godson Lomayani
JF-Expert Member
- Dec 31, 2018
- 538
- 711
Miaka ya zamani msimu wa nyahenge kozi ya awali JW Ilikuwa inafanyika hapoDaaah!! Kumbe umepigia apo mjini kabisa Ruvu!!. Balaa lipo 841kj uko mjini Mafinga.
Sent using Jamii Forums mobile app
Du kuchunga mbuzi bora kulima. Ni wasumbufu hakuna mfano.Kina mkwara wakati kijitu chenyewe kidogo! Kilitukamata mnadani, tukakinunulia nyama, wakati kinakula tukakitoroka. Kufika kambini ati kinasema tumetoroka mara mbili..kikosi na mnadani..tena tulikitoroka mnadani bila kulipia nyama kilizokula.
Nakumbuka nilikuwa mpishi mkuu, nikapiga stop ya maafande kuchukua pororo...looh walinitimua jikoni nikapelekwa kwa mbuzii. Ukienda kuchunga mimbuzi hata nane inaweza zaa machungani basi taabu kuvibeba kurudi zizini.
Ebhana!! Mkuu sahivi ruvu ikovizuri sana nami pia course yangu ya JKT nilipigia pale, chini ya kamanda niliyekua nikimkubali Sir Charles Mbuge: dah huy mister ni kati ya watu nnao wakubali saaana than normal katika jeshi la nchiyetu, huyu mkuu ni very systematic sana majuzi kapewa tengo kali sana na mkuu wa majeshi, dah hakika anastaili sana bna,Wazalendo;
Moja ya shemu ya maisha yangu ambayo kamwe sitasahu ni kupitia JKT.
Nilijiunga na JKT Ruvu na baadaye nikaenda Service Buhemba Lwamkoma.
Sitosahau kamwe mafunzo ya ukakamavu, kwata, mchaka mchaka, disko na vitimbi mbalimbali kati ya Makuruta na Maafande. Nilikuwa Combania E.
Moja ya vituko vya kukumbuka ni simulizi kutoka- Operation OKOA, kulikuwa na huyu jamaa alikuwa ni mweusi sana anaitwa afande Lucas, badala ya kuwaaamsha kuruta kwa filimbi, alikuwa anaingia na kuvuta Sigara. Kuruta inatakiwa ukisikia harufu ya Sigara uamke na kufoleni nje. Usipotoka in time unakula mijeledi.
Basi siku moja Kuruta wakapanga wamfanyizie na wakatoka mapema nje na kujificha huku ndani kwenye Bweni wakiyaviringisha mablanketi mithili ya mtu amelala. Afande alipomaliza sigara hakuna aliyetoka akajua siku hiyo kuruta wamegoma kuamka na kuanza kuchapa viboko yale mablanketi yaliyovingirishwa. Alishtukia kaanza kushambuliwa yeye na kuruta toka nje ambao walikuwa na fimbo kibao mpaka akakoma. Kisha kuruta wakafoleni nje. Nakumbuka Mkuu wa Kombania alipata habari na kulikuwa na drill si kawaida na mpaka push ups za kunusa mkojo katika nyasi walizokuwa wanakojoa kuruta usiku. Hata hivyo yule afande naye alikoma kwani hakurudia mchezo wa kuwaamsha watu kwa sigara.
Kwa waliokuwa Ruvu Operation Okoa:
Na miss - Ugali na korosho mnapojongo kambini
Namiss Mihogo ya Vibwende kwa Babu
Wali na Maembe
Uji wa Mestin ya Jeshi
Bukta na Green Vest
Kuokota kuni
Bustani
Michezo
Disco . . . Ama Johnnnnn ambaaaa ambaaa John, amba Johnnn wa Tanzania . .
. . . . Arusha Mbali, Arusha Mbali, tukumbukane kwa Barua nk.
Nakumbuka pia siku moja sikuimbisha disco vizuri na kipindi kile 1985 bado kulikuwa kuna ubaguzi wa rangi Africa Kusini, basi afande akanipiga mkwala na kuniambia . . . .
"Kuruta nitakutemea mate yenye sumu usoni upofuke macho, na sijui utatibiwa wapi kwani mipaka yote Afrika Kusini imefungwa . . . (Kana kwamba hakukuwa na hospitali ya kutibu mate ya sumu hapa bongo"
Jamani mliokosa JKT, mlikosa mengi, japo tulipata tabu lakini tulijifunza mengi katika maisha.
Je, wewe unakumbuka nini?
[emoji24][emoji24][emoji24]pole sana mkuu, hakika kila binadam ni muhim hapa dunia, maafande wangu wa Roadgan, kuku coy, main get mamaangu mpendwa kamanda Mamuya mkuje huku, wananchi wazalendo tuko pamoja, I miss them very much..Namtafuta afande wangu maìsha yangu yote nimekuwa mzee nimestàfu nina hakika kwa umri ule atakuwa amestaafu.
Alikuwa ni staff Sajenti by then 1986 Ruvu JKT aliokoa maìsha yangu malaria ilipanda kichwani akalazimisha gari main gate nipelekwe Tumbi Kibaha wakati huo kulikuwa na outbreak ya ķipindupindu na homa ya uti wa mgongo(meningitis ) kwa weledi wake akalazimisha gari itoke kama sìo leo ningekuwa RIP namtafuta huyu mutu alikuwa anaitwa staff Sgt Shelukindo
Maparachichi ya AA, mapapai ya AB, karanga za Mgombe hahahahaa miaka minne toka nitoke kule.Wale wa Mtabila 825Kj, Op Merelani..
Nilivundika Papai na Parachichi nakusahau location aiseee Roho iliuma.
Namisi Chenja na Morali ya Jeshi
Amba John
HAPPY SAMBE
Sixweek na Intro
Adhabu za kutundika nk
Pale Mtabila tulikua tuna Doji Vya Hatari.
Maafande wanaa kama Field Marshall na Sura ya yesu
Sent using Jamii Forums mobile app
Namtafuta afande wangu maìsha yangu yote nimekuwa mzee nimestàfu nina hakika kwa umri ule atakuwa amestaafu.
Alikuwa ni staff Sajenti by then 1986 Ruvu JKT aliokoa maìsha yangu malaria ilipanda kichwani akalazimisha gari main gate nipelekwe Tumbi Kibaha wakati huo kulikuwa na outbreak ya ķipindupindu na homa ya uti wa mgongo(meningitis ) kwa weledi wake akalazimisha gari itoke kama sìo leo ningekuwa RIP namtafuta huyu mutu alikuwa anaitwa staff Sgt Shelukindo
Hahahahh mkuu umenikumbusha yale maeneo.....nimetoka kule 2014 ndy intake ya kwanza pale!!Wale wa Mtabila 825Kj, Op Merelani..
Nilivundika Papai na Parachichi nakusahau location aiseee Roho iliuma.
Namisi Chenja na Morali ya Jeshi
Amba John
HAPPY SAMBE
Sixweek na Intro
Adhabu za kutundika nk
Pale Mtabila tulikua tuna Doji Vya Hatari.
Maafande wanaa kama Field Marshall na Sura ya yesu
Sent using Jamii Forums mobile app
Ahaha! Am so happy.....kumbe we nae ni wa 2014 kule mtabila?Maparachichi ya AA, mapapai ya AB, karanga za Mgombe hahahahaa miaka minne toka nitoke kule.
Unafahamu jina la mkufunzi yeyote pale 838?ss wa mwaka jana maramba JKT mpo mujb wa sheria