Je, unakumbuka nini enzi zako za JKT? Ni mambo gani yalikufurahisha au kukukwaza?

Mwenye full story ya kupotea kwa malela jmn kisa kitamu hichii

Story ya malela haina kisa kirefu.ni kwamba,

Alipotea akiwa na wenzake katika mchaka mchaka usiku miaka ya 80s,akatafutwa sana kama ujuavyo jeshi linavyosaka kilichopotea,lakini hola(hakupatikana),badala yake akawa anatokea kama mzimu katika kambi mbali mbali.

Ila hii ishu inasemekana iliwekwa ili kuwafanya kuruta wasipende kujitenga tenga,kwani kuna mzimu(malela),ulipotea katika mazingira ya kutatanisha,unachukua kuruta na kupotea nao.
 
Mwenye full story ya kupotea kwa malela jmn kisa kitamu hichii
Malela alikuwa ni dawiri aliomba kwenda kukojoa wakati wa mkesha,akaenda ila hakurudi akatafutwa kila mahali,mpaka serengeti, angani hakuonekana,wakapiga simu mpaka nyumbani kwao labda katoroka ili wajue lakini hakuwepo nyumbani kwao,wakafuatilia mpaka nyayo za miguu lakini ziliishia pale tu alipokwenda,hivyo ilikuwa ni kama vile alinyakuliwa ndio maana mpaka leo kambi zote tunaimba malela yukwapi tunamtafuta!
 
Yep mkuu ilikuwa mwaka gani
 
Bonge la story!
 
Ukiishi kwa upanga utakufa kwa upanga!
 
Huu uzi umekuja sasa hivi??? Bulombora mpo??? Operation Ujenzi, Combania C: Afande Makani Jamani hao watu!!! Yule Sargent aliyekuwa anabeba pistor nimemsahau jina aliua nyoka wakati serule wanaimba mimi nanga!!! Eee bwana we Majeshiiiii ilikuwa raha. Mnakutana kwenye Makuruma hall mnawasema ma Afande kwa CO, subiri mtoke mnaipata kuliko jana!!!! Makuruma ilijengwa kila intake ni makuti usifikiri ni jengo. Hata mahanga yalikuwa hayana madirisha tulikuwa tunaruka tu.
 
Nilichojifunza ni kuwa jeshini hakuna utaratibu wa kuishi...na huo ndio utaratibu!
 
Na mimi ambaye sikupita JKT na comment wapi jamani?
 
Nimecheka sana!
 
Mi nilikuwa mafinga A coy 87/88 nakumbuka pamoja na mambo mengine kuna mwenzetu mmoja ali act uselule (ugonjwa) mpakabhadi sisi wenyewe tuliamini, akawa mlinzi wa kudumu wa hanger kipindi chote cha ukuruta. Baada ya kumaliza mafunzo tulishangaa ni mzima wa afya na hivi sasa ni mkuu wa wilaya moja kwenye serikali hii ya Magufuli[emoji3][emoji3]
 
Nakumbuka nilimpiga ST sababu alinambia nideki choo nikaona hizi dharau nilimtandika mpaka military police wakaja daah nilipewa kichapo alafu nikawekwa mahabusu wiki mbili sitasahau mateso yale
 
Kitu kikubwa nilichojifunza JKT ni "Endurance".Hii imenisadia sana kuwa na uvumilivu wa hali ya juu hasa katika kipindi hiki ambacho "hostility" imetamalaki nchi nzima.

Enzi hizo Oljoro JKT ilikuwa 16 KJ, CO akiwa Colonel Adamu Mwakanjuki. Alikuwa muungwana sana kuliko watani zangu wengi wa kinyakyusa ninaowafahamu. Inawazekana ni kwa kuwa alikuwa mnyakyusa wa Unguja. Mwenyezi Mungu aiweke roho yake mahali pema peponi.
 
Vibwende+ babu kombania D . nikiwa nanakima rc mongela, DC Richard kasesela Na akina Lt Colnel kalambi, hao walikuwa mabingwa wa ubangaizaji Ruvu!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…