Je, unakumbuka nini enzi zako za JKT? Ni mambo gani yalikufurahisha au kukukwaza?

We acha basi moshi kafariki?aliumwa ama ilikuwaje mshikaji wangu sana yule nilhama kambi tukapotezana
Inasemekana issue za kurogana Sina uhakika sana, kuna dogo wa chuga anasoma pale mwaka Jana tuko geto akawa anatoa hizo story
 
Inasemekana issue za kurogana Sina uhakika sana, kuna dogo wa chuga anasoma pale mwaka Jana tuko geto akawa anatoa hizo story
Duh,kule uchawi sana ukizubaa mwenzio anakuwahi,yaani ni wanataka vyeo balaa nasikia kuna huyo mtu mfupi kakalia TYC mwaka wa kumi huu,akija anayemzidi lazima baada ya wiki ama siku atasepa,yeye ni kapteni miaka hapandi na hashuka,unaambiwa ni moto wa kuotea mbali
 
Wa Bulombora tupeane hi hapa.
 
Safi sana mkuu umechangia vema hoja hii,kipindi nchi ina heshima na adabu!hapo ninaongezea unalipwa kichele cha 100tshs kila mwezi,mmmm 835 kJ ya LT.COL.MTONO then 837KJ pale Chita jkt nilitoka jeshi nimeiva na ngangari.
 
Eeeh ndohapo lazima uwe imara na wewe.

Hivi Liutenant Msangi Yuko wapi now
 
cha maji [emoji38][emoji38]
 
Nimepita hapo hanga lenye jina la mondlane ndio nimelala sana miaka mitatu ilionipa ujeuri na dharau mpka leo kazini, viva bulombora
 
Chenja moja hivi
wote :“ singenya maitalala siiiiiiingenya. aiyo mama singenya maitatalalaaaaa

afande: watu wote kunjeni ngumi ( mnasimika) kama hamjasimika utaskia

afande:unajua staki utani,,,,,

hiiii ngoma ya doso ina maovyo ovyo sana [emoji1787]….
 
843 KJ, Nachingwea a.k.a Nachi ngumu. Ni moja ya vikosi vya ki-battle sana. Palizi ya mahindi shamba dunia la Muhuga sitaisahau
 
Alafu chenja inaendelea"asiyependa jeshi letu atoroke,atoroke sa nane za usiku
 
Mkuu hapo umechanganya na 'shumbwela mashushu', huo muendelezo upo huko
Mkuu hata shumbwela na hyo singe nyama haitalala iko na melod mbili ile ya polepole ndo wanaongezea asopenda jeshi atoroke
 
Daah 821 kuna sir meja (yule anaevaa saa na kifimbo mkononi) aisee jamaa alikua anabiti sana hadi kwa masir meja wa combania…yaani kama kombania yenu haijaleta kuni hamli hadi mueke kuni na pia huchukui chakula bila kufoleni na kwenda na kwata !
 
Nilipitia Ruvu Op Tanzania ya Viwanda 2017. Nilikuwa nachukia kwata asee ndo sababu ikanifanya niachane nayo nikawa KO selule, kingine nisichopenda na wengi naona hawaongelei ni tochi daaahh hii kitu isikie tu.
Mabio nilikuwa nayapenda sana so sikuwa napata shida kwenye hilo. Tukio linaloniuma mpaka leo nilitukanwa tusi moja bila sababu siwezi lisahau mpaka nakufa.
Mpango kazi niliokuwa nauchukia ni kule shamba la vitunguu aka Guantanamo, yaani mtu akipangiwa kule anatafuta kila namna apotee, kuna kombania wakichaguliwa 50 wanafika watano au hawafiki kabisa. Mpango kazi mtamu ulikuwa JKT club kule oya oya kinoma kama umezoeana na maservice men unapewa hata simu utachat utaongea Tani yako. Kiufupi ni hayo tuu
 


Hebu vuta kumbukumbu mimi nakumbuka nilipokuwa JKT mnajongo na birika kwenye mashamba ya mahindi hii ndio ilikuwa LUNCH
 
Zambeee mamaaa... Kilimaaa mbeee kilimaaa kilimaaa mbeeee kilimaaa mbeee...[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3] Hakuna Nyimbo tamu kama Chenja dunianiii...
Mimi nilikuwa radio kwenye chenja, ulikuwa ukifika muda wa mchakamchaka watu wote wanahamia kwenye bogi langu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…