Uchaguzi 2020 Je, wajua kuwa Mfumo wa Serikali ya Majimbo unatumika kwenye Nchi zenye kukosa Umoja wa Kitaifa?

Uchaguzi 2020 Je, wajua kuwa Mfumo wa Serikali ya Majimbo unatumika kwenye Nchi zenye kukosa Umoja wa Kitaifa?

Ndiyo maana tunasema serikali kuu isijihusishe na miradi midogo midogo. Rais hawezi kufika Kila kona ya nchi. Mambo ya Choo cha stand yaangaliwe na local governments. Ndiyo maana utakuta Rais anakariri miradi ili kuwa impress wananchi which is not necessary.
Ndugu,

Tuna balozi mtaani
Tuna mwenyekiti
Tuna mtendaji wa Kijiji
Tuna diwani
Tuna mkurugenzi
Tuna mkuu wa wilaya

Sasa tunataka nini?
 
Japo so kweli... Lakini nikubaliane na wewe kuwa ccm imesababisha kukosekana kwa umoja wa kitaifa nchini kwa miaka 60 sasa...
Najua utabisha....lakini nikuulize...
Hivi kweli kuna umoja wa kitaifa ikiwa wengine wanakunywa maji ya mabomba tena yaliyotibiwa wakati huo huo wengine wanakunywa maji ya tope na hawaoni tatizo lolote...??
Je kuna umoja wa kitaifa ikiwa wengine wanatiririka kwenye mabarabara ya lami wakati huo huo wengine hata lami hawajui inavyofanana...!!
Je, kuna umoja wa kitaifa ikiwa kama mfanyakazi mafao yako unaambiwa ni hadi uzeeni wakati huoni uhakika wa kuufikia huo uzee... Na hata ukifanikiwa kuufikia bado mafao ni ahadi hewa...??

Mkuu rejesheni madaraka kwa wananchi...!!!
 
Waungwana,

Chunguzeni leo hii nchi zote ambazo ni kinara wa mfumo wa Serikali za majimbo (federal government) duniani ni nchi ambazo zilikuwa zinakabiliwa Sana na tatizo la kukosa umoja wa Kitaifa kutokana na Vita, udini au Kukosa lugha ya kuwaunganisha.

Marekani walikuwa mataifa huru 51. Kuwaunganisha ni lazima uwaachie baadhi ya madaraka yao, hivyo mfumo wa Serikali ya Majimbo ni sahihi kwao.

Canada wanashida ya lugha. Kuna majimbo hawajui au hawaongei kabisa kiingereza, wenyewe wanaongea kifaransa. Hawa ni muhimu kuwa na majimbo ili wawe huru kutumia lugha waipendayo.

Ujerumani walitawanyika na kuwa nchi mbili tofauti na ukuta ukajengwa Kati ya Ujerumani ya Mashariki na ile ya magharibi. Hawa ili kuwaunganisha mfumo wa Serikali ya Majimbo ulikuwa lazima ila maeneo hayo yabaki na sehemu ya utawala wake wa awali.

Nigeria imepitia mengi sana sana Kati ya waislamu wa kaskazini na wakristo wa kusini. Waafrika kusini vilevile wamepitia mengi Kuhusu ukoloni na ukaburu. Wazungu wengi walibaki Afrika Kusini baada ya Uhuru kamili mwaka 1994. Kwa misingi hiyo, unaweza kabisa kuona Nigeria na Afrika kusini walihitaji utawala wa majimbo.

Sisi Tanzania tunahitaji utawala wa majimbo ili iweje? Je, changamoto za kiuchumi, utamaduni na kisiasa zinatokana na mazingira hayo niliyoyataja hapo juu?

Wazungu hawana makabila na karibu wote wana dini au imani sawa. Kuwawekea utawala wa majimbo sio mbaya. Hapa kwetu tunajadili sio to dini Bali hata dhehebu. Kuna baadhi ya watu walisema katika uchaguzi wa 2015, Sasa ni zamu ya M-KKKT kuwa wa -RC wametawala Sana. Sasa kwenye nchi Kama hii uanze umajimbo, tunategemea nini kitokee?

