Uchaguzi 2020 Je, Unaweza kupita Ubungo Interchange usiseme asante Magufuli? Mtakubaliana na mimi, asante stahiki ni kura zote kwa Magufuli

Kumbe ana LL.B
Ni hasara tuu.. ndiyo maana mimi nina kabachela tuu lakini hawa wanajiita ma PhD holders siwaogopi hata kidhungu cha kuombea maji ya kunywa hawajui
 
Wito kwa wana JF tuliojiandikisha, Tarehe 28 October, tujitokeze kwa wingi tukapige kura kwa ama kutoa shukrani zetu kwa mazuri tunayo tendewa na serikali ya awamu ya tano ama.
Paskali
Na kwa waliotendewa mabaya unawapa wito gani?
 
Mimi nasema asante kwa walipa kodi wa Lindi ambao Rais m'baguzi amewaambia hatopeleka maendeleo kwenye jimbo lao kwasababu tu mbunge wao ni mpinzani lakini kodi zao zimehusika kwenye huo ujenzi.

Pascal siku ukiotea tenda ya ile ofisi yako ya media na ukawekewa pesa kwenye bank account, ukienda kutoa pesa kwenye ATM usisahu kusema "Asante ATM kwa kunipa pesa"
 
Kwanza wewe unataka kumchonganisha Rais na wapiga kura, yeye na tushukuru tulimpa kibarua na anatupigia magoti hadharani labda tumfikirie tena sasa unasema tumshukuru tena?? Ndiyo maana ulipigwa chini kwenye kura za maoni, upo double standard and hypocrite sana wewe baba
 

Attachments

  • Basii.jpg
    8.9 KB · Views: 1
Jamaa ningekuwa karibu yako haki ningekulipia dinner ya leo, umejua kuusema ukweli hadi ukweli wenyewe unashangaa!
 
Hivi wakati anaweka jiwe la msingi si alisema shukrani na pongezi ziende kwa JK? Kwa kuwa chini ya utawala wake alikuwa keshafanya feasibility study, mchoro ambao baadaye ulichakachuliwa, mkopo ulishapatikana kutoka WB na mkandarasi alikuwa kashapewa kazi, sasa kwanini sifa apewe mtu mwingine?
 
Ni kwel ila zile kodi zetu za Chato sijui nazo tashukuru au tuachane nazo kwa kuwa haizikuwepo kwenye ilani
 
Mkuu,

Bado unaamini kwamba huu utawala utarudi madarakani? Nahisi kama mwaka huu unacheza pata potea na kwa kiasi fulani umecherewa kuwaonyesha msimamo wako. Kwa maoni yangu, hata kama ukirudi madarakani utawala huu naamini hautakuwa tena ule wa honga honga. Kwa nini nasema hivi? Kwa sababu hawatahitaji tena watu kama nyie kwa vile malengo yao yatakuwa yameshatimia. Na kwa hio watu aina yenu watakuwa na status kama ya Lipumba tu!
 
Labda upite uwe umevimbiwa Kama wewe Pasco lakini ukipita wakati umeshindia mihogo ya ferry na mahindi ya kuchoma na kesho hujui itaamkaje utaishia kumlaani hata kumtusi kimoyomoyo!
 
Shukurani ziende kwa watanzania wanaolipa kodi. Praise & Worship tusisahau hizi ni fedha za umma!

Siwezi kuishukuru serikali kutimiza wajibu wake.

Kesho P utakuja na mada tushukuru Gwajiboy kaanza kujenga kanisa lake, lisionekana kama banda la kufugia misukule.

Everyday is Saturday.............................. 😎
 
Ukijsikia kujibu hili swali, naomba ufanye hvo.

Hv flyover iliyopo Dar inamnufaishaje mtu anayeishi Kigoma penye tatizo la barabara, je majimbo yenye shida ya maji yanafaidika nini na flyover?

Binafsi sikatai kumsifia Magufuli, ila mnaosifia mnavuka mipaka kiasi cha kumfanya kama mungu kwamba bila yeye hakuna Tanzania.

Kingine, mzee unazeeka vibaya sana.
 
Yani majukumu ya serikali leo hii inageuka fadhila? Halafu huyu anaesema haya ni mtu mwenye LL.b hahahah...πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€
mkibanwa mnasema majukumu ya serikali,mnapolia mnasema serikali haijafanya kitu,aliewaroga kafa
 
Kule mahoteli tunatoa sana tip za ahsante kuhudumiwa vyema japo tumelipia ni vyema kushukuru awamu ya 5
 
Wasukuma ushamba hauwatokagi hata mkiwa na elimu. Yani mtu mwenye akili timamu katika nchi yenye watu milioni 60 maskini inashangilia daraja? Unasahau watu waliopptezwa, waliouawa, walootekwa, wsliofilisiwa, waliobambikiwa kesi, ufisadi wa mabilioni nk? Njaa na ukabila ni ugonjwa hatari sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…