Mkuu,
MMKJJ kaandika kwa mtindo wa kejeli... soma tena uelewe
Mweshimiwa nimesoma ulicho eleza nikidhani utatoa suluhisho linalokubalika kitaalamu.Lakini suluhisho uliloto limenisikitisha
Yani watu waliosoma waachie uongozi kwasababu niwa jamii fulani wawachie uliowaita wasio soma kwasababu ulizozieleza kwa uhakika tutakuua tunarudi nyuma
Kikubwa swala la wachaga wengi kusoma au kufanikiwa iwe ni changamoto kwa watanzania wote Wafunge mkanda wapeleke watoto shule wasisubiri serikali ijenge shule,ilete walimu,ifundishe watoto kusoma na wakati mwengine iwalazimishe wazazi hao kuwapeleka watoto shule (AIBU)
tupeleke watoto shule wasoma kisha mambo yote hayo yatakwisha sio wasomi waache kusaidia kujunga taaifa eti kwasababu ni wachanga au eti nimafisadi.(asiyefanya kazi na asile)
Regards
LETA wewe kwanza hizo data zinazoonyesha kuwa NAFASI ZOTE WALIZONAZO HAWAJA QUALIFY?
Kihiyo naye MCHAGGA?
Hata waislam wenyewe wameanza kushitukia elimu sasa hivi kwani zamani ilikuwa ni MADRASSA TUUU!
Na SHULE WALISEMA NI ELIM DUNIA!
Hivyo haikupewa kipaumbele sana.Na wakati wakienda ku apply kazi wanakuta kuwa elimu ya MADRASSA haiwasaidii kupata kazi na hivyo wanabakia kulalamikia UDINI NA UCHAGGA!
Jokakuu,
Mkuu umetazama kuhusiana na Wachagga against the rest!..Asilimia 6.7 ni aslimia waliyokuwa nayo Wanyanyusa, Wahaya na pengine mikoa yote mikubwa..Nilichotanguliza hapo juu nina hakika hesabu ya Wahaya na wanyakyusa haipo nyuma sana labda wanazidiwa kwa asilimia 0.0005. tofauti ambayo huwezi kupitisha hukumu kwamba wengine hawakusoma..
Sasa nikuulize ktk mfano huo huo utasema nini kuhusiana na Wakerewe ambao ni asilimi 0.65 ya Population na wana wasomi 2 ktk kitengo cha chuo hicho! hali tofauti ya kiasilimia ilitakiwa kwa kila Wachagga 10 awepo Mkerewe 1. Hapa kuna Wachagga 8 tu....Je, ndio kusema wakerewe wamesoma kuliko Wachagga?... mkuu sikubaliani na hilo nipe hesabu ya chuo kikuu chote! na laukama Wachagga watajenga aslimia kubwa kuliko makabila basi nitakubaliana nanyi katika ajira kwani navyofahamu mimi kinachotakiwa ktk ajira ni uwezo wa mtu sio namba za graduate ktk kila kabila. Kama Wachagga ni asilimia 30 ya wasomi wetu basi kuna uwezekano wa Wachagga kushika asilimi 30 ya ajira ktk hizo nafasi za juu nchini...ikiwa zaidi basi kuna sababu nyingine kabisa pengine wao wanapenda kuajiriwa serikalini zaidi ya mashirika.
