Nimekuelewa japo sio sana, nitakuelewa zaidi ukinisaidia pia maswali haya...
Nilipopita pale tazara, (FLY OVER YETU) niliona bango limeandikwa "kwa ufadhili wa watu wa JAPAN" (najiuliza hapa tuwashukuru watu wa JAPAN au JPM?)
NASIKIA ubungo pia kutakuwa na bango kubwa lililoandikwa "KWA UFADHILI WA BENKI YA DUNIA" (Kama ni kweli, tushukuru benki ya dunia au JPM?)
Lakini pia, naomba nisaidie mkuu, baba yangu aliye staafu tangu mwaka 2018 amekuja lipwa mwaka 2020, yeye pamoja na wenzake waliokumbana na adha hiyo nao wamshukuru JPM?
Watumishi wa umma waliokaa miaka 5 pasipo kulamba nyongeza ya mishahara yao wala kuona juhudi zozote za makusudi kuboresha basic salary zao (wamshukuru JPM?)
Wakulima wa korosho kule kusini je? Nao wamshukuru JPM?
Vipi wahitimu wa elimu ya juu,tangu mwaka 2015 ajira zao ni kitendawili haswa, nao wamshukuru JPM?
Wananchi wa kimara, waliopoteza makazi yao, wakiishi kama wakimbizi baada ya bomoa bomoa iliyozuiwa na mahakama, lakini ikaagizwa zivunjwe haraka, nao pia wamshukuru JPM?
Ukinifafanulia haya machache nitakushukuru sana na pengine nitaungana nawe kuhakikisha natoa shukrani zangu za dhati pia...