Uchaguzi 2020 Je, Unaweza kupita Ubungo Interchange usiseme asante Magufuli? Mtakubaliana na mimi, asante stahiki ni kura zote kwa Magufuli

Uchaguzi 2020 Je, Unaweza kupita Ubungo Interchange usiseme asante Magufuli? Mtakubaliana na mimi, asante stahiki ni kura zote kwa Magufuli

Paskali, Paskali ukiona huteuliwi pamoja na kuwa na sifa zote na kuunga mkono juhudi ujue wewe mwenyewe una tatizo ni vizuri ukajirekabisha au ukabadili mbinu lakini sanasana ungengoja mpaka baada ya Uchaguzi na achaguliwe ndio usifie maana kuna wagombea wengine 15.

Miradi mingi, ikiwa ni pamoja na Ubungo Flyover, Mfugale, Salender Bridge, ni miradi ya Awamu za nyuma iliyoanza au iliyokamilika Awamu ya Tano kama itakavyokuwa miradi ya SGR, Stiegler's Gorge na mingine ambayo itakamilika (hopefully) Awamu ya Saba. Ubungo na TAZARA Flyovers ni madaraja juu ya barabara tu siyo interchange kama mshamba Mayalla (Njaa) anavyokuza na kusifia.

Hata madege yatabaki an eyesore kwa watu wa Dar mpaka yatakapohamishiwa kwenye mapumziko yao ya milele kule homeport yakikamilika. Give credit where it is due!
 
Ujuha na njaaa zako zilipelekee familia yako, Kwamba amemuozesha mtoto ndio kapata pesa za kujengea?? Au kauza mashamb yake?? Kodi hatuwezi kushukuru sio hisani ni wajibu wa SERIKALI. Kadili siku zinavyoenda kiwango chako chakuwa po.po.ma kimaongezeka!! Inawezeka kupata zero kwenye kura za maoni ni chanzo.
 
Mkuu Paskali, ktk hili kila mtu anaona kodi ya wananchi imetendewa haki kwa kuwa huo ndiyo wajibu wa serikali yenye kuwajibika vyema kwa wananchi wake. Lakini hili tu haliwezi kuwa sababu ya yeye kuzidi kuaminika kuendelea kushika madaraka aliyokabidhiwa ya kuongoza taasisi nyeti ya uraisi.

Je! Tujiulize katika masuala mengine ya kiutawala aliweza pia kufanya vyema? Kwa kuwa cheo cha Rais ni cha kikatiba, ambapo mamlaka aliyokuwa nayo alipewa kupitia kwayo. Na hata pia aliapa kuitii, kuilinda na kuitumikia kwa kiapo alichokifanya mbele za Mungu na umma wa Watanzania.

Je! Tunaweza kumpima ni kwa kiasi gani ameweza kutii katiba, sheria na kanuni nyingine ambazo zote zimetungwa kupitia misingi ya katiba yetu? Daraja la Ubungo pekee kamwe haliwezi kuwa "stand alone criterion" ya kuweza kumfanya azidi kuaminika. Ni lazima apimwe kupitia vigezo vingine kama vile maendeleo ya watu ambayo ameshindwa kuyatekeleza kwa kiwango kinachothibitika.
 
Yaani mimi mwananchi wa ngudu nije nimpe kura mtu aliejenga daslamu ili hali huku kwetu katukacha? Wanaopita hizo barabara watampigia kura. Sijui wewe ni mwanasheria wa wapi mpumbavu kiasi hiki
 
Nilikuwa nimebakisha asilimia 10 za kukuheshimu kama mwandishi wa habari nguli ulie bobea. Kwanini kwasababu ulikuwa unasimamia hoja na kuongoza mijadalaa hadi rahaaa. Kaka Tatizo ninini? Umrii?

Au uteuziii? By that time hukuwa mwanasheria now days ukajiendeleza but what your doing is rubbish bakisha hata kidogo kwa heshima ya kizazi chakoo
 
JPM kapiga kazi ya maana na kimaadili ni kiongozi bora kuliko Lissu kwa mara elfu kumi.

Lissu anamkejeli Mwalimu Nyerere asiyeweza kujitetea halafu anakwenda kutembelea Butiama.

Lissu anawatukana polisi akiwa jukwaani halafu akishuka chini ni hao hao wanaomlinda!!.
Kutaja madhaifu yako sio tusi wewe bwana mdogo. Kwani mwalimu alikuwa ni Mungu? Kwamba hakukosea? Yeye mwenyewe alishawahi kusema ameshafanyaga mambo ya kijinga
 
Flyover zinajengeka bila kuteka, kupoteza, kupiga risasi ama kuminya uhuru wa raia. Kutamka neno "vyuma vimekaza" imesababisha watu kuwekwa ndani!!,
 
Yes Kitu Kidogo huzaaa Kitu kikubwa. Mwache Pasco Afurahi na Ashukuru kwa kdogo Daima Kama Huwezi Shukuru jambo Dogo , Huwezi Shukuru jambo kubwa. Habari ya Pole Kabudi Ndio Siasa hiyo Kijanaa HAKUNA Sisa Isiyo na Migongano na Daima HAKUNA nchi inayolea wasaliti

BAVICHA MKUE BASI KIDOGO
 
Laiti Ingekuwa hawa wapiga kura wote wa kitaa ndo hawa wana jf humu wote basi Lissu angekuwa Rais wa awamu ya sita kutoka upinzani,
Pipozzzz pawaaaaaa
 
Kweli Pascal na usomi wako unaita yale madaraja mawili pale ubungo kuwa ni Interchange?!
 
Wasukuma mmezidi ushamba, na wewe ni mshamba mwingine, ashukuru kodi zako sio Magufuli wenu. Hivi pesa katoa mfukoni?
 
Je, unaweza kulala Ikulu ya Magogoni bila kumsifu beberu Mjerumani? Hivi ni vitu ambavyo lazima viwepo nchini maadamu tunalipa kodi.
 
Kutaja madhaifu yako sio tusi wewe bwana mdogo. Kwani mwalimu alikuwa ni Mungu? Kwamba hakukosea? Yeye mwenyewe alishawahi kusema ameshafanyaga mambo ya kijinga
Kabisa mkuu, na alisisitiza kwamba yale ya kijinga tuyaache.
 
JPM kapiga kazi ya maana na kimaadili ni kiongozi bora kuliko Lissu kwa mara elfu kumi...
Mmezoea kuishi kwa uongo, Musa alimkosoa Mungu kuwa asiwateketeze wana wa Israel kwani mataifa watamdhihaki kuwa aliwatoa watu wake Misri kuja kuwateketeza jangwani na Mungu akamsikia, sembuse kumkosoa Nyerere aliyekiri mwenyewe kuwa alifanya makosa mengi.

Tatizo lumumba mmejaa unafiki, mlimjaza Makonda unafiki mwishowe mkabwaka, mnajaza Magufuli sifa za uongo naye atapita
 
Yani majukumu ya serikali leo hii inageuka fadhila? Halafu huyu anaesema haya ni mtu mwenye LL.b hahahah...[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
Elimu elimu elimu.
 
UMEUA MCHANA KWEUPE.
Mayalla amenifanya kuwatilia shaka wasukuma
 
Back
Top Bottom