Hakuna sababu hata moja ya kubweteza udhaifu huu wa kufikiri ambao ndio chanzo cha utumwa wetu. Kama ajira zimetolewa kutokana na wale walioenda kuomba na waka pick watu hawa kutokana na uwezo wao hili swala la Ukabila linatoka wapi?.. na ikiwa walipendelewa nafazi zile kwa sababu ya Kabila lao basi bila shaka dhana ya watu italeta mantiki.. hakuna kati yenu anayeweza kutupa ukweli hivyo hata hizi dhana za Ukabila ni kilio cha maskini..Nina hakika waajiriwa nchini ktk ngazi za wasomi hao Wachagga hawatengenezi 51% ya viongozi ktk mashirika na taasisi isipokuwa watu wanatazama baadhi sehemu za Ulaji kama ulivyotazama kitengo kimoja ktk chuo Kikuu.. kelel zote ni ktk kutafuta ulaji pale TRA na kweli Wachagga wamewahi na uwezo wanao..Sasa kwa kutazama nani kapata ktk ujanja bila shaka Mchagga mshindi hata mseme kitu gani hakuna justfication ya usomi ktk ajira nchini inayokwenda na kabila...Ni maisha tuliyokuwa sote tunafahamu kwamba Tanzania ajira lazia uwe na mtu kifua! uwe Mchagga au Mkerewe.kosa moja watu wanafunga goli sii kosa lao ni kosa la system nzima.
Kukosa kwao (walalahoi) kupata kazi sehemu ya Ulaji ndio chimbuko la malalamishi yote haya wametafuta hoja kama hizi kujenga chuki kama alivyofanya Wangwe.. Binafsi nina hakika NI ULAJI tu ndio ulimsukuma wangwe kuweka madai yale na wanaompinga wanatazama ULAJI badala ya kutoa sababu za msingi..ndio maana wanarushiana wao madongo. hoja bado imesimama pale pale.
Wale wanaotetea hili wanatumia pia Ukabila wa kujionyesha wao bora ati wamesoma!..Hizi ndio kasumba chafu sana kwani Tanzania nzima bado kabisa watu tuko nyuma ktk elimu.. Ni wakati wa kuwahimiza vijana wetu waende shule sii wachagga wala wamakonde sote kwa pamoja tuna tatizo la elimu nchini na ajira hakuna!...Ni vijana wangapi wa kichagga leo hii Machinga tena toka wakati wa Nyerere nakumbuka vizuri vijana wanaopiga kiwi viatu mijini, kuuza magazeti, sigara vituoni, michubuo, sabuni za Gardenia walikuwa vijana wa Kiachagga.. Biashara hiyo haikutokana na elimu hata kidogo..
Tena mara nyingi sana makabila ama nchi ambazo vijana wake wametapakaa kila sehemu kutafuta riziki hutokana na shida nyingi nyumbani.. Wa Ethiopia, na Wasomali wengi tulijenga imani kwamba wao waliamka zamani bila kufahamu kwamba vita kati ya wao kwa wao ndio chimbuko kubwa la wao kukimbia nchi zao. Huko nje kama wageni wakajijenga Upya wakatafuta elimu na makazi mapya.
Kwa hiyo nitazidi kusema hii mada haiwezi kujenga hoja ya msingi kama watu mtaendelea kuonyeshana vidole..
Mwanakijiji,
Sasa ndio umeona wazi kile nilichokuwa nikisema.. na hakika amekuja Mchagga mwenyewe na kudhihirisha kwamba anajiona yeye ni Superior kwa sababu ya ELIMU..tena kachukia povu lamtoka...
Yeye madai yake anavyosema yanatokana na UCHUNGU sijui wale wengine wanasema kwa moyo upi?.. bila shaka WIVU, ni maneno ya Mkoloni, makaburu, Watusi na wengineo ambao wote walisababisha mengi machafu ambayo hawakuyategemea wakati wakijivuna hivyo..
hakuna hata mtu mmoja anaweza kunipa takwimu za kuonyesha Wachagga wamesoma sana..Hakuna isipokuwa navyofahamu mimi Wachagga ni watafutaji na utamaduni wao unawalazimu wengi kuchukua majukumu wakiwa bado wadogo.. Labda niseme kwamba ukitazama ratio ya unemployment Tanzania basi Wachagga ndio watakuwa na kina cha chini zaidi..Hivyo kama society nzima ina population ndogo ya watu wasiokuwa na ajira bila shaka wana hali nzuri kuliko wengine kiuchumi.... Hizi ndizo sifa ambazo Watu mnashindwa kuzizungumzia.. lakini haiwezekani kabisa swala la ajira TRA lihusiane na Wachagga wakati kuna Wahasibu wengi upande wa pili kuliko hili kabila moja tena kwa kiwango kikubwa sana..
