Je, unakumbuka nini enzi zako za JKT? Ni mambo gani yalikufurahisha au kukukwaza?

Je, unakumbuka nini enzi zako za JKT? Ni mambo gani yalikufurahisha au kukukwaza?

841 kj - Operation Oljoro,
.Mkuu wa kikos Calonel Mlay,
.Charlie Coy
.OC Shayo
.Idetero tulipalilia miraba ya kutosha.
.lindo kipindi cha nyahenge asikuambie mtu,una freez
.kurudi na furushi la kuni ukitoka kwenye mraba na jembe juu,
.adhabu detach ya lungemba

Siwezi sahau kabisa zile pilika maishani.
 
Nawatafuta ndugu zangu wa op miaka 50,832kj danger coy intake ya tatu mujibu(2013) platoon number moja,section number moja
 
Jamaa mmoja alikuwa mwoga sana, anaogopa sana adhabu. Kama kawaida ya jeshi. ilikuwa ni lazima utandike kitanda vizuri kwa style ya jeshi, kila kitu, shuka, blanketi, kitanda mess tin, kwa dressing. Haya yote unatakiwa ufanye kabla hujapurukushwa kwa wito wa 'FOLEN'! Basi huyu jamaa alikuwa anatandika kitanda chake vizuri usiku tukitoka disco, halafu alikuwa analala chini! Tulikuwa tunamcheka sana, lakini baadae tukawa tunamuonea huruma.

Njemba moja alikuwa akizurura kutwa na sururu. Akiulizwa, askari unakwenda wapi, anasema ametumwa kazi na afande fulani. Tulikuwa tunamuonea huruma maana alikuwa anazurura kutwa na sururu baada ya kulala porini kama sie wengine wajongomeaji.

Tulijifunza kutomaliza kazi mapema, maana ukiripoti umemaliza kazi uliyopewa, unabambikiziwa nyingine. Tulikuwa na midomo yenye fridge, maana kama jamaa yako alikuwa zamu jikoni, akikuchotea nyama au wali kwenye mess tin, unatakiwa umeze haraka, hata kama ni vya moto kiasi gani. Ulitakiwa uwe mwizi sana, hasa wa kofia, maana kama umeibiwa kofia na hukuvaa, unapewa adhabu. Mimi nilizoea kuwaibia maafande kofia zao, maana ilikuwa ni rahisi kwao kupata nyingine.

Katika kombania yetu tulikuwa na wahindi wawili. Siku moja kwenye disco, baada ya wiki kadhaa za kukaa jeshini, mhindi mmoja akawa anatufundisha wimbo wa kihindi. Tulijifunza, lakini yule mwingine akawa anacheka sana,. Sisi tukadhani kuwa maneno ya wimbo ule yanachekesha. Kesho yake ilibainika kuwa yule Mhindi aliyetufundisha ule wimbo ametoroka. Yule mhindi aliyebaki akatuambia alikuwa anacheka sana maana maneno ya wimbo ni: Kwaherini, mimi kesho natoroka!

Siku moja kombania yetu ilikuwa zamu. Platoon yetu ikapelekwa kwa kuku. Kama kawaida, ukishafika huko unakazana kubugia kwa wingi mayai mabichi kiasi utakachoweza. Baada ya kumaliza kazi, tukachukua mengine, tukajaza kwenye mifuko ya combat. Rafiki yetu mmoja akachukua mengine akayaweka kwenye jungle hat yake, halafu akaivaa.

Tukawa tunaondoka kutoka kwa kuku, tukiwa na dhamira ya kwenda kwenye jongomeo letu msituni. Mara tukakutana na ma MP. Kitu kilichotuponza siku hiyo ni kutokuvaa vizuri. Hatukufunga kamba boot, mashati hayakufungwa vifungo nk. MP mmoja akasema, 'Askari, simama. Mbona mmevaa kama askari wa kukodiwa?' Akamuita yule jamaa aliyevaa jungle hat yenye mayai. 'We, kuja hapa, mbona umening'iniza kofia?

