Je, unataka kulima mazao ya mbogamboga na matunda lakini unakosa maarifa sahihi? Karibu tushauriane hapa

Je, unataka kulima mazao ya mbogamboga na matunda lakini unakosa maarifa sahihi? Karibu tushauriane hapa

Labda nilimjibu kwa kuoverlook tu sehemu, huwez mwagilia masaa 24 kaka tutamwagilia asubuhi kati ya sa 12 hadi sa4 asubuhi, na jioni, kama umemwagilia mda mrefu ni masaa mawili kwa drip line kwa eka1 masaa2 ni lita 20,000
Sawa mkuu nimekwelewa sasa. Je una utaalamu wa sweet pepper (pili pili hoho)? unaeza nipatia darasa lake(kama ulilotoa kwenye ovacado na tomado)? interms of spacing, mbegu mzuri, grarama zake etc... thanks in advance.
 
Mkuu sifa ziende kwa Bwana kwa kukupa maarifa na uelewa mkubwa kutujuza habari hizi.Nakupata vipi kwenye simu mkuu japo tuongee kidogo?
 
nimepiga hesabu hapo naona muda mzuri wa kupanda ni mwezi wa 9
 
Mkuu kilimomaarifa.tajiri nashukuru sana, sana kwa maelezo yako. by the way naona umetaja magomjwa lakini hujaspecify madawa. na je ukiwa unapanda mbegu kuna dawa unaweka wakati wa kupanda?
 
ASANTE MKUU. NIJITAHIDI NIWEKE MAWASILIANO YANGU KABLA YA HII JANUARY KUISHA, KWA WALE WATAKAOPENDA (HIARI) TUTAWEZA FANYA MOBILE COMMERCIAL FARMING CONSULTATION.
Mkuu kuna maswali mawili nitashukuru kama utanisaidia
1)je naweza kuendelea na kilimo cha mbaazi kwa sasa au nimeshachelewa nisubiri mpaka kipindi kingine,shamba lipo ikilishi wilaya ya kiteto
2)naomba unielezee kuhusu kilimo cha matango,mbegu ipi nzuri,maeneo gani inakubali nk
 
NAKUSHAURI ANDAA SHAMBA UPANDE PALE MASIKA INAPOKARIBIA KUISHA MWEZI WA 4/5.LENGO NI UPATE EXPERIENCE KIDOGO, NA USILIME ENEO KUBWA SANA (JUST 1/2 EKA, AU 1 EKA INATOSHA), NA KAMA MBEGU ANZA NA ZA OPV USINUNUE HYBRID (F1) KWANZA, ILI KUREDUCE RISK/LOSS. UKIPATA EXPERIENCE NDIO UTAONGEZA ENEO KUBWA NA KUTUMIA HYBRID MBEGU.
nashukuru kwa ushauri, experience ndio mwalimu mzuri kuliko wote duniani
 
vp kuhusu magugu mkuu, huwa hayasumbui nyanya? kama yanasumbua tupe na elimu ya jinsi ya kuyadhibiti kwa ufanisi
 
Magugu ni shida mkuu, kana usipoyadhibiti utakula hasara maana mbolea unayoweka italiwa na magugu maaba yenyewe yanafeed haraka sana. Cha kufanya spray glyphosate herbicides kama Roundup 60 days before kupanda mfano spray january 1, kisha rudia tena tareh 15, tena tareh 30 upande tarehe 30 february, na ujue kuwa ni muhimu sana kuondoa magugu na remains( Old crops) maana huwa ni chanzo cha wadudu na magonjwa. FIELD SANITATION ni muhimu sanaa, hizo tunaziita kama Cultural Measures/Control
Glyphosate herbicides ni non selective hapo uwe makini usije spray wakati mazao yameota. Wakati unaspray unaweza mix Glyphosate na Urea mbolea kidogo ili ile mbole istimulate magugu kumea, then yanakutana na dawa- Glypohosate then yanauwawa mpaka chini ktka mizizi kadri ile dawa/ Mbolea inavyoshuka chini. NI MUHIMU KULIMA SHAMBA VIZURI NA KUSPRAY HIZI DAWA ZA PRE INERGENCY - NON SELECTIVES HERBICIDES 60 DAYS BEFORE KUPANDA MIMEA, UKIPANDA NDANI YA SIKU 15 TANGU UPIGE NON SELECTIVE HERBICIDES, MAZAO YAKO YATAUNGUA, UWE MAKINI. ZIKO HERBICIDES BAADHI AMBAZO NI MAALUMU KWA MAZAO FULANI FULANI AMBAZO UNAPIGA WAKATI MAZAO YAKIWA YAMEOTA TAYARI. Mfano ktika zao kama Kinguu ipo dawa inaitwa Oxyfen au Sulfen hiyo unapiga between the rows vitunguu vikiwa vimemea tayari, ila ni dawa kali sana maana ni second grade Herbicides. Katika kibandiko wameandika Mls 80 za dawa kwa maji lita 20 ila ukifanya hivyo vitunguu vitaungua, inapractical mix dawa mls 40 kwa maji lita 15/20 lita. Zipo pia herbicides maalumu za kupiga ktika maharage ( bean herbicides). HIVYO NI MUHIMU SANA KUDHIBIT MAGUGU MAANA YATASABISHA HASARA- MAVUNO KIDOGO KWAKO NA HATA MENGINE NI SOURCE YA MAGONJWA.
Cc real G

