Uchaguzi 2020 Je, Unaweza kupita Ubungo Interchange usiseme asante Magufuli? Mtakubaliana na mimi, asante stahiki ni kura zote kwa Magufuli

Uchaguzi 2020 Je, Unaweza kupita Ubungo Interchange usiseme asante Magufuli? Mtakubaliana na mimi, asante stahiki ni kura zote kwa Magufuli

Hivi nikienda ATM kuchukua fedha zangu natakiwa kuisifia machine ya ATM? barabara zinajengwa kwa kodi zetu vipi tunaambiwa tumsifie mtu? Tena aliyeanza kuijenga (Kikwete) hakutaka kusifiwa kwani alijua anatimiza wajibu wake!
 
Pesa zetu tumshukuru yeye tena yeye anapaswa kutushukuru sisi kwakuwa malengo yake huko Chato yanatimia
wacha uongo ni msaada wa japan na korea, mshukuru jpm tu, kodi yako imeliwa na mdee kamuulize hela za mfuko wa jimbo ziko wapi?
 
Hivi nikienda ATM kuchukua fedha zangu natakiwa kuisifia machine ya ATM? barabara zinajengwa kwa kodi zetu vipi tunaambiwa tumsifie mtu? Tena aliyeanza kuijenga (Kikwete) hakutaka kusifiwa kwani alijua anatimiza wajibu wake!
kwakipato gani unalipa kodi? hako ka payr kako hata mita moja ya mtaro hakawezi jenga
 
Hivi ndugu yangu Mayala tangu lini umekuwa kichaa????Tumpe jpm asante kwani Fedha katoa mfukoni mwake??hata jiwe la msingi nakumbuka ni Gharib bilal ndio aliweka akiwa makamu wa raisi tz!!!
 
mimi nakula vumbi huku kasulu wew unaleta habari za fly ova wew ni mpuuzi kabisa mimi inanihusu nini..? atoe vumbi mkoa wa kigoma acheni ubinafsi hii nchi ni ya wote
 
Wajinga ni wale wanaomuona Lissu kuwa ni mkombozi wakati ni dalali wa Amsterdam na wapumbavu wengine wa huko ulaya.
Na magu ni mkombozi na dalili wa nani? Kama si dalali wa Barrick awake hadharani makubaliano aliyoingia na barrick tuone? You are a stupid ideot
 
Wanabodi

Hili ni bandiko la swali, Jee ukitendewa wema, unatoa shukrani? Jee Sisi Watanzania ni watu wa shukrani?. Kwa wema wote tuliofanyiwa na serikali ya awamu ya 5 katika kutuletea maendeleo, tarehe 28 October tutatoa shukrani au?

Kama kitu Watanzania wanachotaka ni maendeleo, then Magufuli ni Maendeleo!.

Leo, baada ya kupita kwenye ile Ubungo Interchange, kiukweli nimejikuta roho kwatu. Kwa wale wote wanayoyajua mateso ya foleni ya Port Access Rd, leo unasimama Tazara tu kidogo, then unasimama Buguruni kidogo, baada ya hapo ni unateleza tu, hakuna foleni, hakuna kusimama popote, na ukifika Ubungo, ni kama unapaa juu, kushuka foleni unakuja kuikuta Mwenge.

Wale wote waliokuwa wanateswa na foleni ya Tazara, Buguruni, Tabata, Ubungo, na wengine wote watakaopita hapo, Ubungo Interchange, kama ni watu wa shukrani, utakubaliana na mimi, utajikuta unawiwa, kumshukuru Magufuli na kumwambia "asante Baba Magufuli" na utajikuta, namna pekee ya kumshuru Magufuli, ni kwa tarehe 28 October kura zote ni kwa Magufuli!, na kama shukrani kwa Magufuli, then kura zote ni kwa CCM.

Ukiwa ni mtu wa shukrani, ukitendewa vyema, utajikuta una wajibu wa kushukuru, hata kama huyo anayekutendea ni anatimiza wajibu wake, lakini kama ni mtu wa shukrani bado utashukuru!.