Majimbo yatatutenga zaidi badala ya kutuleta pamoja. Mfumo wa Serikali za mitaa kwa Tanzania ni mzuri na toshelevu. Kama Kuna changamoto basi ni Kuboresha tuu.

Ninawashangaa Sana wapinzani, sijui wamekunywa wanzuki ya wapi. Tasilimali za kila eneo husaidia eneo hilo na maeneo mengine. Hii ni kwasababu watu wanaingiliana na wanaweza kuishi popote. Mtoto wa Kagera anapangiwa kazi Tanga na maisha yanaenda. Mtu wa Mtwara anahamia Mbeya anakuwa mnyaki maisha yanaenda.

Watanzania tuukumbatie umoja, amani na mshikamano wetu kwa kuchagua mafiga matatu happy 28 Oktoba, 2020. Tuwaashibu wapinzani wanaotaka kutugawa kwa kuwanyima kura.

Amani Msumari

Tanga (kwasasa Kigamboni kuogelea kidogo na kumtafutia Rais Magufuli kura za bonus).
Badala ukadanganye huko Nanjilinji ambako kuna watu wanaoikubali ccm kwa mujibu wa TWAWEZA, sasa ulivyo MBULULA unakuja hapa kudanganya ma GT?
Lumumba lini mtakuwa na akili?!

Sent from my Infinix X606B using JamiiForums mobile app
 
Nchi haiendeshwi kwa ndoto ya mzee Mtei ambayo CHADEMA wote wanalazimika kuihubiri na kuitetea. Haifai kwani itatuletea shida kubwa Kama taifa. Tutawakataa na hata sasa tumewakataa
Nakushauri useme umewakataa, na siyo mmewakataa, kwa sababu hujashirikiana na mtu kuweka hili andiko, na zaidi ya hapo 28oct
 
Kwanza wewe ni Muongo, Ujerumani sio Nchi mbili, Ujerumani ni Nchi 17 na kila Nchi ina Raisi wake, na wanatumia hio Dhana ya Majimbo ingawa wote wanazungumza kijerumani. Siri kuba ya mafanikio yao ni huo mgawano wa Majimbo, kua Kodi zinakuswanya kuanzia chini, kilichobaki ndio kinaenda serikali kuu.

Baadae Serikali kuu inaangalia jimbo lopi ni Tajiri Zaidi na lipi ni Maskini inachangia kuweka usawa baina ya Majimbo. Hata Baada ya Ujerumani ya mashariki na Magharibi , Magharibi walikuwa Matajiri ukilinganisha na Mashariki, kwa hiyo Wafanyakazi wa Magharibi walikuwa wanalipia kodi iliyokuwa ikiitwa Solidarity Tax (Kuonesha umoja) mpaka mwaka huu ndio kodi hio iimeondolewa
Mwambie hata kabla ya East na West kuungana, West walishakuwa na majimbo. UK ni mfano mwingine. Nchi kubwa huwezi kuzitawala toka sehemu moja, majimbo yanakuja naturally.
 
Japo so kweli... Lakini nikubaliane na wewe kuwa ccm imesababisha kukosekana kwa umoja wa kitaifa nchini kwa miaka 60 sasa...
Najua utabisha....lakini nikuulize...
Hivi kweli kuna umoja wa kitaifa ikiwa wengine wanakunywa maji ya mabomba tena yaliyotibiwa wakati huo huo wengine wanakunywa maji ya tope na hawaoni tatizo lolote...??
Je kuna umoja wa kitaifa ikiwa wengine wanatiririka kwenye mabarabara ya lami wakati huo huo wengine hata lami hawajui inavyofanana...!!
Je, kuna umoja wa kitaifa ikiwa kama mfanyakazi mafao yako unaambiwa ni hadi uzeeni wakati huoni uhakika wa kuufikia huo uzee... Na hata ukifanikiwa kuufikia bado mafao ni ahadi hewa...??

