Je, Unafikiriaje kuanzishwa kwa Sarafu Mpya kwa Nchi za BRICS italeta manufaa?

Je, Unafikiriaje kuanzishwa kwa Sarafu Mpya kwa Nchi za BRICS italeta manufaa?

Sarafu Mpya kwa Nchi za BRICS.

Nchi za BRICS zinaripotiwa kufanya kazi katika kuunda aina mpya ya sarafu na mpango wa kuwasilisha maendeleo yake katika mkutano wa kilele wa viongozi wa BRICS mnamo Agosti mwaka huu, Naibu Mwenyekiti wa Jimbo la Duma Alexander Babakov alisema Alhamisi kando ya Jukwaa la Biashara la India na Urusi huko New Delhi.
View attachment 2573724
Kongamano hili linaashiria kuanza kwa matukio ya kimataifa katika Kongamano la Kiuchumi la Kimataifa la St. Petersburg 2023. Afisa huyo mkuu wa Urusi alinukuliwa akisema:

"Mpito kwa makazi katika sarafu za kitaifa ni hatua ya kwanza. Inayofuata ni kutoa mzunguko wa dijiti au aina nyingine yoyote ya sarafu mpya katika siku za usoni."

Kwa mujibu wa waziri wa mambo ya nje ya Urusi aitwae Sergey Lavrov alisema kuna Nchi nyingi takribani 20 zimeonyesha nia ya kujiunga na jumuiya hiyo ya kiuchumi, zikiwemo Argentina, Iran, Indonesia, Mexico, UAE, Uturuki, Saudi Arabia, Algeria, Misri na Nchi nyingi za Afrika. Afrika Kusini itakuwa mwenyeji wa mkutano ujao wa BRICS mwezi Agosti, 2023 ambapo waliotuma maombi ya kujiunga na umoja huo yatajadiliwa.
View attachment 2573735
Masuluhisho kwa sarafu ya kitaifa yameanza miongoni mwa mataifa ya BRICS. Hivi majuzi, Rais wa Urusi Vladimir Putin na Rais wa China Xi Jinping walikubaliana kupitisha Yuan ya Uchina kama sarafu ya makazi na nchi zinazoinukia kiuchumi. Serikali ya China pia imetia saini mkataba wa pande mbili na Brazil kuwezesha biashara kwa kutumia sarafu zao za kitaifa.

Tujadiliane sasa ili jambo mnalionaje ndugu zangu, USA na washirika wake wa EU wataendeleza sanctions amah!!!?
Wamesha tepete na vigezo vinavuja vilivyo,ni matokeo ya misimamo ya Uturuki,Hungury,nawengine wengi wanagombea maamuzi ya kuburuzwa dhidi ya Ukraine 🤔
 
Ni muungano kama wa G7 ila wenye washirika ambao wengi wao hawafuati Demokrasia
Wana tofauti nyingi sana katika siasa zao. Hali inayopelekea utofauti mkubwa sana wa sera, malengo na mipango yao ya kiuchumi.

Kuna ambao ni democratic kwa kiasi fulani, huku wengine wakiwa ni authoritarian waliokamilika wenye marais wa maisha.
 
Itakua hatua nzuri kwa nchi za Brics kuanza kujinasua kutoka kwenye utegemezi kwa nchi za EU na USA. Shida ni moja tu nchi za Brics kwao demokrasia ni sumu, kwaio unaweza ukawa mfumo flani ambao viongozi wataona fresh ila wananchi wasifuraishwe
Ila Brazil na South Africa si wana practise western democracy na hata mashoga wanapata haki zote za kufanya ushenzi wao.
 
