Je, unakumbuka nini enzi zako za JKT? Ni mambo gani yalikufurahisha au kukukwaza?

'Hiyolela hiyolela hiyolea aah, Hiyolela hiyolela hiyolea na bolingo. Magagula na Lusonga sitaenda tena, maafande wa Mlale watanisurubu.'
Mhh jamani JKT kulikuwa na raha zake, Mlale hiyo Songea wimbo mmojawapo wa mchaka mckaka. Nakumbuka wimbo mwingine.
'Nalia yombwe nalia yombwe nalia yombwe nalia yombwe. Mama mbali Mlale mbali tukumbukane kwa barua na Baba mbali Mlale Mbali tukumbukane kwa barua.'
Utasikia afande Kuruta maliza hiyooo yaani muache kuimba nyimbo za masikitiko.
Ila umoja, ushirikiano, uvumilivu, usafi, ukakamavu, uzalendo nk. ni mambo muhimu niliyojifunza.
 
Mlale JKT- ruvuma jamani mko wapi? Kwa wenyeji kule chakula kebekebe tena ugali mkubwa wa makuruta shurti kusongwa na wanaume. Halafu ugali bure mnanunua tu mboga- maarufu kule kiti moto. Embakasi shamba la mahindi. Unapewa palilia mistari 3 ambayo unaona mwanzo tu mwisho wake huuoni.
Maafande: Nguvu ya Nyani ( a.k.a yake), Rweikiza, madame Grace ( Matron), Afande Sabuni, Mwaipopo, Mande??, Chuma n.k!
 
Nilikuwa operation miaka 30 ya uhuru Makutupora. Kuna magumu mengi na pia kuna mafunzo mengi. Nikikutana na nilokuwa nao shule na chuo huwa nafurahi but nikikutana na nilokuwa nsye jeshini huwa nafurahia zaidi maaba ni jambo la onky 1yr lkn lenye kumbux2 nyingi.
 
lol!!.................green vest af nyekundu

ila ukweli ukakamavu tulijifunza sana ivi wa siku hizi bado zile staili za zaman zipo?
ivi yale amteso tuliyopata bado wa siku hizi wanayapata?

Duh na wewe ulikwenda majeshi?
 
Siku hizi hakuna mateso kivile, hakuna kubeba dunia wala kupigwa nuwa, watoto wanakufa kufa so wameamua kulegeza kuendana na wakati.
 
Wengi wa watoto wetu siku hizi ni wagonjwa, mara moyo mara Nina mshono basi kamanda lazima uone huruma........... Mungu ilinde Jeshi letu
 
Mafinga jkt e coy kwa afande mangwembe we acha tu ,kwenye mziki tukiwa na lali wawa ,mbio ndefu tukiwa na nyoka,hiyo ilikuwa operation usafi kabla ya vita,na afande makona usisahau mp ngere, ee bwana acha tu ,mahindi ya kuchoma na uchinjaji wa kiti moto.mkuu wa kambi msilu, sharp shooter afande mwandemane.nyimbo kalebuse
 
Aise mimi nilikuwa kule Makutupora operesheni ni siri yangu. Yaani kuna jamaa wakati afande anauliza majina yetu akasema yeye anaitwa MBORO SULULU. Basi ilikuwa ni mshke mshike maafande wakadhani anawatania na kuwatukana . Jamaa aliteswa kisawasawa. Sasa huyo sijui yuko wapi huenda akawa ni profesa somewhere. I salute you MBORO SULULU wherever you are and if you are still alive.
 

Hao kuruta wa Oljoro walikuwa operation ipi? Mimi nilikuwa Okoa please update me
 

Nilikuwa oljoro nikapigwa bogi la mgambo!
 
Nilikiwa Oljoro nikapigwa bogi la
Mgambo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…