Je, wajua kuwa Simba ndio ilisababisha Tanzania kuitwa kichwa cha Mwendawazimu?

Stephen Musa master,athman china
 
Uchawi wake ulimdanganya
 
Kabisa aisee,nakumbuka ligi daraja la tatu ilikua na wachezaji viwango kuliko ligi kuu leo
 
Simba ndiyo nembo ya mpira wa nchi hii kwa upande wa vilabu. Naona baada ya kutoka eda ya miaka minne ndiyo mmekua mazuzu. Kila uto akiamka, anawaza kuijadili Simba! Na nyinyi baada ya miaka dahali ndiyo mnaambulia point saba muitweje?!
 
Dua Saidi alikuwepo Simba, ila hakusajiliwa katika mashindano ya kimataifa, Alicheza mashindano ya ndani pekee.
 
Naweza kukubaliana na wewe, Mimi ni Yanga asiyeamini hili atafute video ya mechi ya fainali kombe ka Cecafa Kampala, kama nakumbuka vizuri fainali ilikuwa either ni Yanga na SC Villa au ilikuwa na express maana Yanga ilizifunga hizi timu zote mbili za Uganda moja Nusu fainali na moja kwenye fainali.

Baada ya refa kupuliza filimbi mpira umekwisha Yanga bingwa wa Cecafa Abbas Gulamali alikuwa uwanjani pale Nakivubo stadium alikuwa analia, hapo kumbuka Lunyamila ndio yupo kwenye ubora wake.

Na kilio hiki aliwaahidi wachezaji wakichukuwa ubingwa atawapa kila mchezaji seti ya video na television.

Hii ahadi mpaka kuja kutimizwa Gulamali aliingiza makontena kadhaa ya TV kwa msamaha wa kodi ndio akawapa wachezaji TV, nilikuwa zulikuwa ahadi tu ambazo hazikuwa za dhati.
 
Simba ina rekodi nyingi sana za hovyo. Ona mwaka jana ilipigwa faini ya kulipa dola elfu 10 za Kimarekani, kwa kufanya vitendo vya kishirikina hadharani walipocheza na Orlando Pirates kule Afrika ya kusini!!
 
Yanga iliwafunga Express 3-1katika nusu fainali, ikawafunga Sports club villa 2-1Siku ya finali dk za mwisho naodha Paul Asule alivua jezi akimwomba kocha wake atoke maana alishindwa kabisa ku mdhibiti winga wa Yanga kijana, wamoto kabisa akitokea shule Edibily Jonas Lunyamila, lakini kocha wake alimkatalia na kumtaka amalizie mechi.
Yanga wali ahidiwa Tv baada ya kutwaa ubingwa.
Simba wali ahidiwa KIA katika mechi Yao ya fainali dhidi ya Stella na walipokosa ubingwa walipewa gari ndogo Carina.
Bahati Mbaya Kuna baadhi ya wachezaji wachache mpaka Leo hawakuwai kupewa gari zile.
 
Simba ndiyo nembo ya mpira wa nchi hii kwa upande wa vilabu. Naona baada ya kutoka eda ya miaka minne ndiyo mmekua mazuzu. Kila uto akiamka, anawaza kuijadili Simba! Na nyinyi baada ya miaka dahali ndiyo mnaambulia point saba muitweje?!
Nakumbuka wakati ule, jina lile lilitokana na timu ya taifa, sio Simba! Hivi kweli, timu imefika FAINALI, bado utaidharau? Huu ni upunguani, kama wakati ule kudharau mashindano ya SHIRIKISHO, na kuyaita ni ya WALIOSHINDWA! Lakini leo hii timu yao ipo huko, wanayaona mashindano hayo ni bora kuliko KLABU BINGWA! Jamaa ni MABINGWA wa kubadilisha mambo, na kuaminisha kibovu kionekane ni bora kuliko kilicho bora zaidi yao!
 
Umenikumbusha hiyo siku...
Mtangazaji wa RTD alisema "goooool" alipoangalia wavuni hakuna mpira akakanusha "sio goli"
Kuangalia vizuri ndipo akatangaza kuchanwa nyavu
 
Kia naijua vizuri sana ila toyota kia ndio siijui mpaka leo.
 
Kwa jinsi alivyotambulishwa siku ile pale ZBC2 inaonyesha alikuwepo kwenye kikosi kile. Inawezekana wanasiasa walikula njama na Azim Dewji kufanikisha njama za kufungwa. Nchi ngumu sana hii.
 
Kwa jinsi alivyotambulishwa siku ile pale ZBC2 inaonyesha alikuwepo kwenye kikosi kile. Inawezekana wanasiasa walikula njama na Azim Dewji kufanikisha njama za kufungwa. Nchi ngumu sana hii.
1993 hapakua na siasa hizo,Azim alikwepa kutoa kia
 
1993 hapakua na siasa hizo,Azim alikwepa kutoa kia
Siasa za kubaniana zimekuwepo toka nchi hii inapata uhuru, ongea na wazee watahuhadithia vimbwanga vya nchi hii. Niliwahi kusikia story ya kweli ya Sunday Manara kubaniwa kucheza mpira wa kulipwa Ufaransa.
 
Siasa za kubaniana zimekuwepo toka nchi hii inapata uhuru, ongea na wazee watahuhadithia vimbwanga vya nchi hii. Niliwahi kusikia story ya kweli ya Sunday Manara kubaniwa kucheza mpira wa kulipwa Ufaransa.
Ni Sunday au golikipa flan hivi wa stars,alibaniwa na marehemu bendera
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…