Pia sheria ya ndoa inaruhusu mke au mume kumiliki mali zake binafsi. Ina Maana kwamba ndoa haiondoi umilikaji wa mali binafsi kwa mwanandoa, kama mke au mume alikuwa na mali fulani kabla ya ndoa mali hiyo inabaki kuwa yake peke yake hata baada ya ndoa. Mali zinazopatikana kwa nguvu ya wanandoa wote wawili hizo huwa ni mali za pamoja na zinamilikiwa na wanandoa wote wawili.