Shadeeya
JF-Expert Member
- Mar 12, 2014
- 49,759
- 118,798
- Thread starter
- #261
Jinsi nipikavyo Makande ya nazi.
Kwanza huwa nina sufuria moja hivi hilo ndio maalum kwa kuchemshia Makande 🙈🙈 hapa ni mchanganyiko wa mahindi ya kukobolewa na maharagwe. Basi yakishaiva nayashusha kisha nachukua sufuria nyingine kwa ajili ya kuungia.
Hapo tayari nimeshaandaa kitunguu maji, karoti, hoho , nyanya na nazi yangu ambayo nimeshaichuja katika sehemu mbili.
Nabandika sufuria kisha naweka mafuta kidogo yakishapata moto naweka kitunguu maji vikishachemka kidogo naweka hoho na karoti baadae naweka nyanya na chumvi kidogo. Vikishaiva namiminia makande yangu niliyoyachemsha kisha nachanganya pamoja na vikishachanganyika naweka tui langu lile jepesi ambalo huwa naliweka chache mno lengo ni nazi ikolee baada ya hapo nasubiria ichemke kwa dkk mbili tatu kisha naweka tui langu zito nalo nachanganya kidogo na kuangalia kama chumvi imekolea likishachemka kidogo nashusha. Hapo Makande yangu yanakuwa tayari kwa kuliwa.
Pia huwa siku nyingine naweka sukari kidogo. Hii huwa ni hiari ya mtu.
Kwanza huwa nina sufuria moja hivi hilo ndio maalum kwa kuchemshia Makande 🙈🙈 hapa ni mchanganyiko wa mahindi ya kukobolewa na maharagwe. Basi yakishaiva nayashusha kisha nachukua sufuria nyingine kwa ajili ya kuungia.
Hapo tayari nimeshaandaa kitunguu maji, karoti, hoho , nyanya na nazi yangu ambayo nimeshaichuja katika sehemu mbili.
Nabandika sufuria kisha naweka mafuta kidogo yakishapata moto naweka kitunguu maji vikishachemka kidogo naweka hoho na karoti baadae naweka nyanya na chumvi kidogo. Vikishaiva namiminia makande yangu niliyoyachemsha kisha nachanganya pamoja na vikishachanganyika naweka tui langu lile jepesi ambalo huwa naliweka chache mno lengo ni nazi ikolee baada ya hapo nasubiria ichemke kwa dkk mbili tatu kisha naweka tui langu zito nalo nachanganya kidogo na kuangalia kama chumvi imekolea likishachemka kidogo nashusha. Hapo Makande yangu yanakuwa tayari kwa kuliwa.
Pia huwa siku nyingine naweka sukari kidogo. Hii huwa ni hiari ya mtu.