Njoo hapa nikuonyeshe namna ya kuvaa'!! Akashika kofia, akaishusha kwa nguvu ili aizingushe zungushe kwa nguvu kichwani. Lo, si mayai yakavunjika! Yakaanza kumwagika usoni mwa jamaa. Basi tukazingirwa tusikimbie. Tukasachiwa likapatikana karai zima la mayai. Tukapigishwa fang fang usawa wa Quarter Guard, tayari kwa kufungwa na kuwa court marshalled.

Muda huo ulikuwa mchana na chakula cha ma MP kilikuwa kimeletwa. Basi ma MPwote, isipokuwa mmoja, wakaenda kula. Ikatokea kuwa kitabu cha kuandikisha mahabusu kimejaa, MP akaenda kuchukua kingine. Wakati huo tupo kwenye baraza la Quarter Guard, bado hatujawekwa ndani. Kuona upenyo huo, tukaamua tutoroke. Mmoja wetu akakumbuka kuwa tumesahau karai letu la mayai, akalirudia, tukatokomea nalo msituni. Mchana ule tulikula vizuri sana mayai ya kuchemsha .

Wakati wa usiku kwenye disco, tukaona kundi la ma Mp linakuja usawa wa kombania. Tukajua, leeo tumepatikana. Wakaongea na kamanda wa kombania, halafu muda si mfupi wakaondoka. Baada ya wao kuondoka,kamanda akasoma majina yetu na kutuita tutoke mbele. Akautuuliza, nyie mlikuwa kwa kuku leo? Tukamuambia ndio. Akasema safi sana, nyie askari wazuri sana, mmekamatwa, lakini mkaweza kutoroka, pamoja na mayai yenu. Huo ndio uaskari. Hatukupewa adhabu, disco likaendelea!
Nimecheka mpaka kilio
 
Habari wanaungwana,

Moja kwa moja niende kwenye maada. Kama wewe ni miongoni mwa watu umepitia JKT lazima kuna kituko umefanya au ulishuhudia ukikikumbuka kinakufanya ufurahi mpaka leo.

Mimi huwa nakumbuka tulikuwa na jamaa yangu anaitwa Charles wakati wa msosi tulikuwa tunaenda kukaa meza yenye wasichana wengi sababu walikuwa hawamalizi msosi halaf wakiondoka tunausogeza tunamalizia😂😂!

Hii tabia nlioona tena chuoni rafiki alimnunulia demu chakula akala kidogo tu akaachia, alilalamika sana akaamua kuumalizia mwenyewe mbele yake. Salute kwa mwanangu nimuhifadhi jina.
 
841 kj - Operation Oljoro,
.Mkuu wa kikos Calonel Mlay,
.Charlie Coy
.OC Shayo
.Idetero tulipalilia miraba ya kutosha.
.lindo kipindi cha nyahenge asikuambie mtu,una freez
.kurudi na furushi la kuni ukitoka kwenye mraba na jembe juu,
.adhabu detach ya lungemba

Siwezi sahau kabisa zile pilika maishani.
Kulikuwa na Operesheni Oljoro? Ilikuwaje hapo Mafinga? Mwaka gani?
 
Nimecheka mpaka kilio
siku moja mkuu wa kikosi lt col Meena wa Ruvu 832kj mwaka 1986 alikamata makuruta walikuwa wanatoroka.Akawapakia kwenye gari lake nyuma magari wakati huo yaliitwa Dube.Akawa anawaendesha kuwapeleka kikosini wakapewe adhabu cha ajabu alivofika kati ya waliokamatwa wa5 wanne hawakuwepo waliruka kwenye gari wakakimbia akabakia mmoja tu.
Akasema hawa ndio askari hata vitani wakikamatwa ni raisi kumkimbia adui.
Yule aliyebaki akaambiwa sasa wewe utabeba adhabu za wenzako wote maana ni askari rahisi sana kukamatwa na adui kisha ukaenda kutoa siri wewe ni askari legelege.
 
Heshima yako mkuu[emoji23][emoji23][emoji23]
Unatisha, op gani hiyo? Kifupi ambae hakupita jkt(ya enzi zile) hawezi jua utamu wake. Ni sehemu ambayo akili ilitumika sana kufanikisha kila jambo.
 
Back
Top Bottom