Alafu mkuu kilimomaarifa.tajiri , nimerudi tena, ningeomba pia elimu kuhusu ulimaji wa mpunga/mchele kuanzia maandalizi ya shamba, mbegu, madawa na mavuno yake.
 
e bana hiyo 60 days kabla ya kupanda ni kwa eka moja nzima? au ni kwa sehemu uliyosia mbegu tu? na kwenye nyanya hakuna selective herbicides zake kama ilivyo kwa kitunguu, na kipimo cha hiyo GLYPHOSATE unachanganyaje plz, halafu naona kwenye hayo maelezo ya kuchanganya mls 80 ya oxyfen/sulfen kwa lita 20 maji kwa ajili ya shamba la vitunguu kama hujamalizia vile, malizia plz
 
mkuu nikipiga hiyo glyphosate kipindi cha mvua inabidi nichanganye na kile kinatisha sumu ulichosema ili isisafishwe na maji?
 
Prishaz


Dawa kukinga Denguwe/Kanitangaze/Tuta Absoluta-HIZI NI BAADHI TU. DAWA HIZI NI VIZURI ZIKATUMIKA KUJIAHAMI (KUKINGA) MICHE IKIWA KITALUNI, AU MARA TU UNAPOKUWA UMEHAMISHIA MICHE SHAMBANI.

1. Match 500EC (Kiambata-Lufenuron)
2. Rimon 10EC (Novaluron)
3. Actra 25WG (Thiamethoxam)
4. Duduall etc
5. Buffalo 100EC

Dawa za kutibu Denguwe/Kanitangaze/Tuta Absoluta-HIZI NI BAADHI TU YA ZILIZOTHIBITISHWA TPRI

1.Evisect 50SP (Kimbata-Thiocyclam)

2. Ascotin 0.15EC/Nimbecidine (Kiambata-Azadirachtin-Mwarobaini)
3. Coragen SC (Kiambata-Chlorantraniliprole)
4. Avaunt 150 EC/ Mavuno 25EC (Kiambata-Indoxacarb)
5. Belt 480 SC (Kiambata-Flubendiamide)

JAMBO LA MSINGI JITAHIDI KUJUA VAMBATA VILIVYOMO KATIKA HIZO DAWA, MAANA HAYO MAJINA YA DAWA (Ie Belt/ Evisect et al.. ) NI MAJINA YA KIBIASHARA TU HUBADILIKA MUDA WOWOTE

ATHARI ZA DENGUWE/KANITANGAZE/Tuta Absoluta katika zao la Nyanya

attachment.php

attachment.php


attachment.php





adult Tuta Absoluta

attachment.php

Larvae Tuta Abosluta

Tuta Absoluta Life Cycle
attachment.php
ukili nyanya ndani ya green hause ukosefu wa nyuki siutafanya nyanya ziwe seedless ana shapeless kama ulivyosema hebu fafanua
 