Ila Brazil na South Africa si wana practise western democracy na hata mashoga wanapata haki zote za kufanya ushenzi wao.
Yah ila wakubwa wa umoja (Russia na China) wapo tofauti na hiyo na ndio wenye ushawishi zaidi kwa wengine. Sijajua itakuaje lakini
 
Itaamsha vita ya 3 ya dunia kutokana na ushindani mkali kwa sababu zifuatazo:-

1. BRICS inataka ku-replace WB, IMF na WTO, ikiwezekana na ADB.

2. BRICS inataka ku-replace nguvu za sarafu za USD na EURO duniani.

Sent from my SM-A260F using JamiiForums mobile app
Kwa sababu Gani baadhi ya watu kwa utashi wao na kidemokrasia kabisa kujiamlia mlengo wao kutaka kuachana na Dola ,IMF na WB watu wengine wamzishe vita ya Dunia?
Mbona vyombo hivyo vipo Sasa hivi na havikuletwa kwa vita?
Wivu ni kitu kibaya sana,muda ukifika umefika TU.
Mida wao wa kutawala umekwisha wakubali matokeo kiungwana TU.
Mbona USD ili replace pound hakukua na vita?
Mbona euro imereplace pound hakukua na vita?
Kwa Nini itokee vita Kwa Brics kuweka sarafu itakayo replace USD na vita itokee?
 
Tatizo la BRICS ni muungano ambao hauna misingi ya kipekee (common interests and values) ambayo inaziunganisha hizo nchi, tofauti na miungano mingine kama vile EU ama G7.

Tofauti zao ni kubwa sana kiasi kwamba inawawia vigumu kufikia muafaka katika jambo ambalo wote watakuwa na maslahi nalo.

Ukitazama mifumo yao ya kisiasa ya ndani, ni tofauti kabisa. Tukija kwenye malengo na maslahi ya kila mmoja, uhasama ni mkubwa.

Members wawili wenye uchumi mkubwa zaidi katika huo muungano (China na India) ni mahasimu wakubwa. Migogoro ya kimipaka n.k. imepelekea ugomvi wa muda mrefu.

Je, suala lolote lile linalohitaji muafaka ambalo litaonekana kuwa na maslahi zaidi kwa China, hasimu wake (India) italikubali? Na kinyume chake pia, China itaridhia?

Tofauti, uhasama na migogoro ya aina hii ni vigumu kuleta muafaka wenye maslahi ya pamoja.
Aisee eti tatizo la nchi za Brics ni muungano amabao Haina misingi ya kipekee amabyo inaziunganisha nchi hizo ofauti na EU pamoja na G7.
Dah.
Kuna watu mna akili sana aisee.
Yaani wewe jamaa una akili kuliko wataalamu wote wa nchi zote Tano za Brics,yaani wataalamu wa uchumi na mipango wa nchi hizo wewe umewazidi kufikiri.yaani wabunge wao,mawaziri wao,wachumi wao na wasomi wao waliokubaliana kuunda umoja huo kwako wewe ni weupe TU lakini wewe ambae naamini hata ukuu wa wilaya TU hapa kwetu huna.
Sasa ona maajabu.
EU ni muungano wa nchi zinazotokea eneo moja yaani ulaya.ingawa sio nchi zote za ulaya ni memba wa EU.
Pointi yangu hapa ni kwamba Kuna nchi ni wanachama kwa sababu TU zipo eneo hili,lakini ni masikini kuliko baadhi ya nchi za Brics.kwa hiyo sioni u special wa muungano wao zaidi ya kua wanatokea eneo moja
Mfano mzuri wa EU ni kama EA na AU.

Haya njoo kwa G7.
Huu ni umoja kama club TU na kimuundo umezidiwa hata na Brics amabo wewe unajitia kuuponda.ingawa unafanana kijiografia TU
Brics sio kama EU amabo wanatokea sehemu moja Brics imeanzishwa kwa kufuta uwakilishi wa maeneo .mfano kutokea Afrika,Amerika na Asia.

Sasa ona kituko Cha G7 hawa ni kama klabu TU.tunaambiwa ni umoja wa nchi 7 tajiri duniani.