Hata zile huduma, unazinunua bei ya jumla, kwa kulipia mahari, ni mali yako, jukumu lake ni kukudumia, na katika kutoa huduma hizo ni kutimiza wajibu wake, lakini kwa wenye shukrani, ukihudumiwa bado unashukuru na kusema asante, hivyo hata kama ni jukumu la serikali kuleta maendeleo, serikali ikileta maendeleo, ishukuriwe. Magufuli akileta maendeleo ashukuriwe, CCM ikileta maendeleo hata kama ni ya utekelezaji wa ilani yake, ishukuriwe!.

Shukrani pekee stahiki ni Tarehe 28 October!

NB, na ukitendewa vyema, ukawa ni mtovu wa shukrani ujue ... naomba nisimalizie.

Namalizia kwa hili swali la msingi la bandiko hili. Jee ukitendewa wema, unatoa shukrani?. Jee Sisi Watanzania ni watu wa shukrani?. Kwa wema wote tuliofanyiwa na serikali ya awamu ya 5 katika kutuletea maendeleo, jee tarehe 28 October tutatoa shukrani au ...?

Wito kwa wana JF tuliojiandikisha, Tarehe 28 October, tujitokeze kwa wingi tukapige kura kwa ama kutoa shukrani zetu kwa mazuri tunayo tendewa na serikali ya awamu ya tano ama.

Paskali
Sasa ndio tukeshe kwa kumsifu na mapambio? Je hakuna eneo alilokosea katika utawla wake? Sisi tunaona Hafai si kwa kuwa hakujenga Barabara ,laa bali kwa Mengine yahusuyo haki za watu na maisha yao,Katiba Mpya n.k upande huu kateleza. na kwa hiyo Tutamuhukumu kwa kutomchagu kuwa raisi., akiwa Ubaoni Tutakwenda kuchukua Ushauriwake akiwa kama Mpizani. Mbola limekaa vizuri hili.

Baada ya Kupata Katiba yetu mpya ambayo CCM hawawezi kulifanya hilo Tutawaalika waje kuibariki na kutia neno
Wanabodi

Hili ni bandiko la swali, Jee ukitendewa wema, unatoa shukrani? Jee Sisi Watanzania ni watu wa shukrani?. Kwa wema wote tuliofanyiwa na serikali ya awamu ya 5 katika kutuletea maendeleo, tarehe 28 October tutatoa shukrani au?

Kama kitu Watanzania wanachotaka ni maendeleo, then Magufuli ni Maendeleo!.

Leo, baada ya kupita kwenye ile Ubungo Interchange, kiukweli nimejikuta roho kwatu. Kwa wale wote wanayoyajua mateso ya foleni ya Port Access Rd, leo unasimama Tazara tu kidogo, then unasimama Buguruni kidogo, baada ya hapo ni unateleza tu, hakuna foleni, hakuna kusimama popote, na ukifika Ubungo, ni kama unapaa juu, kushuka foleni unakuja kuikuta Mwenge.

Wale wote waliokuwa wanateswa na foleni ya Tazara, Buguruni, Tabata, Ubungo, na wengine wote watakaopita hapo, Ubungo Interchange, kama ni watu wa shukrani, utakubaliana na mimi, utajikuta unawiwa, kumshukuru Magufuli na kumwambia "asante Baba Magufuli" na utajikuta, namna pekee ya kumshuru Magufuli, ni kwa tarehe 28 October kura zote ni kwa Magufuli!, na kama shukrani kwa Magufuli, then kura zote ni kwa CCM.

Ukiwa ni mtu wa shukrani, ukitendewa vyema, utajikuta una wajibu wa kushukuru, hata kama huyo anayekutendea ni anatimiza wajibu wake, lakini kama ni mtu wa shukrani bado utashukuru!.

Hata zile huduma, unazinunua bei ya jumla, kwa kulipia mahari, ni mali yako, jukumu lake ni kukudumia, na katika kutoa huduma hizo ni kutimiza wajibu wake, lakini kwa wenye shukrani, ukihudumiwa bado unashukuru na kusema asante, hivyo hata kama ni jukumu la serikali kuleta maendeleo, serikali ikileta maendeleo, ishukuriwe. Magufuli akileta maendeleo ashukuriwe, CCM ikileta maendeleo hata kama ni ya utekelezaji wa ilani yake, ishukuriwe!.

