mbele yangu upande wa kushoto,abiria wakaendelea kuingia km kawa .Tulipofika Arusha akaingia mmama mmoja na kapu lake na watu wengine wakaingia safari ikaendelea.Tulipotoka Arusha Yule kijana akatoa pafyumu akaanza kupulizia kabegi kake kadogo alikokuwa amekaweka kwenye carrier ndani.
Mimi nikawa namtazama na sikuekewa chochote.
Hakusema na mtu yooyote akawa baada ya muda analipulizia .
Eee bwaneeee,kufika makuyuni gari ikapelekwa kituo Cha piolisi ,tukaambiwq Ni ukaguzi kwani inasemekana kuwa tumebeba dawa za kulevya,kufumba na kufumbua lile kapu la Yule mama nikalikuta karibu na miguu yangu,pembeni ya abiria mwenzangu.
Polisi wakaingia ndani,wakaanza kunusa mabegi yote yaliyokuwa ndani.
Wakalichukua like begi la kijana na kuuliza Hilo Ni la Nani,kijana akakaa kimya,na watu wote tutakaaa kimya,wakalichukua wakashuka nalo.
Walipofika pale kwenye siti yangu,wakachukua kapu kutuelekeza mwenye kapu,Mimi na abiria aliyekuwa jirani tushuke tuambatane nao.
Tukaingizwa pale kaunta ya polisi,wakatuhoji kidogo Mimi nikasema hili kapu sii langu na sijui kilichomo.
Wakamwambia mama mwenye kapu abaki,Mimi na jirani tukaambiwa tuingie kwa gari.
Gari ikaanza safari Tena,Sasa Yule kijana akaanza kupiga simu mfululizo,anamwambia wa kwenye simu kuwa mzigo umeshushwa makuyuni kituo Cha piolisi.
Baadae kijana akampigia mtu mwingine na kumwambia kuwa mzigo umeshushwa Ila bosi kamwambia asiwe na wasiwasi aendelee na safari kwani mzigo utawekwa kwenye gari nyingine na yeye itabidi ashuke babati ili aupokee.
Kijana akawa very relaxed na alivyofika babati akashuka ,kilichoendelea sijui.
Ila kwa ujumla nilishtuka sàna,Yule mama alikuwa anataka kuniingiza matatizoni,kusogeza kapu upande wa miguu yetu.
Nikajifunza kuwa makini Sana kwenye safari,huko Kuna mengi Mambo mengi na unaweza pata msala kizembe kabisa.
Ubarikiwe sana 😢 kuna la kujifunza hapa
 
Kwa uzoefu nilionao kwenye usafiri wa Bus hata siku moja huwa sikai siti ya dirishani
 
Back
Top Bottom