Lakini ukiangalia Kuna nchi ziko ndani ya kundi hilo zimepitwa kiutajiri na baadhi ya nchi zilizo nje ya kundi hilo,mfano china Iko nje lakini imezipita nchi kadhaa za G7.
Urusi iliingizwa ndani ya kundi hilo,lkni ilipoitwaa krimea ikafukuzwa,Sasa hapa najiuliza kwa kuitwaa krimea Urusi ilifiriaiaka na kupoteza sifa?
Kimsingi kama iliingizwa kwa sababu ni tajiri,basi kuivamia Crimea hakuiondolei sifa yake. Ndio nikajua kundi hilo ni la kinafiki TU,mtuvmmoja akiamua Fulani aingizwe anaingizwa,mtu huyohuyo akichukizwa na mtu mwingine anaamua atolewe.

Hata hivyo kijiografia G7 inafanana TU na Brics,G7 Kuna nchi inatokea Amerika,nyingine Asia na nyingine Europe Haina tofauti na Brics.

Sasa wewe ndugu yetu unawezaje kuiona Brics Ina tatizo na haitafanikiwa?
Kama migogoro ya nchi za Brics ni issue mbona Hadi Leo wapo pamoja miaka karibu 20 Sasa?
 
Wana tofauti nyingi sana katika siasa zao. Hali inayopelekea utofauti mkubwa sana wa sera, malengo na mipango yao ya kiuchumi.

Kuna ambao ni democratic kwa kiasi fulani, huku wengine wakiwa ni authoritarian waliokamilika wenye marais wa maisha.
Kwa hiyo Brics haitafanikiwa?
Itavunjika?
Je haya mataifa yanayogombea kujiunga hawana akili?
Je Brics Ina umri Gani Sasa hivi?
 
Ndugu mtoa mada nakuhakikishia kua Brics inaenda kua umoja mkubwa sana hapa duniani na utakua umoja fair kabisa kuliko umoja zote za kinyonyaji zilozoanzishwa.
Sarafu ya Brics inaenda kupokelewa kwa furaha na mataifa mengi sana hapa duniani kwa sababu sio sarafu ya kinyonyaji na ya kikandamizani kama USD .sarafu ya USD iliyumika kama fimbo.sarafu ya Brics ni ya Dunia nzima.
Hata ukiangalia muundo wa umoja wa Brics ulianza kwa uwakilishi,wapo memba kutoka Amerika ,Afrika ,Asia na east Europe.
Hakuna unyanyasaji ndani ya Brics na ndio maana Sasa Kuna wimbi kubwa mno la nchi zilizoomba kujiunga na Brics.
Sarafu itakayoundwa na Brics itakua na sura ya sarafu halali ya kidunia kwa sababu ya uwakilishi na nchi nyingi zimejitokeza kujiunga bila shuruti.

Hebu fikiria Afrika tunawakilishwa na south Afrika ndani ya Brics na Kuna nchi nyingine za Afrika zitaomba kujiunga huko tuendako.

Pia mtoa mada subiri mwezi august Brics inaenda kusajili wanachama wapya huko south Afrika.

Hivi nchi kama Soud Arabia,Iran, Argentina Algeria, turkey na nchi kibao zinaweza kua na Viongozi wajinga kweli kutaka kujiunga na Brics?
 
Tatizo la BRICS ni muungano ambao hauna misingi ya kipekee (common interests and values) ambayo inaziunganisha hizo nchi, tofauti na miungano mingine kama vile EU ama G7.

Tofauti zao ni kubwa sana kiasi kwamba inawawia vigumu kufikia muafaka katika jambo ambalo wote watakuwa na maslahi nalo.

Ukitazama mifumo yao ya kisiasa ya ndani, ni tofauti kabisa. Tukija kwenye malengo na maslahi ya kila mmoja, uhasama ni mkubwa.

Members wawili wenye uchumi mkubwa zaidi katika huo muungano (China na India) ni mahasimu wakubwa. Migogoro ya kimipaka n.k. imepelekea ugomvi wa muda mrefu.

Je, suala lolote lile linalohitaji muafaka ambalo litaonekana kuwa na maslahi zaidi kwa China, hasimu wake (India) italikubali? Na kinyume chake pia, China itaridhia?