Mkuu rejesheni madaraka kwa wananchi...!!!
Nieleze n kivipi serikali ya majimbo itashughulikia hayo uliyoyataja
 
Wengi wanaongelea serikali ya majimbo kwasababu tuu Lissu na CHADEMA wamesema ilihali hawalijui chimbuko lake
 
Waungwana,

Chunguzeni leo hii nchi zote ambazo ni kinara wa mfumo wa Serikali za majimbo (federal government) duniani ni nchi ambazo zilikuwa zinakabiliwa Sana na tatizo la kukosa umoja wa Kitaifa kutokana na Vita, udini au Kukosa lugha ya kuwaunganisha.

Marekani walikuwa mataifa huru 51. Kuwaunganisha ni lazima uwaachie baadhi ya madaraka yao, hivyo mfumo wa Serikali ya Majimbo ni sahihi kwao.

Canada wanashida ya lugha. Kuna majimbo hawajui au hawaongei kabisa kiingereza, wenyewe wanaongea kifaransa. Hawa ni muhimu kuwa na majimbo ili wawe huru kutumia lugha waipendayo.

Ujerumani walitawanyika na kuwa nchi mbili tofauti na ukuta ukajengwa Kati ya Ujerumani ya Mashariki na ile ya magharibi. Hawa ili kuwaunganisha mfumo wa Serikali ya Majimbo ulikuwa lazima ila maeneo hayo yabaki na sehemu ya utawala wake wa awali.

Nigeria imepitia mengi sana sana Kati ya waislamu wa kaskazini na wakristo wa kusini. Waafrika kusini vilevile wamepitia mengi Kuhusu ukoloni na ukaburu. Wazungu wengi walibaki Afrika Kusini baada ya Uhuru kamili mwaka 1994. Kwa misingi hiyo, unaweza kabisa kuona Nigeria na Afrika kusini walihitaji utawala wa majimbo.

Sisi Tanzania tunahitaji utawala wa majimbo ili iweje? Je, changamoto za kiuchumi, utamaduni na kisiasa zinatokana na mazingira hayo niliyoyataja hapo juu?

Wazungu hawana makabila na karibu wote wana dini au imani sawa. Kuwawekea utawala wa majimbo sio mbaya. Hapa kwetu tunajadili sio to dini Bali hata dhehebu. Kuna baadhi ya watu walisema katika uchaguzi wa 2015, Sasa ni zamu ya M-KKKT kuwa wa -RC wametawala Sana. Sasa kwenye nchi Kama hii uanze umajimbo, tunategemea nini kitokee?

Majimbo yatatutenga zaidi badala ya kutuleta pamoja. Mfumo wa Serikali za mitaa kwa Tanzania ni mzuri na toshelevu. Kama Kuna changamoto basi ni Kuboresha tuu.

Ninawashangaa Sana wapinzani, sijui wamekunywa wanzuki ya wapi. Tasilimali za kila eneo husaidia eneo hilo na maeneo mengine. Hii ni kwasababu watu wanaingiliana na wanaweza kuishi popote. Mtoto wa Kagera anapangiwa kazi Tanga na maisha yanaenda. Mtu wa Mtwara anahamia Mbeya anakuwa mnyaki maisha yanaenda.

Watanzania tuukumbatie umoja, amani na mshikamano wetu kwa kuchagua mafiga matatu happy 28 Oktoba, 2020. Tuwaashibu wapinzani wanaotaka kutugawa kwa kuwanyima kura.

Amani Msumari

Tanga (kwasasa Kigamboni kuogelea kidogo na kumtafutia Rais Magufuli kura za bonus).
Ngoja kwanza, Majimbo yanayohubiriwa na Chadema Unayajua? Kila Jimbo Linajumuisha Mikoa mingapi na ipi?

