Je, wajua haya kuhusu bwawa la Mtera?

Je, wajua haya kuhusu bwawa la Mtera?

Emmanuel180

JF-Expert Member
Joined
Dec 17, 2019
Posts
342
Reaction score
626
Je, Wajua?
Mara ya mwisho Bwawa la Mtera kufunguliwa ili kuruhusu maji yapungue ilikuwa 21/3/2020 na haikuwahi kufanyika hivyo toka mvua za El Nino mwaka 1997/98

Je, Wajua?
Ujenzi wa bwawa la Mtera ulianza enzi za Nyerere, mwaka 1970 na lina ukubwa wa 'catchment' kilomita za mraba 68000

Je, Wajua?
Wazo la kwanza la ujenzi wa Bwawa la Mtera lilikuwa ni kwa ajili ya kuhifadhi maji na kuyachepusha kwenda Bwawa la Kidatu ili yatumike kuzalisha umeme. Baadae ikaonekana iwekwe mitambo ili izalishe umeme Mtera bila kuathiri flow ya maji kuelekea Kidatu.

Je, Wajua?
Pale darajani unapopita kwenye bwawa ni kizuizi cha kuzuia maji ili yaingie kwenye njia maalum na yakazalishe umeme baadae yashuke mpaka Kidatu

Je, Wajua?
Mtera kuna 'Turbines' mbili tu zenye uwezo wa kuzalisha umeme Megawati 80 japo uwezo wa maji kwenye Bwawa ni kuendesha 'Turbines' zaidi ya nne. Kutokana na lilivyojengwa hakuna namna ya kuongeza mitambo mingine zaid ya kujenga bwawa sehem ingine

Je, Wajua?
Mtera kuna handaki lenye urefu zaidi ya mita 800 limechongwa kwenye mwamba na ndani huko kuna chumba cha mkata umeme(control room) na mitambo yote ya kuzalisha umeme na kuingiza kwenye 'grid' ya Taifa ipo handakini.Yaani maji yamepitishwa chini kwa chini mpk mitamboni

Je, Wajua?
Licha ya kuwa maji ya Mtera ndio tegemezi kwa Bwawa la Kidatu, Bwawa la Mtera linazalisha umeme kiasi kidogo Megawati 80 kulinganisha na Bwawa la Kidatu MegaWati 200

Je, Wajua?
Kuanzia saa 10 mpaka saa 4 usiku ndio 'Peak Hour' yaani muda ambao Watanzania wanakuwa na matumizi ya umeme ya makubwa sana.

Je, Wajua?
Umeme wa AC huanza kutumika hapohapo baada ya kutengenezwa na ndio maana hauwezi kuhifadhika!

Je, Wajua?
Kigoma na baadhi ya sehemu mkoani Lindi haijaungwa kwenye umeme gridi ya Taifa, maana yake hata ikitokea hitilafu kwenye gridi ya Taifa kwenyewe umeme hautoathirika

Je, Wajua?
Je wajua zote hizi hazina picha kwasababu ni MARUFUKU kupiga picha maeneo ya Bwawa la Mtera kwenye mitambo na mifumo ya kuzalisha umeme.

Je, Wajua?
Mojawapo ya sababu ya kuzuia kupiga picha maeneo ya Bwawa la Mtera ni kulinda hakimiliki ya teknolojia iliyotumika kupatengeneza. Kuna kamera sehemu nyingi kiasi kwamba uwezekano wa kuonwa ukipiga picha hata ukiwa ndani ya gari ni mkubwa sana

Cc. imma
 
Nilipita pale mara moja ila sikuwa na wazo la kupiga picha kwa sababu ya kushangaa daraja
 
Bila Shaka Wewe Ni mfanyakazi wa bwawa hilo.. tunashukuru kwa elimu nzuri Sana
 
Je, Wajua?
Mara ya mwisho Bwawa la Mtera kufunguliwa ili kuruhusu maji yapungue ilikuwa 21/3/2020 na haikuwahi kufanyika hivyo toka mvua za El Nino mwaka 1997/98

Je, Wajua?
Ujenzi wa bwawa la Mtera ulianza enzi za Nyerere, mwaka 1970 na lina ukubwa wa 'catchment' kilomita za mraba 68000

Je, Wajua?
Wazo la kwanza la ujenzi wa Bwawa la Mtera lilikuwa ni kwa ajili ya kuhifadhi maji na kuyachepusha kwenda Bwawa la Kidatu ili yatumike kuzalisha umeme. Baadae ikaonekana iwekwe mitambo ili izalishe umeme Mtera bila kuathiri flow ya maji kuelekea Kidatu.

