Je, unataka kulima mazao ya mbogamboga na matunda lakini unakosa maarifa sahihi? Karibu tushauriane hapa

Tunaweza kupata mawasiliano tafadhali?#kilimomaarifa.utajiri
 
kilimomaarifa.tajiri sikupiga dawa ya kinga ya kantangaze miche ilipokuwa kwenye kitalu, sasa naweza kupiga dawa gani baada ya kupanda. Nimesoma option ulizotoa lakini nahisi zinanichanganya. Pia ni mbolea gani nzuri kwa migomba zaidi ya samadi? Asante
 
Last edited by a moderator:
je kuna ukweli kuwa ukikata maua au ukipunguza majani kwenye viazi mviringo vinavyokuwa eti unaongeza mavuno ,yaani kiazi kitakuwa na viazi vikubwa tofauti na ungeacha hivi bila kukata maua au kupunguza majani?
 
nilipandikiza nyanya na kuweka mashine iwe inamwagili , sasa kuna jirani kasema ukimwagilia nyanya kwa saa 24 au zaidi sehemu moja bila kuhamisha mashine unasababisha ziungue, mimi nilijua kuwa ndio zitaota vizuri,ulisema yara miller winner unaweza kupandia na kukuzia ,je mbolea ya dap nayo naweza kupandia viazi na nikakuzia? kwani nimeona mtu anakuzia dap kachanganya na can. Eti kuna parachichi zinazozaa mara mbili kwa mwaka? Asante sana.
 
Nimepandakiza miche 5000 ya nyanya aina ya eden ,je ikiota vizuri na kuhudumiwa vizuri naweza kupata kilo ngapi za nyanya mpaka mwisho wa mavuno.
 
NINA IMANI
WASTANI WA MAVUNO KWA EKA MOJA UNAPASWA USIKOSE KRETI (@40 KG) 400 NA KUENDELEA ILI UWEZE KURECOVER GHARAMA ZAKO, AMBAPO HATA BEI IKIFIKA TSH 10,000 KWA KRETI MOJA (BEI YA CHINI KABISAAA) BADO UTAPATA JUMLA YA MAVUNO YA TSH 4,00,000, NA GHARAMA ZAKO HATA ZIKIWA KUBWA VIPI HAZITAZIDI 3 MILIONI KWA EKA MOJA, HIVYO UTAPATA FAIDA YA TSH 1,000,000 KWA EKA . KILA LAKHERI
Nimepandakiza miche 5000 ya nyanya aina ya eden ,je ikiota vizuri na kuhudumiwa vizuri naweza kupata kilo ngapi za nyanya mpaka mwisho wa mavuno.
 
Asante sana, je dawa za ukungu na booster starter natakiwa kupiga kuanzia siku ya ngapi tangu kuipandikiza shambani
 

nashukuru sana
 
kilimomaarifa.tajiri hivi naweza kupiga dawa ya kinga ya kantangaze na kinga ya wadudu zote kwa wakati mmoja?
 
Last edited by a moderator:
Pia kwa ajili ya majani kusinyaa na kuwa njano kama picha ya jani uliyoweka nilipiga Grino 70WP na Dimethoate kwa ajili ya wadudu ni wiki sasa toka nipige lkn sioni badiliko lolote na nyanya nyingi zikiiva ndani zimeoza! Nirudie dawa au maoni yako ni yepi? Huu ugonjwa naona umesogea mpaka kny bustani ya spinach na chinese!
 
Dah nimepitia siku tatu huu UZI toka mwanzo mpaka mwisho hapa page ya 14 kwa umakini kabisa.

Aisee sijawahi kutana na UZI mtamu, wenye akili na unaokuelekeza direct hata kwa mkulima mdogo kabisa wa kule kijijini anaelewa.

Mkuu kilimomaarifautajiri salute kuu kwa mkono juu mwingine umenyooka chini. Nimechukua notes nyingi sana kwa ajili ya msaada.

Nikiwa na swali naliandika pembeni kwani nikiuliza itanipoteza ajabu nilivyozidi kusoma nikawa napata majibu na kujikuta nakata maswali.

Nililima nyanya riogrande mkulima tena kwa kuanza kwa mbwembwe sana pale kahe ekari 3. Shamba zilikuwa 2 moja ekari na robo nyingine mbili kasoro. Nililima kipindi cha January nikavuna March mwishoni.

Dah jamaa walikuwa wanakuja shamba kuchuma kreti moja la 40Kg lile niliuza kwa mara ya kwanza 45,000. Mwishoni niliuza 20,000.