Kiongozi kuhusu mbaazi take time pitia uzi wangu namba 20 ukurasa wa kwanza nilikuwa namjibu mdau mmoja, upitie. Kuhusu Matango, ziko aina nyingi kutoka makampuni mbalimbali ila nazijua aina mbili[ 1. Darina F1, 2. Botonya F1, Darina ni makubwa sana kiumbo, na Botonya ni madogo kiumbo. Ziko aina za OPV kama Ashley hii ndio inapendwa sana Sokoni , umbo iko saizi ya kati na inavimiba kiasi. Utahitaji punje 13500 kwa eka moja, Matango ni kama maboga au matikiti yanapenda maji Mengi sana mwanzoni ila kadri yanavyokaribia kukomaa maji yapubguzwe. Matango yako ya kukomaa siku 45,60, na 75. Ili kuyalinda yasiharibike ni vizuri ukayafanyia staking yaani yakawa na Nguzo za kutambalia kwenda juu.MBEGU GHARAMA, punje za Hybrid 1000 zinauzwa kti ya tsh40000 hadi 45000, Mavuno yanategemeana sana na Management( Lishe, kucontrol Magonjwa,) Mavuno kwa Eka 1 ni kati ya tani 5 hadi 15. MBOLEA kama shamba ni lako ni vizuri mwanzoni ukatumia Samadi au Mboji mixed with DAP utapata mavuno mengi mazuri. WADUDU- Wengi wanaishambulia matikiti na maboga hushambulia matango, kuna wadudu kama thrips, white flies, fruit worm, na mites ( Red). Magonjwa ya UKUNGU pia huathiri sana matango,magonjwa kama UBWIRI PODA/ UNGA - Powderly Mildew,dawa kama Ivory, au Ebony72 zafaa kumaliza matatizo hayo ya Ukungu, ila ni vizuri sana ukaanza na kutumia dawa za Jamii ya Copper mapema,kama blue Copper au Tan Copper ili kukinga mimea na shida ya fangasi- Ukungu. Dawa za kutumia dhidiya wadudu ni Nyingi tu kama karate,duduall, Suberclones. BOOSTER, NImuhimu kuspray booster ili zikupe maua mengi na yasidondoke,MAANA MAUA MENGI NDIO MATUNDA MENGI,MATUNDA MENGI BORA NDIO PESA NYINGI NDIO MAENDELEO. QUOTE="brenda18, post: 15053570, member: 171429"]Mkuu kuna maswali mawili nitashukuru kama utanisaidia
1)je naweza kuendelea na kilimo cha mbaazi kwa sasa au nimeshachelewa nisubiri mpaka kipindi kingine,shamba lipo ikilishi wilaya ya kiteto
2)naomba unielezee kuhusu kilimo cha matango,mbegu ipi nzuri,maeneo gani inakubali nk
[/QUOTE]
Asante sana nimepata mwanga,ubarikiwe
 
Nikajua kuzalisha mazao ya mboga mboga na matunda. Sina au na pungukiwa na taaluma ya soko (uuzaji) na usindikaji. Nisaidieni
 
Samahani. Ninataka kulima heka moja ya vitunguu maji kwa sasa.je nimbegu gani nzuri kwa msimu huu WA mvua.
Naomba kama ukiweza nipe ushauri ewa mbolea za kutumia pamoja na dawa.nitashukuru ukinipa msaada WA elimu hiyo
 
Samahani .nataka kulima kitunguu Maji kwa sasa kwa msimu huu WA mvua .je ni mbegu gani inafaa kwa msimu WA mvua .
Nitumie mbolea gani toka kupanda hadi kuvuna pia dawa nitumie dawa zipi?.ntashukuru ukinipa jibu Niko serious
 
MAANDALIZI YA SHAMBA
Andaa shamba sasa, na upande mwezi wa pili mwanzoni
utavipeleka shambani mwezi wa tatu mwishoni au wa nne

wakati masika inaishia mwezi wa4, tunguu linajitengeneza, mvua zinapungua, utamwagia kwa muda wa miezi 2 extra

MBEGU

TUMIA JAMBAR F1-HYBRID AU NEPTUNE F1-HYBRID, AU RED BOMBAY (OPV)

MBOLEA ZA KUPANDIA
DAP, AU YARA MILLER, AU NPK YA 17:17:17

DAWA ZA WADUDU
Jiandae ununue dawa za kupambana na thrips na cut worms (Ng'onyo), Nunua Attakan au Match, kila moja lita 2, zitakutosha mpaka unavuna utakuwa unaalternate kuzipiga

MBOLEA ZA KUKUZIA
UREA, THEN CAN, AU YARA NITRABOR
Mkuu maarifa mimi nataka kuanza kulima nyanya february je mpaka navuna bei itakuwa nzuri?
 
kama utapanda mwezi wa pili kitaluni, means zitakwenda shambani march mwanzoni, ukiweka siku 45-60 shambani, utavuna mwezi wa Tano. Si mbaya sana maana bado hapo february na march wengi watakuwa wanahofia masika. Mazao ya horticulture kuanzia December mpaka May/June bei ni nzuri sana. Kama sasa gunia la debe 8 kitunguu liko tsh 160,000 sasa, Kwa upande wa nyanya sijapata bei yake, lakini masokoni nyanya 5ni tsh 1000, bilashaka ni adimu nyanya.

LEO Mabibo kitunguu 230,000. Nyanya box 30,000 lile la 40 kg
 
Back
Top Bottom