Tofauti, uhasama na migogoro ya aina hii ni vigumu kuleta muafaka wenye maslahi ya pamoja.
Common interest ni kuondoa Unipolar world kwenda Multipolarity. Kila mtu aheshimiwe sio mtu akikuazima mkopo anakufosi uwe shoga au ugombane na majirani
 
FACT CHECK: Hakuna uthibitisho wowote kuhusu hiyo picha ya pili uliyoambatanisha na maelezo yaliyomo.

Maandishi katika hiyo picha yanaeleza kwamba Putin alikaa Tanzania kwa miaka minne (1973-1977) akitoa mafunzo kwa wapigania uhuru huku katikati kukiwa na mtu anayetajwa kama Samora Machel na pembeni yake, Mnangagwa.

Fact ni kwamba, katika hiyo miaka inayotajwa, Putin alikuwa mwanafunzi wa chuo kikuu na alihitimu mwaka 1975, ambao ndio mwaka aliojiunga KGB, wakati wote huo akiwa USSR.

Swali la kushangaza kidogo:
Aliwezaje kuwa USSR kama mwanafunzi wa chuo kikuu na wakati huohuo akawa Tanzania akitoa mafunzo ya kijeshi kwa miaka minne?

Swali jingine:
Hiyo miaka inayotajwa kwamba alikuwa Tanzania, alitoa hayo mafunzo kama nani wakati hakuwa mwanajeshi wa ngazi yoyote ile ilhali mtu anayeonekana pichani ni mwanajeshi mwenye mavazi rasmi ya kijeshi?

Jambo jingine, wakati picha inapigwa (mwaka 1973), huyo Mnangagwa anayetajwa hapo ambaye kwa sasa ni rais wa Zimbabwe, alikuwa gerezani akitumikia kifungo cha miaka kumi tangu mwaka 1965 kwa makosa ya uhujumu uchumi ambako huko ndiko alikutana na Mugabe kisha kuunda urafiki wa karibu.

Maana yake ni kwamba, maelezo yaliyomo katika picha husika hapo si maelezo yenye ukweli wala uthibitisho wowote ule.
Labda nami nikuulize; iliwezekanaje Mseveni kuwa mwanafunzi wa chuo kikuu Cha Dar es salaam, huku akiongoza kikosi cha waasi huko msumbiji na kushiriki operation mbalimbali na baadaye kuweza kufanya mapinduzi yaliyo muweka madarakani Uganda?

Nikwambie tu Kwenye ulimwengu huu wa ujasusi kila kitu kinawezekana, ikiwemo utumiaji wa fake identity. Mtu aweza onekana kuwa ni mwanafunzi, muuguzi au mwalimu lakini kumbe bonge la jasusi. Anaweza tumia identity ya uanafunzi kusafiri overseas ikidhaniwa anaenda kufanya research kumbe mamlaka zimetaarifiwa kuwa huyo ndo kitengo chenyewe, mpeni kila aina ya ushirikiano. Na hii hufanyika ili kuepusha hujuma iwapo huyo mtu akitambulika mapema kwa upande wa adui.
 
Labda nami nikuulize; iliwezekanaje Mseveni kuwa mwanafunzi wa chuo kikuu Cha Dar es salaam, huku akiongoza kikosi cha waasi huko msumbiji na kushiriki operation mbalimbali na baadaye kuweza kufanya mapinduzi yaliyo muweka madarakani Uganda?

Nikwambie tu Kwenye ulimwengu huu wa ujasusi kila kitu kinawezekana, ikiwemo utumiaji wa fake identity. Mtu aweza onekana kuwa ni mwanafunzi, muuguzi au mwalimu lakini kumbe bonge la jasusi. Anaweza tumia identity ya uanafunzi kusafiri overseas ikidhaniwa anaenda kufanya research kumbe mamlaka zimetaarifiwa kuwa huyo ndo kitengo chenyewe, mpeni kila aina ya ushirikiano. Na hii hufanyika ili kuepusha hujuma iwapo huyo mtu akitambulika mapema kwa upande wa adui.
Acha porojo, Putin hajawahi kufika Tanzania wala hajawahi kuwa mkufunzi wa kijeshi.
 
Back
Top Bottom