mumewanguu
JF-Expert Member
- Mar 2, 2018
- 261
- 259
Haya mkuu hongera. Kuna mabadiliko yoyote? Shida ya maji bado iko? Mnaenda “stesheni” kugombea maji na wafungwa? Mlima wa kwa koko ushaenda? Kuchanja kuni porini?[emoji3]
Nakumbuka mwaka 1972 tulitoka Bulombora jkt Hadi Nguruka Kijiji Cha Mtego kujenga Zahanati kufika huku tukaanza ujenzi Kama kawaida ya majkt wakaanza kuwahonga mabinti wa Kijiji mchele Hadi wake za watu Bwana weee, habari zikavuma kuwa Kati yetu Kuna wakware kumbe wanakijiji wakakaa vikao vya Siri na kuazimia kuwa hawatutaki tuondoka na Kama ni Zahanati hawaitaki kwa hiyo tuondoke.
kijiji wakaenda porini na kukata mafimbo na marungu tayari kutuadhibu maana tumeacha kilicho tupeleka .Mimi nilikuwa na dogodogo moja matata sana.sasa siku akafika ya kutupiga nadhani ilikuwa jumapili,jirani kambi kulikuwa kilabu Cha pombe ya kienyeji miminilikuwa hapo ,saa 10 jioni Mungu wangu nilishangaa karibu nusu ya Kijiji wanna marungu na wanapiga kila JKT huku wanauliza kwa Nini mnatongoza wake zetu.ile nataka kutimua mbio wapi nikadakwa e bwana e kill si kipigo usiombe.
Jamaa yangu anaitwa Kalikubwa nikamuona yupo chini anakoroma nikaanza kushushiwa kipigo,nikabebwa na kutumbukizwa katika pipa la pombe Sasa Mimi naomba msaada wapi,kumbe kwa kunitumbukiza katika pipa la pombe kukanisaidia wengine wakidai ule ni uharibifu wa pombe kwa hiyo wakanichomoa humo ,wakati wanarumbana Mimi nikatoka nduki,huyo huyo huyohuyo nikatokomea msituni
Cha ajabu huko porini nikamkuta mwenzangu Mr Mika,mwenzangu angalau alikuwa vizuri tukaondoka Hadi Nguruka station nikamuomba mwenzangu anpe nguo akanipa.usiku tukapanda treni Hadi Tabora,mwaka 1982 niliamua kwenda Tena Hadi Nguruka na kwenda Kijiji Cha Mtego wakati huo nimesha jiunga na jeshi la polisi,kweli Jkt sintosahau.
Sent using Jamii Forums mobile app
Nakumbuka mwaka 1972 tulitoka Bulombora jkt Hadi Nguruka Kijiji Cha Mtego kujenga Zahanati kufika huku tukaanza ujenzi Kama kawaida ya majkt wakaanza kuwahonga mabinti wa Kijiji mchele Hadi wake za watu Bwana weee, habari zikavuma kuwa Kati yetu Kuna wakware kumbe wanakijiji wakakaa vikao vya Siri na kuazimia kuwa hawatutaki tuondoka na Kama ni Zahanati hawaitaki kwa hiyo tuondoke.
kijiji wakaenda porini na kukata mafimbo na marungu tayari kutuadhibu maana tumeacha kilicho tupeleka .Mimi nilikuwa na dogodogo moja matata sana.sasa siku akafika ya kutupiga nadhani ilikuwa jumapili,jirani kambi kulikuwa kilabu Cha pombe ya kienyeji miminilikuwa hapo ,saa 10 jioni Mungu wangu nilishangaa karibu nusu ya Kijiji wanna marungu na wanapiga kila JKT huku wanauliza kwa Nini mnatongoza wake zetu.ile nataka kutimua mbio wapi nikadakwa e bwana e kill si kipigo usiombe.
Jamaa yangu anaitwa Kalikubwa nikamuona yupo chini anakoroma nikaanza kushushiwa kipigo,nikabebwa na kutumbukizwa katika pipa la pombe Sasa Mimi naomba msaada wapi,kumbe kwa kunitumbukiza katika pipa la pombe kukanisaidia wengine wakidai ule ni uharibifu wa pombe kwa hiyo wakanichomoa humo ,wakati wanarumbana Mimi nikatoka nduki,huyo huyo huyohuyo nikatokomea msituni
Cha ajabu huko porini nikamkuta mwenzangu Mr Mika,mwenzangu angalau alikuwa vizuri tukaondoka Hadi Nguruka station nikamuomba mwenzangu anpe nguo akanipa.usiku tukapanda treni Hadi Tabora,mwaka 1982 niliamua kwenda Tena Hadi Nguruka na kwenda Kijiji Cha Mtego wakati huo nimesha jiunga na jeshi la polisi,kweli Jkt sintosahau.
Sent using Jamii Forums mobile app
JKT KANEMBWA,sintosahau shughuli ya kuandaa mashamba,
1.mnaingia kwenye chaka kubwa mnatengeneza fire break kwa fyekeo na jembe
2. mnawasha moto kwenye nyasi zilizo kauka na kuuzunguka usivuke fire break kwa ajili ya upepo
3.Mnadondosha miti yote kwa mashoka, mnachimba kuitafuta mizizi ya miti mnaikata mpaka miti idondoke.
Mwisho sitokuja kusahau somo la uchap, Moto unawashwa porini mnaamshwa saa nane usiku mnaenda kuuzima mpaka hasubuhi hamjamaliza.
Nyimbo za kupeana hamasa pia zilikua sehemu kubwa ya faraja wakati huo.
Mkuu bado uko zenji?Wale wa Mlale jkt wapo wapi 842KJ OP KIKWETE 2015
wapi RSM William
Wapi sir meja mwarabu
Wapi afande Nyingo
Wapi afande pilato
Wapi afande wa kikosi Lyimo mchaga aliyekosa mwili hahaaaa
A-COY YA DEMO ndio mana molari
Sent using Jamii Forums mobile app
napafahamu mkuu...chanzo kikuu cha maji kuleMkuu unakufahamu AMAZON,long live kanembwa
Nimeishi jirani na afande machibya ame staafu akiwa Lt Col alikuwa mtu poa yeye hata mkewe pia sikujua Kama alikuwa RuvuMimi nilikuwa OperesheniTIMIZA nikiwa na maafande wachache ninaowafahamu pale Ruvu, Marehemu Makame Mkuu wa Kambi, Urio nakumbuka alikuwa Luteni, Londo, Agnes, Afande machibya aliyewahi kuwa Mkuu wa Mikoa kadhaa etc. Nakumbuka sana kuchoma nyama porini hasa tukiwa zamu ya kupika, pili kula mayai mabichi hasa ukipangwa kwenda kufanya kazi kwenye mabanda, tatu siku Bendi ya muziki inapotumbuiza siku hiyo kwenye kambi la Ruvu. Mwisho hakuna ya Mwanamke au Mwanaume wote siku ya kwanza mnatupiwa bukta/pitishot ya kuvaa na ndiyo sare ya kila siku. Kweli ilipendeza na pale mara chache kuugua sababu ya mikiki mikiki ya pale.