Haya hubiri utengano namna utakavyotokea.
 
Badala ukadanganye huko Nanjilinji ambako kuna watu wanaoikubali ccm kwa mujibu wa TWAWEZA, sasa ulivyo MBULULA unakuja hapa kudanganya ma GT?
Lumumba lini mtakuwa na akili?!

Sent from my Infinix X606B using JamiiForums mobile app
Tumewazoea pingapinga.

Nipo Kivukoni hapa naongea na wavuvi. Nimewaeleza kuhusu ubovu wa Sera za CHADEMA, wameniemewa Sana. Wamesema hivi " hapa labda kidogo utaje ACT hao wapinzani wengine hamna kitu. Sisi tunakuahudi tunamchagua diwani Tarik, mbunge Zungu na Rais Magufuli.
 
Ndugu,

Tuna balozi mtaani
Tuna mwenyekiti
Tuna mtendaji wa Kijiji
Tuna diwani
Tuna mkurugenzi
Tuna mkuu wa wilaya

Sasa tunataka nini?
Hao Watendaji na Wakuu wa Wilaya wasiteuliwe na serikali, wachaguliwe na wananchi kama Madiwani. Mkurugenzi awe mwajiriwa wa Wilaya husika na siyo mteule wa Rais toka Dodoma!!
 
Nieleze n kivipi serikali ya majimbo itashughulikia hayo uliyoyataja

Yaani hata kama hili huna jibu basi upo gizani...!!
Kupitia serikali ya majimbo kila eneo litakuwa na funds za kutokana na vyanzo nyake kwa ajili ya miradi yake...!! Mipango ya mapato na matumizi watafanya watu wa eneo husika...!!
Serikali kuu itakuwa ndogo na yenye wajibu wa kusaidia bajeti au miradi pale inapohitajika hasa hasa kwenye majimbo yenye changamoto...!!
Kwa utaratibu wa sasa... Kazi tunafanye sisi huku mikoani lakini mipango na matumizi wapange Dar/Dodoma... Maendeleo yanaelekezwa kule Chato kunakowafurahisha mawaziri...
Hakika huu ni unyonyaji, ukandamizaji na ukoloni zaidi ya ule wa wajerumani na waingereza...

Pelekeni Madaraka Kwa Wananchi...!!
 
Badala ukadanganye huko Nanjilinji ambako kuna watu wanaoikubali ccm kwa mujibu wa TWAWEZA, sasa ulivyo MBULULA unakuja hapa kudanganya ma GT?
Lumumba lini mtakuwa na akili?!

Sent from my Infinix X606B using JamiiForums mobile app
Wahurumie tu CCM . Hawajui kuwa humu Tupo watu wengi wenye exposure zetu na ufahamu mkubwa wa mambo ya dunia na maendeleo
 
Lakini huo mfumo wa majimbo angalia Marekani na hio Canada ilipo kimaendeleo sisi miaka 58 Ujamaa umetufilisi mpaka akili zetu.


Ndukiiiii 🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️
Hukuelewa logic ya mtoa Uzi.
 
Waungwana,

Chunguzeni leo hii nchi zote ambazo ni kinara wa mfumo wa Serikali za majimbo (federal government) duniani ni nchi ambazo zilikuwa zinakabiliwa Sana na tatizo la kukosa umoja wa Kitaifa kutokana na Vita, udini au Kukosa lugha ya kuwaunganisha.

Marekani walikuwa mataifa huru 51. Kuwaunganisha ni lazima uwaachie baadhi ya madaraka yao, hivyo mfumo wa Serikali ya Majimbo ni sahihi kwao.

Canada wanashida ya lugha. Kuna majimbo hawajui au hawaongei kabisa kiingereza, wenyewe wanaongea kifaransa. Hawa ni muhimu kuwa na majimbo ili wawe huru kutumia lugha waipendayo.