Je, Wajua?
Pale darajani unapopita kwenye bwawa ni kizuizi cha kuzuia maji ili yaingie kwenye njia maalum na yakazalishe umeme baadae yashuke mpaka Kidatu

Je, Wajua?
Mtera kuna 'Turbines' mbili tu zenye uwezo wa kuzalisha umeme Megawati 80 japo uwezo wa maji kwenye Bwawa ni kuendesha 'Turbines' zaidi ya nne. Kutokana na lilivyojengwa hakuna namna ya kuongeza mitambo mingine zaid ya kujenga bwawa sehem ingine

Je, Wajua?
Mtera kuna handaki lenye urefu zaidi ya mita 800 limechongwa kwenye mwamba na ndani huko kuna chumba cha mkata umeme(control room) na mitambo yote ya kuzalisha umeme na kuingiza kwenye 'grid' ya Taifa ipo handakini.Yaani maji yamepitishwa chini kwa chini mpk mitamboni

Je, Wajua?
Licha ya kuwa maji ya Mtera ndio tegemezi kwa Bwawa la Kidatu, Bwawa la Mtera linazalisha umeme kiasi kidogo Megawati 80 kulinganisha na Bwawa la Kidatu MegaWati 200

Je, Wajua?
Kuanzia saa 10 mpaka saa 4 usiku ndio 'Peak Hour' yaani muda ambao Watanzania wanakuwa na matumizi ya umeme ya makubwa sana.

Je, Wajua?
Umeme wa AC huanza kutumika hapohapo baada ya kutengenezwa na ndio maana hauwezi kuhifadhika!

Je, Wajua?
Kigoma na baadhi ya sehemu mkoani Lindi haijaungwa kwenye umeme gridi ya Taifa, maana yake hata ikitokea hitilafu kwenye gridi ya Taifa kwenyewe umeme hautoathirika

Je, Wajua?
Je wajua zote hizi hazina picha kwasababu ni MARUFUKU kupiga picha maeneo ya Bwawa la Mtera kwenye mitambo na mifumo ya kuzalisha umeme.

Je, Wajua?
Mojawapo ya sababu ya kuzuia kupiga picha maeneo ya Bwawa la Mtera ni kulinda hakimiliki ya teknolojia iliyotumika kupatengeneza. Kuna kamera sehemu nyingi kiasi kwamba uwezekano wa kuonwa ukipiga picha hata ukiwa ndani ya gari ni mkubwa sana

Cc. imma
Sifa nyingi lakini bado mgao wa umeme upo palepale
 
Dah umenikumbusha nilipiga picha nikiwa kwenye Basi nikitoka Iringa, mbele kwenye geti wakasimamisha basi Askari wa SUMA JKT akatangaza kuna mtu kapiga picha Ajisalimishe, dah nilikosa amani watu wote kimya konda naye akaanza kusema jamani aliypuga licha ashuke, huku askari ananikazia macho akaniuliza ni wewe nikamwambia hapana uzuri nilikuwa nikishafuta picha zote nikampa simu nikamwambia angalia huku mapigo ya moyo yakienda resi vibaya sana.

Mwisho wa siku wakaturuhu dah ilikuwa siku mbaya sana kwangu
 
Kati ya tecnologia niliyoikubali ni ile mitambo kule chini, jinsi walivyochimba ule mwamba kwa urefu na ukubwa ulee, hewa nzuri ya oksijeni iliyochujwa na kuingizwa, kupitia mitambo,

Ukiwa kule ndani na palivyo pakubwa na yale maofisi ni kama upo nje tuuh, palivyo pasafi na pazuri.

Ukiangalia zile bomba zilivyokubwa na ile pressure ya maji ilivyokubwa, huwezi hata msikia mwenzako akiongea.
 
Nikiwa kwenye basi la Isamilo kuna raia alipiga picha na hakuna aliyemkamata
wengi ni uoga wao tu....izo imani zilikuwaga zamani sana mfano mdogo ni pale tazara ya dar kulikuwa na katazo ilo ila kuna wadau wanapiga picha na hakuna lolote la picha kuungua
 
Back
Top Bottom