paul c
Senior Member
- Jan 20, 2015
- 123
- 110
Heshima kwenu wanajamii wenzangu tunaokutanika katika mtandao huu. Niende moja kwa moja kwenye mada husika.
Kutokana na hali ya uchumi kuwa ngumu na mazingira ya kibiashara kuwa magumu ni awzi sasa uwekezaji unatakiwa kufanywa kwa uwangalifu mkubwa. Hapa namaanisha kuwa na uhakika katika uwekezaji unaotaka kuufanya.
Watu wamekuwa na mtazamo tofauti juu ya wapi hasa awekeze fedha aliyonayo ili kupata tija katika uwekezaji wake. Kwa kuzingatia hali ya kiuchumi na mazingira ya kibiashara basi nimekuja na hili biashara amabayo kwa sasa inashika kasi maeneo mengi ya Tanzania ili kwa watakaoona ni fursa basi tujadiliane namna ya kuanzisha hii biashara katika eneo lako unaloishi.
Aina ya biashara: STUDIO
Neno studio linatumika kama duka la kuuza cd, na dvd za movie, music, gospel, documentary etc. Kuweka music, movie na games kwenye hard disk, flash, memory card, laptops, etc. Pia kuuza flash disks, memory cards, card reader, usb cables etc.
Mahitaji:
1. Desktop computer iwe na processor kuanzia duo core, hard disk tofauti na ya operating system iwe kuanzia 4tb (terabyte nne). Hii ni ya muhimu zaidi kwani ndio mtaji kuu katika ofisi yako sehemu kubwa ya kipato itatokana na uwezo wa computer yako katika storage.
2. Sound system (subwoofer inafaa) hii ni kwa ajili ya kutangaza nyimbo na movie zilizopo ofisini kwako. Pia hutumika na wateja pindi wanapochagua nyimbo na movie.
3. Meza ya ofisi na viti vinne. Hii ni meza kwa ajili ya kuweka computer na vitu vingine. Viti ni kwa ajili ya mhudumu na wateja.
4. Mahitaji mengine ni kama extension, usb hub port 4, dvd na cd empty kopo moja, mabango ya ofisi, memory card, flash card, card reader, moderm, external hard disk 1, sleeves, marker pen, software na usb cable.
5. mazingira yanayofaa kwa kufanyia biashara husika kama chumba chenye usalama, shelve za kutundika vitu ka flash , memory n.k mapambo mengine unayopendelea katika ofisi yako.
Mahitaji yote niliyoorodhesaha hapo juu yanaghrarimu shilingi za kitanzania 3,000,000/= (milioni tatu) bila kuhusisha gharama za kodi za nyumba, leseni na mapatao na kodi nyininezo.
Baada ya kupata ufafanuzi huo sasa tuangalie masuala muhimu ya kuhusiana na biashara hii.
1. Eneo la biashara: hili ni jambo la muhimu sana wakati unachagua eneo la kuanzisha hii biashara. Kuna maeneo mengi watu wanakosa huduma ya hizi studio. Sehemu nyingine unakuta kata nzima hakuna au kijiji kizima hakuna hata moja. Anzisha kwenye hayo maeneo ndio fursa ilipo.
2. Mhudumu : hapa inahitajika mtu mwenye ujuzi wa computer katika basic issues kama kuburn cd na dvd, kusend file kwenye flash memeory, n.k, kuconvert files, kudownload, na uelewa wa format mbali mbali zinazotumika kataika simu, deki na tv. Mtu mwenye ujuzi wa kawaida wa computer anaweza kufundishwa na akaelewa kwa muda mfupi.
3. Upatikanaji wa mahitaji yote niliyoyataja: yote yanapatikana utakapo kwama utaniuliza mimi na nitatoa ufumbuzi na hata kukuletea mahitaji unayotaka kwa gharama nafuu.
4. Mapato: biashara hii inaweza kuzalisha fedha nyingi kwa kadiri unavyoweka usimamizi mzuri na upatikanaji wa mahitaji ya wateja kwa muda muafaka. Kama eneo ulilopo lina umeme wa uhakika na hakuna hii biashara unaweza kutengeneza hela nyingi kwa siku. Hapa Mara nyingi ni uwezo wa mtu kibiashara ndio unampa mapato mengi kwa siku.
5. Usimamizi : usimamizi wa karibu ni muhimu sana katika biashara hii ili kuweza kujua mahitaji ya wateja na mapungufu ya kibiashara ili kuyaborsha kwa wakati. Unaweza ukafanikiwa sana kama utafanya bishara hii peke yako kabla ya kuajiri mtu.
Chanagamoto :
1. Umeme: umeme unasababisha biashara kuwa ngumu kama utakuwa unakatika mara kwa mara. Hata wateja wengi wanategemea umeme ili kufurahia huduma hii.
2. Ujuzi: hii ni changamoto kwenye kujua format na matatizo mbalimbali yanayaowakabili wateja na kuyatatua.
Mwisho : kwa waliokuwa wanatamani kufanya biashara hii na ukawa hujui pa kuanzia karibu tuelezane namana ya kuanza na kuendesha hii biashara. Pia kwa wale waliovutiwa pia karibuni tuanzishe hii biashara na kupata kipato nitatoa muongozo wote katika hili.
Kwa wale ambao hawajavutiwa pia karibuni kwa michango mbalimbali yenye kujenga na kuelimishajuu ya kujikwamua kimaisha.
karibuni wote kwa maboresho au maswali au maoni kuhusiana na hili.
