Magufuli hakuwahi kusafiri nje ya Africa na wala hakupandisha gharama za maisha lakini alifanya yafuatayo.............👇

1. JPM anajenga Reli ya Mwendo kasi – SGR.
2. JPM anajenga Bwawa la Umeme – Nyerere HydroPower.
3. JPM amenunua Ndege 13 aina tofautitofauti.
4. JPM amejenga Ikulu kule Dodoma na yale Magorofa ya Wizara kule Mji wa Serikali Dodoma ( Mtumba) Magufuli City
5. JPM amehamisha Makao Makuu ya Serikali na ameijenga Dodoma imekuwa Jiji
6. JPM amejenga FlyOver Dar es Salaam pale Ubungo na TAZARA.
7. JPM amejenga daraja la Tanzanite pale Selander.
8. JPM ametengeneza huu Mfumo wa Kompyuta wa Malipo ya Serikali.
9. JPM alikuwa anaweka umeme hadi Vijijini (kwa Tsh. 27,000/= tu.)
10. JPM ameshawishi Bomba la Mafuta kutoka Uganda lipite Tanzania.
11. JPM anajenga daraja la Kingongo Ferry Busisi kule ziwa Victoria.
12. JPM amejenga Meli kubwa mbili mbili kila ziwa, yaani Ziwa Victoria 2, Ziwa Tanganyika 2 na Ziwa Nyasa 2.
13. JPM amejenga Hospital za Kanda kubwa nne… Dodoma, Mara, Mtwara, Geita na Songea
14. JPM amejenga Hospitali za Wilaya Zaidi ya 70
15. JPM amejenga Mradi Mkubwa wa Maji ya Victoria kule Tabora
16. JPM amejenga Mradi wa Maji Mkubwa Arusha
17. JPM amejenga Barabara ya Njia Nane Dar es Salaam hadi Kibaha
18. JPM alikuwa anajenga Mizani za Kisasa kabisa Kwenye Barabara zote kubwa
19. JPM amejenga Vituo vya Afya Zaidi ya 500
20. JPM amejenga na Kununua Rada 4 za AirPort
21. JPM amejenga Viwanja vya Ndege Mara, Iringa, Mbeya, Chato, Songea na Rukwa
22. JPM amejenga Masoko ya Madini kila Mikoa yenye migodi ya madini
23. JPM amejenga ukuta wa Mirerani na kuweka Camera za Ulinzi
24. JPM amejenga Bandari Kilwa, na kuzipanua Bandari Mtwara, Tanga na Dar es Salaam
25. JPM amejenga Masoko ya Kisasa zaidi, ya maana kama Dodoma, Morogoro, Dar es Salaam
26. JPM amejenga Bus Stand za Kisasa Zaidi mikoani kama Dodoma, Morogoro, Dar es Salaam
27. JPM amenunua Vifaa Tiba kama MRI, CT Scan, Vifaa vya Kufanyia Oparations za Moyo pale JKCI Wagonjwa wanatoka nchi jirani kuja kutibiwa.
 
ndani ya miaka mitano na miezi kidogo aliyokaa ikulu,Rais Magufuli alifanya Mambo makubwa ambayo Marais wa nne kabla yake walishindwa kufanya,kama Rais wa Malawi alivyosema siku ya msiba wake,"No body new Magufuli was coming,and no body new Magufuli was going, Magufuli himself new he had little time,he did everything like he was in a rush to go somewhere,thank you President John Magufuli"

Hakika Mungu alitupa zawadi,na sasa zawadi hiyo ameichukua mfano wa Musa na wana wa israel kutoka misri.
Katika harakati za Musa kumtafuta Mungu arekebishe mambo,Aliinuka Haruni,raia wakamzidi nguvu akawatengenezea ndama sawasawa na matakwa yao(Wengi wape)

Tunamsubiria Yoshua aendelee na kazi,mengine yote ni kipindi cha mpito.Kanaani ni lazima tufike.
 
Trash
 

Peleka ujinga mbali.
 
Nyerere hakuwa msukuma mshamba
 
Aliuza nini hadi akapate pesa zote hizo na je kodi iliyotozwa toka kwa Watanzania ilifanya kazi gani?
 
Atakayekulaani na kukudhihaki atalaaniwa kabisa na atakayekutetea wazi wazi atabarikiwa hakika.

mtu akivaa suti akaja kwenye tv akaanza kumsema makufuli huyo mtu huwa anaonekana yupo uchi ila yeye hajijui, kiongozi mwenye heshima akikosa ajenda akaanza kumsema makufuli huwa anaonekana kama mbeba magunia. chadema na vyama vya upinzani tangu mlipo ruhusiwa na mama kufanya mikutano ya hadhara mmeona sifa kumpa zawadi ya kumsema makufuli kila mnapoalikwa kwenye mahojiano kwenye media zote hamtaki kuongelea vyama vyenu vitaifanyia nini tanzania mmekaa kumsema jpm mwanzo wa kipindi mpaka mwisho sasa nawaambieni majukwaa yenu baada ya muda mtakosa watu watabaki manyumbu kama nyinyi na huyo nabii wenu lisu ndio anakuja yeye hana jipya ataanza kumsema jpm mwanzo mwisho utafikiri aliwachukulia wake zenu
 
Umesikia CHADEMA wataanza mikutano Mwanza, mmeanza kuleta vimaneno vya kijinga. Nani amdhihaki Marehemu?
1. "Hawa wanaoropoka ropoka huko bungeni wafukuze watoke huko na wakija huku nje 'I will deal' with them"
2. "Huwezi kuwa msaliti na ukategemea uishi"
3. "Hawa watuhumiwa wenye silaha muwanyang'anye silaha haraka haraka"
4. "Viongozi wanaopanga kufanya maandamano wakae mstari wa mbele ili wakione wasikae nyuma nyuma kwa maana mimi huwa sijaribiwi"
5. "Msinijaribu, msinidrive!"
6. "Mwenye kuleta fyoko fyoko atakiona"
7. "I wish I was the IGP"
 
Aliuza nini hadi akapate pesa zote hizo na je kodi iliyotozwa toka kwa Watanzania ilifanya kazi gani?

bidii yake na kujiamini kwa kodi ya ndani alifanya makubwa kuliko marais wote wa tanzania na africa alikuwa akizungumzwa sana na matv za nje ya nchi hasa india kwa uchapaji kazi wake na utayari wake
 
Umesena vyema kabisa. Chukua tano
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…