Shukrani pekee stahiki ni Tarehe 28 October!

NB, na ukitendewa vyema, ukawa ni mtovu wa shukrani ujue ... naomba nisimalizie.

Namalizia kwa hili swali la msingi la bandiko hili. Jee ukitendewa wema, unatoa shukrani?. Jee Sisi Watanzania ni watu wa shukrani?. Kwa wema wote tuliofanyiwa na serikali ya awamu ya 5 katika kutuletea maendeleo, jee tarehe 28 October tutatoa shukrani au ...?

Wito kwa wana JF tuliojiandikisha, Tarehe 28 October, tujitokeze kwa wingi tukapige kura kwa ama kutoa shukrani zetu kwa mazuri tunayo tendewa na serikali ya awamu ya tano ama.

Paskali

Yatupasa kuwashukuru wakoloni pia ,maana hata wao waliikuta Tanzania haina shule , wala Hopitali wala Reli wala Barabara.
Wao walijenga vitu hivyo kama serikali pamaoja na Haja za kiuchumi walizokuwa nazo lakini Serikali ndio ilisimamia kuyafanya hayo kwa manufaa ya Taif zima.
Je na wao Tuwatupie Sifa kabla ya CCM na serikali yake??

Hebu tukubaliane kuwa Serikali kusimamia Maendeleo ni wajibu wake wa Msingi na wa Lazima, si suala la kuwaaliye fanya katufanyia Fadhila na kwa hiyo Tukeshe kwa kumsifia.
Kwani sisi Wapinzania tumemlaumu Raisi kwa kujenga Reli, bwawa la umeme au Hospitali? Si katimiza wajibu wake.
sisi tunamlaumu kwa Kunyima haki za watu z Kujieleza, kisiasa, kiuchumi na ukandmizaji mwingine wa uhuru wa watanzania.
 
Wee jamaa kanjanja sana, unaingia kwenye uchaguzi unaambulia kura yako mwenyewe. Unaonyesha jinsi gani usivyoweza kujenga hoja hata kushawishi watoto wa chekechea..
 
Tundu Lissu aliwahi kusema kuwa "Tunamshukuru Rais Magufuli kwani kwa namna moja ametusaidia kufagia takataka ndani ya chama chetu"

Na mimi namshukuru kwani amenisaidia kujua kuwa baadhi ya watanzania kuuza utu wao au kujidharaulisha kutokana na njaa ili apate chochote kitu ni swala la muda mfupi sana.

Unajua Tanzania ipo nyuma sana kidemokrasia na kuwa na watu wenye akili kwakuwa tumetengwa eneo moja na tukajikuta tumekaa na mazuzu wengi.

Pascal Mayalla anajua kuwa kwa vyovyote vile kama kiongozi huwezi kufanya jambo la maendeleo ya miundo mbinu kuwa hisani ya kutesa, kuua, kunyima wengine haki na kuzuia watu wasikukosoe. Ila kwa kuwa ni moja ya watanzania aliowasema Tundu Lissu ndiyo maana unamuona anachotuletea humu.

Hivi kweli ukiwa mtanzania mwenye akili timamu unaanzaje kumshabikia Magufuli? Narudia tena, unaanzaje? Emb tuweni na aibu jamani! Tunachekwa na dunia.

Ila ndiyo watanzania wenzetu, tunaishi nayo humu humu Tanzania.

Hili linchi nadhani limekuwa likubwa halafu hata faida ya kuwa linchi likubwa haionekani. Uwe na linchi likubwa basi walau ionekane faida yake. Halafu nawaza sana inakuwaje mfano mtu kama huyu mleta mada unaweza kukuta kasoma hadi chuo kikuu tena kwa kufaulu lakini ona alivyo na uwezo mdogo wa kufikiri mambo kwa undani.

Unajua zuzu likiona kitu kidogo tu linalipuka kwa shangwe maana huwa halina uwezo wa kujiuliza. Huyu mleta mada kapita tu kwenye barabara ya juu ghafla kaona ewaaa matatizo yote yameisha Tanzania. Anaenda kulala ana amani kabisa kabisa. Nataka uone ni jinsi gani tulivyo na watanzania mazuzu.