Kutokana na hali ya uchumi kuwa ngumu na mazingira ya kibiashara kuwa magumu ni awzi sasa uwekezaji unatakiwa kufanywa kwa uwangalifu mkubwa. Hapa namaanisha kuwa na uhakika katika uwekezaji unaotaka kuufanya.
Watu wamekuwa na mtazamo tofauti juu ya wapi hasa awekeze fedha aliyonayo ili kupata tija katika uwekezaji wake. Kwa kuzingatia hali ya kiuchumi na mazingira ya kibiashara basi nimekuja na hili biashara amabayo kwa sasa inashika kasi maeneo mengi ya Tanzania ili kwa watakaoona ni fursa basi tujadiliane namna ya kuanzisha hii biashara katika eneo lako unaloishi.
Aina ya biashara: STUDIO
Neno studio linatumika kama duka la kuuza cd, na dvd za movie, music, gospel, documentary etc. Kuweka music, movie na games kwenye hard disk, flash, memory card, laptops, etc. Pia kuuza flash disks, memory cards, card reader, usb cables etc.
Mahitaji:
1. Desktop computer iwe na processor kuanzia duo core, hard disk tofauti na ya operating system iwe kuanzia 4tb (terabyte nne). Hii ni ya muhimu zaidi kwani ndio mtaji kuu katika ofisi yako sehemu kubwa ya kipato itatokana na uwezo wa computer yako katika storage.
2. Sound system (subwoofer inafaa) hii ni kwa ajili ya kutangaza nyimbo na movie zilizopo ofisini kwako. Pia hutumika na wateja pindi wanapochagua nyimbo na movie.
3. Meza ya ofisi na viti vinne. Hii ni meza kwa ajili ya kuweka computer na vitu vingine. Viti ni kwa ajili ya mhudumu na wateja.
4. Mahitaji mengine ni kama extension, usb hub port 4, dvd na cd empty kopo moja, mabango ya ofisi, memory card, flash card, card reader, moderm, external hard disk 1, sleeves, marker pen, software na usb cable.
5. mazingira yanayofaa kwa kufanyia biashara husika kama chumba chenye usalama, shelve za kutundika vitu ka flash , memory n.k mapambo mengine unayopendelea katika ofisi yako.
Mahitaji yote niliyoorodhesaha hapo juu yanaghrarimu shilingi za kitanzania 3,000,000/= (milioni tatu) bila kuhusisha gharama za kodi za nyumba, leseni na mapatao na kodi nyininezo.
Baada ya kupata ufafanuzi huo sasa tuangalie masuala muhimu ya kuhusiana na biashara hii.
1. Eneo la biashara: hili ni jambo la muhimu sana wakati unachagua eneo la kuanzisha hii biashara. Kuna maeneo mengi watu wanakosa huduma ya hizi studio. Sehemu nyingine unakuta kata nzima hakuna au kijiji kizima hakuna hata moja. Anzisha kwenye hayo maeneo ndio fursa ilipo.
2. Mhudumu : hapa inahitajika mtu mwenye ujuzi wa computer katika basic issues kama kuburn cd na dvd, kusend file kwenye flash memeory, n.k, kuconvert files, kudownload, na uelewa wa format mbali mbali zinazotumika kataika simu, deki na tv. Mtu mwenye ujuzi wa kawaida wa computer anaweza kufundishwa na akaelewa kwa muda mfupi.
3. Upatikanaji wa mahitaji yote niliyoyataja: yote yanapatikana utakapo kwama utaniuliza mimi na nitatoa ufumbuzi na hata kukuletea mahitaji unayotaka kwa gharama nafuu.
4. Mapato: biashara hii inaweza kuzalisha fedha nyingi kwa kadiri unavyoweka usimamizi mzuri na upatikanaji wa mahitaji ya wateja kwa muda muafaka. Kama eneo ulilopo lina umeme wa uhakika na hakuna hii biashara unaweza kutengeneza hela nyingi kwa siku. Hapa Mara nyingi ni uwezo wa mtu kibiashara ndio unampa mapato mengi kwa siku.
5. Usimamizi : usimamizi wa karibu ni muhimu sana katika biashara hii ili kuweza kujua mahitaji ya wateja na mapungufu ya kibiashara ili kuyaborsha kwa wakati. Unaweza ukafanikiwa sana kama utafanya bishara hii peke yako kabla ya kuajiri mtu.
Chanagamoto :
1. Umeme: umeme unasababisha biashara kuwa ngumu kama utakuwa unakatika mara kwa mara. Hata wateja wengi wanategemea umeme ili kufurahia huduma hii.
2. Ujuzi: hii ni changamoto kwenye kujua format na matatizo mbalimbali yanayaowakabili wateja na kuyatatua.
Mwisho : kwa waliokuwa wanatamani kufanya biashara hii na ukawa hujui pa kuanzia karibu tuelezane namana ya kuanza na kuendesha hii biashara. Pia kwa wale waliovutiwa pia karibuni tuanzishe hii biashara na kupata kipato nitatoa muongozo wote katika hili.
Kwa wale ambao hawajavutiwa pia karibuni kwa michango mbalimbali yenye kujenga na kuelimishajuu ya kujikwamua kimaisha.
karibuni wote kwa maboresho au maswali au maoni kuhusiana na hili.