Je unajua "hili" kuhusu Tume ya Warioba?


nimekuwa mpole ghafla, haya bhana!
 
sasa huoni wameacha maoni mengi ya wananchi hasa ya wakuu wa mikoa na wilaya, bado wananchi tunalia na wakuu wa mikoa na wilaya!

pamoja mkuu, tupiganie liongezwe hili lakini siyo kuondoa kilichowekwa tayari
 
sheria nimeisoma ila sijaona mahali ambapo swali langu hili limejibiwa kwa ufasaha
ama mimi sijui kuitafsiri sheria husika naomba nisaidie kwakweli

upo sahihi, jibu lako halipo pale!
 

MMK mimi niliitafsiri kwamba tume ya kukusanya maoni ya katiba ni ili iwepo ama isiwepo basi lakini siyo kukusanya yatakayokuwemo kwenye katiba hiyo.
kwann nasema hivyo mbona maoni ya wananchi hayapewi kipaumbele???
mfano kuna mzee alipropose katiba itamke kwamba serikali ziwe moja tu, na kusiwe na dola mbili ila wakati wa mjadala hii iliambiwa sio mahali pake nikajiuliza sasa mahali sahihi pa kuongelea hili ni wapi?? ama je hii tume inamipaka ya nii kijadiliwe na nini kisijadiliwe kwenye hii katiba??
 
Eneo moja katika Rasimu hii ya Katiba inanipa taabu kwa mtindo uliotumika, sehemu ya mfumo wa utawala na hasa aina ya muungano. Yalikuwa maoni yangu kuwa tulitakiwa kwanza kuwa na kura ya maoni ili kutafuta aina ya muungano tuutakao kabla ya kuingizwa kwenye Katiba. Hii inahakikisha maoni ya wengi ndiyo yanafuatwa. Njia hii iliyotu ika haihakikishi maoni ya wengi bali matakwa ya Tume kwa muono wao. Ndiyo maana Mh Warioba anadema maoni ya wengi yalikuwa hivi na sababu za msingi zilitolewa lakini Tume imeamua tofauti....
 


You are proving my point; Katiba kama inatoka kwa wananchi; kama wananchi wanataka turudi kwenye mfumo wa chama kimoja na wengi wao wanataka hivyo wao Tume ni nani hadi wawakatalie wananchi? Hapa pia najibu hoja ya Pasco.. hivi kama kweli Tume ya kina Marmo ingewasikiliza wananchi na kuacha nchi kwenye mfumo wa chama kimoja na badala yake kuboresha demokrasia ya chama kimoja (kama ilivyo China) unafikiri tungekuwa wapi? Nina uhakika mgawanyiko mkubwa wa taifa wa leo hii usingekuwepo!

Na utaona kuwa kwa muda wote huu CCM bado inakubalika kwa karibu asilimia 80 hivi; je Wananchi miaka ishirini iliyopita walikuwa sahihi?
 

Mkuu maoni yako ni mazuri na yenye mantiki; Kama huwezi kupata unachohitaji chukua unachopewa Na songa mbele
 
Ishu ya wakuu wa mikoa na wilaya yatajadiliwa katika Katiba ya Tanganyika
 
ilichofanyika ni kuwa walikuwa WANASIKILIZA MAONI YA WATU kama adventure ila wana rasimu yao tayari.

Hii ndiyo hofu yangu; kwamba walishajua wanataka kitu gani na kwa kutumia nafasi zao kama tume wakakipendekeza. Hivi mmejiuliza watu wangapi walisema nchi igawanywe katika majimbo 25?
 
Tutoe maoni, tupate katiba!, vinginevyo we'll be back to squire one!.

Pasco.

Kutoa maoni kunahusiana vipi na kupata Katiba kama Katiba inaweza kupatikana bila kujali maoni yanayotolewa?
 
Wewe sasa unakotaka kutupeleka siko unalako jambo kama hujatumwa basi mnampango wa kuruga mchakato wa katiba ila hamtafanikiwa kamwe.
 
Katiba haitoweza kuwa na maoni na matakwa ya kila Mtanzania! ni lazima tukubaliane na mtengamano wa mgongano wa mawazo, Rasimu iliyotolewa na tume ya warioba bado inatuhitaji sisi wananchi tuijadili na kutoa mapendekezo yetu kupitia mabaraza ya wilaya au babaraza ya makundi mbalimbali, pia kupitia wabunge wetu katika bunge maalum la katiba!
Cha msingi makundi yote yenye mlengo wa kulia, kushoto au wa katikati (Vyama vya siasa, taasisi za kidini, asasi za kiraia) wajipange kuwaelimishe wananchi juu ya ustawi wa taifa utakaopatikana kupitia katiba yenye mlengo au mfumo fulani! ili kupata marekebisho sahihi kipindi hiki cha mchakato na mwisho wa siku Watanzania tuseme NDIO au HAPANA kwa haki na mustakabali wa TAIFA LETU na isiwe kwa kuburuzwa!
 

Ndugu Je kilicholetwa kinamapungufu?
Je rasimu inapingwa na wengi?
Je rasimu inapendelea kundi fulani?
Je kuna ushahidi kuwa rasimu sio maoni ya wananchi?
 
Tanzania ni nchi ya "kusadikika",

Mtu yoyote anayetegemea CCM na makada wake wafanye kitu tofauti si vibaya tukamkumbusha tafsiri isiyo rasmi ya "insanity"

"Doing the same thing over and over again expecting different results"
 

Wasalaamu waungwana
Binafsi nashawishika kuamini kwamba yale yote yaliyomo katika rasmi ya Warioba yamewekwa wazi ili yaweze kujadiliwa. Labda kama hiyo rasimu iko out of discussion. At STP the rasimu better by far compared to what was expected (taking into consideration the composition of the tume itself). Hata hivyo itakuwa .ni kuwakosea heshima wajumbe wa tume hiyo tukisema kwamba hakuna kilichofanyika. Pengine tume hii ingekuwa ni ya kijinga kuliko tume zote zilizowahi kuwapo kama kweli ingefanya kazi ya kutuletea kila kilichosemwa na wananchi. Tume ilitakiwa na ndicho ilchofanya, kusikiliza na kuyaoganise mawazo hayo ili kuleta kitu cha maana kidogo. Tume ya Warioba haikutakiwa kfanya kazi in a dodoki style. Baada ya hapo tunao wajibu wa kufanya marekebisho tukakayoona yanafaa kwa ujumla wetu sote. Tuacheni malalamiko yasiyo na mwisho, tutoe ushauri. Napendekeza tusikosoe kwa ujumla, tujaribu kuwa tunacite kipengele chenye upungufu kila tunapokosoa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…