Ujerumani walitawanyika na kuwa nchi mbili tofauti na ukuta ukajengwa Kati ya Ujerumani ya Mashariki na ile ya magharibi. Hawa ili kuwaunganisha mfumo wa Serikali ya Majimbo ulikuwa lazima ila maeneo hayo yabaki na sehemu ya utawala wake wa awali.

Nigeria imepitia mengi sana sana Kati ya waislamu wa kaskazini na wakristo wa kusini. Waafrika kusini vilevile wamepitia mengi Kuhusu ukoloni na ukaburu. Wazungu wengi walibaki Afrika Kusini baada ya Uhuru kamili mwaka 1994. Kwa misingi hiyo, unaweza kabisa kuona Nigeria na Afrika kusini walihitaji utawala wa majimbo.

Sisi Tanzania tunahitaji utawala wa majimbo ili iweje? Je, changamoto za kiuchumi, utamaduni na kisiasa zinatokana na mazingira hayo niliyoyataja hapo juu?

Wazungu hawana makabila na karibu wote wana dini au imani sawa. Kuwawekea utawala wa majimbo sio mbaya. Hapa kwetu tunajadili sio to dini Bali hata dhehebu. Kuna baadhi ya watu walisema katika uchaguzi wa 2015, Sasa ni zamu ya M-KKKT kuwa wa -RC wametawala Sana. Sasa kwenye nchi Kama hii uanze umajimbo, tunategemea nini kitokee?

Majimbo yatatutenga zaidi badala ya kutuleta pamoja. Mfumo wa Serikali za mitaa kwa Tanzania ni mzuri na toshelevu. Kama Kuna changamoto basi ni Kuboresha tuu.

Ninawashangaa Sana wapinzani, sijui wamekunywa wanzuki ya wapi. Tasilimali za kila eneo husaidia eneo hilo na maeneo mengine. Hii ni kwasababu watu wanaingiliana na wanaweza kuishi popote. Mtoto wa Kagera anapangiwa kazi Tanga na maisha yanaenda. Mtu wa Mtwara anahamia Mbeya anakuwa mnyaki maisha yanaenda.

Watanzania tuukumbatie umoja, amani na mshikamano wetu kwa kuchagua mafiga matatu happy 28 Oktoba, 2020. Tuwaashibu wapinzani wanaotaka kutugawa kwa kuwanyima kura.

Amani Msumari

Tanga (kwasasa Kigamboni kuogelea kidogo na kumtafutia Rais Magufuli kura za bonus).
Mada ya kitoto kabisa hii.
 
Kwavile dawa ya kutojitenga ni majimbo sasa ubaya wake nini?.
 
Huko hakuna wewe ni kabila flani au dini flani. Halafu nchi yao imeshaendelea na wanapata mahitaji yote. Hapa kwetu aki tutashikana uchawi. Kwani Nigeria au Somalia ni mbali kaka? Mifano ipo hai
Kwani kipi kilianza;majimbo au maendeleo? N unaposema issue ya Ukabila inakujaje? Kwani tukisema Mwanza,Geita,Shinyanga liwe jimbo moja ndio itachochea ukabila? Kwani watu wa makabila mengine hawatoruhusiwa kufanya kazi?Kazi zitatolewa kwa kigezo cha ukabila? Shule zitafundishwa kwa kisukuma? Askari watakao toka depo watagawanywa kwa ukabila? maswali mengi tu
 
Sio ishu ya Rais, n ishu ya bunge. Bajeti huandaliwa kutoka ngazi ya chini kabisa ili kuleta uwakilishi
Ilitakiwa iwe hivyo lakini siyo hivyo. Bajeti inatayarishwa, pesa zinakusanywa kuanzia huku chini ... lakini matumizi yanaamuliwa Dodoma. Mfano, Chato Airport iko kwenye bajeti ya mwaka gani ...!?
 
Back
Top Bottom