Je, unakumbuka nini enzi zako za JKT? Ni mambo gani yalikufurahisha au kukukwaza?

Mimi operation Kambarage 1990/1991. Oljoro/Makuyuni. Naomba niandikie mistari yote ya wimbo wa kulekule kwa chinoma/chinova! nimeusahau. Namkumbuka sana Afande Kunesa/Salum wa jikoni. Ukimwambia chakula kidogo anakujibu, mwaga kanywe maji kalale.

Mimi wa 832 KJ Ruvu Operesheni Kambarage 1990/91 .
“Kule kule ,Kule Kule kuchinovaa.
Baba nae mama wa kuzanga na kuzimbabweee
 
Mkuu, tulikua Intake moja hapo Oljoro JKT. CO akiwa afande Mirudi. Mimi nilikua combania "G" kwa "Sergeant wa jeshi" Mwambuluma. Bila kumsahau CI Captain Mlimba.
 
Sabufa nahisi kahama m nilikua hapo 2014 msenge bufa anamabiti hatari kinouma nouma
Labda awe kahama miaka ya karibuni ila 2015 sie na 2016 kuna mdau hapo juu kathibitisha alikuwepo.

Kuruuuuti .. singee nyama italala singee aiyomama [emoji23]
 
Nilikuwa 841 Mafinga miaka ya 2000 daa kuna siku zilipigwa ngumi kati ya kruta na afande nyota 2 anaitwa Mosi wakigombania demu na bahati mbaya yule afande alichezea ndonga za kutosha mpaka akaja kuamua koplo mmoja ambaye baada ya sakata akawasimulia baadhi ya maafande ambao walifikisha taarifa ingawa kwa utani kuwa officer kapigwa na kruta.
Baadae mkuu wa mafunzo wanamwita Chief instructor au kifupi CI akazisikia kwa kuwa ilikuwa imepigwa marufuku ma-officer na kruta kwenda married kotazi afande akaitisha foleni mapema uwanja wa damu tulipomuona tu mnyama CI tukajua kazi tunayo maana alikuwa katili kuliko commandat kanali Mtonga ambae alikuwa ndio mkuu wa chuo.

Kilichofuata CI akasema kruta mnatupiga maofisa kwa jana zile ngumi zilizopigwa hazikuwa rasmi na ushindi mliopata makruti ni batili kwa hiyo leo mbele yenu pambano linarudiwa ili muone kuwa kruti hajawahi kumshinda ofisa.

Basi aliitwa mzee mmoja alikuwa mtu wa physical fitness akaambiwa achore mstari halafu awe refa wa pambano kati ya yule kruti aliyeshinda pambano jana na yy CI duuu basi baada ya kipyenga yule kruti alisukumiziwa makonde ya kutosha mpaka damu zikamtoka mdomoni.

Baada ya kuona kruti amesalenda KANYATA ambaye ni bridgedia general kwa sasa huku akijiridhisha kwamba ameshinda alituamuru tumpigie makofi kwa ushindi na kesi ikawa imekwisha huku ushindi ukienda kwa maofisa na makruti rukiambulia patupu.

Kwa hiyo kwa maamuzi hayo kesi ikawa imekwsha bila kuamuliwa hivyo yule kruti angefukuzwa kozi.

Jeshini bwana moja jumlisha moja usitegemee kuwa ni mbili.

Nasikia kanali MTONGA alifariki ila meja KANYATA ni bridgedia general kwa sasa.
 
Kambi yangu iliyoondoa mafuta baada ya form 6.
Kuivisha ndizi kwa kufukia na kukoa moto juu yake....

Nguvu ya nyani mnyakyusa yule...

Yote raha
Kwa wale tuliokuwa nao Mlale JKT, Operation Azimio la Arusha, 1987/1988. nadhani mnawakumbuka afande Pilato, Nguvu ya Nyani, Mtono(RIP) na vijiwe kama Lusonga, Magagula, Mlandizi, Chipole
 
Mtanzania,
Dah mduda unampata marehemu now yeye na mkewe.anasema simama namguu mmoja akikuona unasinzia kwenye somo lake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…