Walikuwepo kina Bashiru, Polepole kina Ryoba kina Kabudi. Hawa tulikuwa tukiwaona wakiwa mstari wa mbele kuhubiri haki. Lakini kumbe wooote ni mazuzu. Walikuwa wanaongozwa na shida binafsi. Sasa wamepata kidogo na kwakuwa hawana uwezo wa kufikiri tena baada ya kupata imekuwa basi. Hawa ni watanzania walioenda shule lakini ona vichwani mwao kwa sasa.

"Stupid generarion"
Umemena vyema kwamba "kujidharilisha kutokana na njaa (aka mayalla kule kwetu) ili apate chochote". Sina uhakika, lakini pengine jina linaakisi ukweli huu.
 
Wanabodi

Hili ni bandiko la swali, Jee ukitendewa wema, unatoa shukrani? Jee Sisi Watanzania ni watu wa shukrani?. Kwa wema wote tuliofanyiwa na serikali ya awamu ya 5 katika kutuletea maendeleo, tarehe 28 October tutatoa shukrani au?

Kama kitu Watanzania wanachotaka ni maendeleo, then Magufuli ni Maendeleo!.

Leo, baada ya kupita kwenye ile Ubungo Interchange, kiukweli nimejikuta roho kwatu. Kwa wale wote wanayoyajua mateso ya foleni ya Port Access Rd, leo unasimama Tazara tu kidogo, then unasimama Buguruni kidogo, baada ya hapo ni unateleza tu, hakuna foleni, hakuna kusimama popote, na ukifika Ubungo, ni kama unapaa juu, kushuka foleni unakuja kuikuta Mwenge.

Wale wote waliokuwa wanateswa na foleni ya Tazara, Buguruni, Tabata, Ubungo, na wengine wote watakaopita hapo, Ubungo Interchange, kama ni watu wa shukrani, utakubaliana na mimi, utajikuta unawiwa, kumshukuru Magufuli na kumwambia "asante Baba Magufuli" na utajikuta, namna pekee ya kumshuru Magufuli, ni kwa tarehe 28 October kura zote ni kwa Magufuli!, na kama shukrani kwa Magufuli, then kura zote ni kwa CCM.

Ukiwa ni mtu wa shukrani, ukitendewa vyema, utajikuta una wajibu wa kushukuru, hata kama huyo anayekutendea ni anatimiza wajibu wake, lakini kama ni mtu wa shukrani bado utashukuru!.

Hata zile huduma, unazinunua bei ya jumla, kwa kulipia mahari, ni mali yako, jukumu lake ni kukudumia, na katika kutoa huduma hizo ni kutimiza wajibu wake, lakini kwa wenye shukrani, ukihudumiwa bado unashukuru na kusema asante, hivyo hata kama ni jukumu la serikali kuleta maendeleo, serikali ikileta maendeleo, ishukuriwe. Magufuli akileta maendeleo ashukuriwe, CCM ikileta maendeleo hata kama ni ya utekelezaji wa ilani yake, ishukuriwe!.

Shukrani pekee stahiki ni Tarehe 28 October!

NB, na ukitendewa vyema, ukawa ni mtovu wa shukrani ujue ... naomba nisimalizie.

Namalizia kwa hili swali la msingi la bandiko hili. Jee ukitendewa wema, unatoa shukrani?. Jee Sisi Watanzania ni watu wa shukrani?. Kwa wema wote tuliofanyiwa na serikali ya awamu ya 5 katika kutuletea maendeleo, jee tarehe 28 October tutatoa shukrani au ...?

Wito kwa wana JF tuliojiandikisha, Tarehe 28 October, tujitokeze kwa wingi tukapige kura kwa ama kutoa shukrani zetu kwa mazuri tunayo tendewa na serikali ya awamu ya tano ama.

Paskali
NGOJA nikukumbushe kidogo!Wakati wa Mwalimu Nyerere .Wasafiri wa Tanga walikuwa walipanda mabasi pale mnazi mmojq kama saa 12 .30 hivi za jioni kuelekea Tanga .Na walikuwa wakifika Tanga majira ya saa 10 hivi za alfajiri sababu ya ubovu wa barabara .Kiongozi anapotengeneza miundo mbinu ni jukumu lake
 
Back
Top Bottom