Trust me, katika kila taaluma hata kama tuseme kuwa Wachagga wanashika asilimia 20 ya wasomi wote nchini lakini haiwezi kuwa sababu ya wao kukamata asilimia 75 ya viongozi wa juu ktk mashirika na serikali wakati wapo wasomi aslimia 80 (makabila yote kwa jumla) wenye uwezo kama wao..
Kilichotangulia hapo juu ni exactly nilichokuwa nikisema na ndio maana nimeombamada hii ibakie kama ilivyo kwa sababu sio tu wale wanaolalamika wana makosa ila kuna Wachagga pia wanaamini kuwa wao wamesoma sana na kujishughulisha sana!..
Kushughulika sana haina maana kabisa ya kupewa madaraka ya juu!.. hakuna mtu anayezungumzia kufanikiwa kimaisha isipokuwa kama kweli kuna Ukabila. Ningeomba huyu ndugu yangu Tonga anieleze ni juhudi gani alizofanya mchagga apate uhalali wa kuajiriwa TRA kuliko watu wa makabila mengine..Kujishughulisha kupi huko kama ni elimu kuna list ya wahasibu (NAD na CPA) ktk board ya Taifa!... nambie Wachagga ni wangapi ama asilimia ngapi..
wewe Mushi mzima? kuuza mtori kuna qualification gani? kupiga KIWI viatu au shoeshine unahitaji digrii gani?ufundi gereji n.k.
kazi za wachagga hadi kuuza mishikaki na kuwa wahudumu wa Bar, kama wamesoma wasingefanya kazi hizo.
JMushi,
Kubwajinga aweza kuwa ni mchanga na wala usishangae! Ila pengine ni mchaga ambaye hana chuki na makabila mengine! Hapana, mimi natania tuu..
Mkuu JokaKuu,
Kwanza naomba nikufahamishe kwamba, sina tatizo na editing yako yoyote yenye lengo la kuifanya original post yako ibaki na MAANA ILE ILE YA MWANZO. But my VERY BIG PROBLEM comes when the same editing is intended to negate or distort the whole meaning of your original post. Hebu soma maneno yako mwenyewe hapa chini kisha fikiria mara mbili:
..naomba nirekebishe kauli niliyoitoa hapo mwanzo. nimerejea makala niliyoisoma kuhusu Mangi Marealle na nasikitika kwamba nilifanya makosa ktk kuelezea habari hiyo.
Kwa mantiki hii nalazimika kusema kwamba sina imani na post zako zote kuhusiana na hii mada kwa sababu, nalazimika vile vile kuamini kwamba, chochote ulicho-post hapa hakina ukweli wowote bali kimesukumwa na ushabiki wako wa KIKABILA au na mapenzi yako kwa KABILA unalolitetea, liwe la wadigo au WACHAGG.
Jipange upya mzee kisha ufanye tathimini juu ya uhusiano baina ya jambo zima la ujambawazi na utajiri wa wachagoa na umasikini wa makabila mengine ambayo yanadai kupotelewa si tu na mali yao bali ni pamoja na upotevu wa maisha ya ndugu zao wengi waliopoteza maisha katika matukio mengi ya ujambawazi katika sehemu mbalimbali za hapo nchin. Hili nalo wanasema ni sababu mojawapo ya chuki zao juu ya kabila la wachegga wa kili. Binafsi sijui na siamini kama madai haya ni ya kweli kwani nawakilisha maneno niliyoyasikia mitaani.