Nilitumia milioni tano kasoro ikiwa ni jumla ya kila kitu, shamba, mashine mbili, mbegu, mbolea, Dawa, vitendea kazi na wafanyakazi.

Pamoja nakupata bei nzuri nilivuna kama kreti 60 tu mfano jumla zilinipa 2.1m pekee. Nyanya zilitafunwa na mdudu ambaye Sasa nimemjua ni kanitangaze kwani namtangaza Sasa.

Nimepitia kwa nguvu sana na kwa akili kwani narudi tena kahe msimu huu. Nafreka shamba Sasa na nataka kuandaa kitalu. Aisee nataka nilime kisasa zaidi. Huwa nanunua mbegu pale Moshi, nimepita maduka kadhaa nimeona wana kipato. Japo natafuta Eden.

Sasa swali langu tu hapa ni unanishauri pale kahe nipande ipi? Kipato inafanya vizuri au eden? Je Moshi duka gani linauza pembejeo za kilimo zilizo bora kama madawa, mbegu na kadhalika? Nakuuliza hivi kwani nimeona mahala umegusia kahe nikahisi unapaelewa vizuri.

Kwasasa napanda lile shamba la ekari mbili kasoro pekee baada ya kulipumzisha kwa Mwaka na miezi je kanitangaze bado atakuwa around?

Kuna sehemu umegusia kulima kwa kupandisha matuta kilimo kilicho bora kwa drip lines Sasa sikuelewa vizuri kwa umwagiliaji wa furrow niwekeje matuta? Nitamwagiliaje?

Kipindi kilichopita nilitumia majaluba kama ya mpunga ila sikupenda kwani hata shamba halipendezi.

Asante sana mkuu kwani kiukweli nililima nikiwa sina ujuzi. La mwisho mkuu tupatie namba tukupe walau kifurushi kwa roho nyeupe kabisa.

Umefanya kitu kikubwa hakina mfano wake.mtu anavyouliza unavyojibu Safi sana kaka, wala hujali kwamba ulishalijibu kabla.

Pamoja mkuu.
 

mkuu hivi nyanya kitaalamu inahitaji lita ngapi za maji kwa mche
 

mkuu nashukuru ,tatizo maji ni shida kwa hiyo nilitaka nijue kiasi cha maji mche mmoja unatumia kiasi gani ili ninue maji kwahiyo nikiwa na mche 2000 kila mmoja unatumia 500ml itakuwa ni : 2000x500=1000000ml sawa na lita 1000,lita 20 wanauza sh. 50 kwahiyo 50 x 59
= sh 2500 kwa siku x siku 100 =250000 si tupo pamoja mkuu ,Sasa kwa miche 2000 ntapata tani ngapi? je itanilipa?
 
chayowa


Kiongozi asante kwa kushukuru, Shukrani sana

Mkuu baraka ZIWE nyingi kwako na kwa kikazi chako hata milele. Kaswali kengine kameclic kichwani.

Nimepata elimu ya starter solution ambayo unachukua mbolea ya kupandia kiganja kimoja kikiwa kimenyooka na kuweka kwenye Lita 20 za maji zikiyeyuka tunaweka shimoni 250mls then ndio tunaotesha mmea.

Kwenye kuweka mbolea ya kukuzia kama urea au wakati wa matunda ile yenye calcium je naweza pia ichanganya na maji nikamwagia kama solution badala ya kupima na kuzungushia kwenye SHINA? Na je kama ni sawa nahapa napima 250mls pia?

Je unashaurije mkulima wa kawaida katika umwagiliaji pump zile za mafuta au moneymaker pumps hasa katika umwagiliaji wa matuta hayo? Nimeuliza kwani nahisi mmea utabaki bila udongo hapo kwani maji yakipita yatapita nao.

Na pia dizaini hii ya matuta nikitaka kufungia nyanya ile dizaini ya nguzo mbili imara halafu nyingine baada ya mita 2 nitazichomekaje kwa tuta mbili au nguzo moja moja na kushuka hivyo? Au wewe unashaurije mkuu?

Nakushukuru
 
Naomba kuuliza,je naweza panda parachichi kwa mbolea ya chumvi tu na baada ya mwaka nikaweka samadi? Nina taka kupanda mwezi wa kwanza ila nimekosa samadi.asante.
 
Asante sana mkuu ubarikiwe, dawa nimeshapiga naamini itasaidia.
 
nataka kulima sijui pakuanzia au zao gan litanilipa
 
Viazi mviringo kwa wastani vinatakiwa vipigwe booster mara ngapi mpaka kukomaa? Watu wanasema ukizidisha booster unasababisha viazi kuoza kuna ukweli. Asante.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…