Ben Zen Tarot
JF-Expert Member
- Dec 13, 2014
- 4,298
- 7,612
Uliwahi kusikia kuhusiana na ngekewa? Basi leo nataka nikufumbue ufahamu vizuri. Ngekewa ni mnyama aishie porini moja ya tabia zake kuu ni kupendwa na wanyama wenzie. Anapokaa ngekewa hukaa na kila aina ya wanyama na ndege na hawamdhuru. Kwa maana hiyo ngekewa ni mnyama ambaye anapendwa na kila mnyama alie mbugani.
Hali hii inasababisha vitu vyake kutumika kutengenezea dawa za mivuto na waganga. Mnyama huyu hupatikana kwa msimu na kumuona kwake ujue una bahati sana anaishi kwenye majani marefu kandokando mwa mito au maziwa makubwa.
Mara nyingi mnyama huyu anapotembea hufuatwa na wanyama wengine nyuma. Mkia wake hutumika kutengeneza dawa kwa watu wanaohitaji wafuasi mfano wasanii, wanasiasa wanaofanya kazi za kutembea na kuongea mbele za watu.
Kiufupi mnyama huyu hutengenezewa dawa nyingi za kuvuta wapenzi kuvuta mali nk Anapokanyaga mnyama huyu na wewe ukakanyaga kama kazi zako ni za kusafiri utapata safari mpaka utazichoka Ukichukua majani aliyelalia mnyama huyu ukayaanika ukamuwekea mtu sehemu anapolala au kwenye maji ya kuoga kitakachotokea huyo mtu atakuwa hana kauli kwako iwe bosi mpenzi nk.
Nimejitahidi kuelezea navyoelezeka
Hali hii inasababisha vitu vyake kutumika kutengenezea dawa za mivuto na waganga. Mnyama huyu hupatikana kwa msimu na kumuona kwake ujue una bahati sana anaishi kwenye majani marefu kandokando mwa mito au maziwa makubwa.
Mara nyingi mnyama huyu anapotembea hufuatwa na wanyama wengine nyuma. Mkia wake hutumika kutengeneza dawa kwa watu wanaohitaji wafuasi mfano wasanii, wanasiasa wanaofanya kazi za kutembea na kuongea mbele za watu.
Kiufupi mnyama huyu hutengenezewa dawa nyingi za kuvuta wapenzi kuvuta mali nk Anapokanyaga mnyama huyu na wewe ukakanyaga kama kazi zako ni za kusafiri utapata safari mpaka utazichoka Ukichukua majani aliyelalia mnyama huyu ukayaanika ukamuwekea mtu sehemu anapolala au kwenye maji ya kuoga kitakachotokea huyo mtu atakuwa hana kauli kwako iwe bosi mpenzi nk.
Nimejitahidi kuelezea navyoelezeka