Mkuu Joka Kuu,
Naishangaa akili yako jinsi ilivoshindwa kuelewa umuhimu wa maneno ya mtaani! Kwa kukusaidia tu ni kwamba maneno ya mtaani ni maneno ya watanzania. Au kwa kukufafanulia zaidi ni kwamba, huko mtaani wamechanganyikana watu wa aina mbalimbali ukianzia wamachinga hadi wasomi wa nchi hii wakiwemo baadhi ya wana JF. Watu hawa hukutana katika vikao mbalimbali vikiwemo vile vya harusi, bar na vinginevyo, bila kujali tofauti za kiwango cha elimu yao katika familiya zao na za marafiki zao.
Pia nakushauri uelewe kwamba, hata hizo habari za kwenye magazeti mashuhuri ya tz unazoziamini wewe, chanzo chake ni huko huko mtaani kwani huko ndiko wanakokaa watu ambao hufanya kazi kwenye makampuni mbalimbali ya tz. Hata zile habari za EPA hawa watu wa huko mtaani ndio wamesaidia kupatikana kwa urahisi, kwani ni wao haohao wanaofanya kazi huko BOT na sehemu zingine nyeti katika nafasi mbalimbali na kisha jioni hurudi mtaani kwao kujipumuzisha wakijichanganya na watu wa mtaani kwao.
Please Think Big! Elewa kwa upana nini maana ya mtaani!
Naona watu wamecomment kwa ghadhabu sana, especially wale ambao thread hii imewagusa, kitu cha Muhimu tujue kwamba hii issue ni nzito wala si ya kupuzwa kiasi hicho. Wenzetu nchi zilizoendelea hasa za Ulaya kuna legal binding za kuzisimia nchi kutekeleza mshikamano kwa jamii mbalimbali zinazounda nchi zao. Mnaweza pitia European Charter for Regional and Maniority Languages (1992) na pia Convention for Protection of Maniorities (1994). Nchi zilizoendelea wanasoma vyuoni kozi kama Diversity managements, Social Cohesion na Social Intergration kwa ajili ya matatizo kama haya. Sisi tunafumba macho huku watu wengine wanaumia kama tunavyoona kwenye hisia zao kwenye michango yao katika thread hii. Ni muhimu tukaelewa tofauti ya ajira ya Umma na Ajira Binafsi. Kama serikali inalengo la kutumia ajira kama kigezo mojawapo cha kuleta mshikamano katika nchi si sahihi kuajiri watu kwenye sector za umma kwa kufuata kigezo cha merit tu. Kwenye suala la Umma hakuna merit hata siku moja la sivyo hata wanawake wasingeweza kuwezeshwa ili wapate ajira au kujoin vyuo kama serikali ingekuwa inafuata merit tu. Kwa tuliofanya kazi serikalini tunajua kwamba kuna kazi ambazo hazina utalaamu sana kiasi kwamba uhusiano wa merit na utendaji kazi serikali si wa kuzingatia sana. Common service ya serikali ya Tanzania wala haiitaji merit recruitment kama inavyofikilika, hiyo ingeweza kutumika kubalance uiano wa watumishi baina ya makabila.
Na siyo sahihi kabisa kuwa wachaga hawapati upendeleo katika kupata ajira kwani wanaweza wakawa wanapata upendeleo inderectly kwa kuwa ndugu na jamaa wengi wako jikoni. Kwa wale wataalamu wa Social Science, Jaribuni kujikumbusha, Social Capital ya Bourdeux na Social Network ya Granovettor ili kujua jinsi gani mambo haya yanafanyika pasipo hata wakati mwingine kujua.
Swala la wachaga, wahaya, wanyakyusa kuwa na elimu zaidi ya mabila mengine ni swala la Kihistoria toka enzi za mkoloni wala haina maana kuwa hayo makabila ndio yamedondoshewa akili toka mbinguni. Mimi natoka mojawapo ya makabila hayo na nimeowa uchagani, kama serikali itakaa kimya na haioni matatizo ya baadaye inapandikiza mbegu za ubaguzi mbaya sana. Hiyo portifolio ya ndugu Stiven Waasira ndio kazi yake, lakini wala haitumiki hivyo imekaa kisiasa tu. Kwa tuliopitia kozi za Social Diversity management, ni wazi Tanzania imeundwa na vipisi vingi vya makabila na mapande mawili ya Dini (Muslim and Christian). Na hivyo vipisi vya makabira na mapande ya dini yanahitaji hekima na utaalam kuyamanage wala si kwa kufuata merit ambayo mwisho wake inatoa ajira ya makabila machache kwenye sector za umma pia kama inavyofahamika dini mojawapo inanung'unika kwa swala hili. Ieleweke hizo ni ajira za umma wala si mtu binafsi. Ajira za Umma zitumike kujenga taifa kama inavyofanywa kwenye ajira za vyombo vya ulinzi na usalama.
Nimeambatanisha paper ya Mtalaam wa Social Capiatl and Social Networks- Robert D Putnam kwa wale wanopenda kujielimisha kwa undani nadharia hii ya Social Capital and Networks na jinsi gani unaweza husianisha na makabila yenye nguvu na dini yenye wasomi wengi kwa Tanzania jinsi yanavyofaidika na hiyo hali ili hali wengine hawajui kama wanafaidika.
Mungu ibariki Tanzania.
Duh kweli Chacha Wangwe kawashika vibaya.....yaani yote haya ni mwendelezo wa hoja yake
my take:
Chadema hawana budi kushughulikia hoja za Wangwe badala ya kukaa kwenye comfort zone huku wakijiburudisha na kujiliwaza kwa hoja kama hii ya mwanakijiji ya eti "wachaga wanabaguliwa kwa kuwa wao ni wachagga tu" na si kwamba wao wachagga wanawabagua wasio wachagga kwa kuwapendelea wachagga wenzao
Ngoma inakuja kwa wale waliojenga utajiri wa kufa mtu Ukanda wa Afrika mashariki, kwa bidii zao bila ajira ya serikali ya bongo....[shirika landege precissiopn air][mabasi dar express].[Baa ya Mchagaa][duka la mchaga] [guest house ya mchaga] wakwere msijenichukia nishauri mchaga afunge guest house mnayoitumia iba wake za wenzenu mkijfanya vidume..haha.kuna wageni akina bakhressa, mohamed interprises.
Usishangae wabongo wakitimiza agenda wasizozijua kwa kutaja ukabila, udini etc
Naomba waingie hizo anga wakatoe wachaga, waarabu na wahindi ili wao wawe wakurugenzi....?tumekosa kazi wabongo.My friend mchaga ambaye elimu ya juu ni std seven. baba aliuza ng`ombe na kumpatia nauli ya kuenda mjini km wenzie .leo ni millionea wa kufa mtu ambaye ktk huduma zake amekuwa akikopesha wasomi wajinga wetu kwa kiasi kinachozidi mishahara yao(pombe,mahitaji ya nyumbani).Anashangaa watoto wa kiswahili wapo busy lalamikia ndugu zao hawawatoi, tangu anakuja mjini kuuza karanga, baadaye chipsi baadaye ndipo alipo...huyu ananiambia hahitaji hata kuwaajiri watu km hawa atawapa chakula, hela na sifa tuu.Ananiambia hela wanazopokea watoto wa mjini km msahahara au zawadi ni nyingi zaidi ya mataji anaohitaji leo kuanza kazi na kuwa tajiri tena within a year.Huwa anapata shida elewa hadithi ya ukabila na udini...
Baada ya wachaga kumaliza, na wakisto wawaachie waislamu....
Hivi hii success ya wachaga mbona siioni? unless our standards are too low, maendeleo ya wachagga ni ya kawaida kabisa na hayatofautiani kiadi kikubwa na ya makabila mengine.
Kama kuna tofauti, ufumbuzi wake wake ni KAZI. Wakinga ni wazuri sana katika biashara na wanapata maendeleo haraka. Hawakusaidiwa, wamrjisaidia, kwa kazi. Wamachinga wako kazini, na humo baadaye watatoka mamilionea, halafu wapo wataoanza kushangaa. KAZI, KAZI.