Je, wajua kuwa Simba ndio ilisababisha Tanzania kuitwa kichwa cha Mwendawazimu?

Sio kweli, umesema uongo.
 
Reactions: BRN
Mwaka 1994 Tanzania ilifanikiwa kuchukua kumbe la cecafa liliofanyika Kenya...fainali ilikuwa Tz na Uganda...
Timu ilipofika nchini ikafanyiwa sherehe ndogo ...ambapo Rais Mwinyi ndo alihutubia kuwapongeza ...na akasema Hongereni Kwa kukataa kuwa kichwa cha mwendawazimu ...ambapo kila kinyozi anajifunzia kunyoa ..ndo chanzo cha huo msemo..

Kama hujui uliza ueleimishwe...

Mods rekebisheni hii thread inamtaja Rais Mwinyi kwenye uwongo...
Maxence Melo Cookie
 
Humu watu wako kwenye utani wa jadi we unashupaza shingo utafikiri umechukuliwa mke wako? Ebooh? Huna majukumu ya msingi ya kufanya paka unakimbilia kushtaki? Relax maisha hayapo hivi, au hili jambo limekugusa Moja Kwa Moja? Sio Kwa kupanic kiasi hichi
 
Wewe hujui humu watoto Wengi umri kuanzia miaka 24..mwaka 1994 Wengi hawajazaliwa...why ulete utani wa kutunga uongo???na kuharibu history na kumsingizia Mzee Mwinyi kitu sio cha kweli??
 
Wewe hujui humu watoto Wengi umri kuanzia miaka 24..mwaka 1994 Wengi hawajazaliwa...why ulete utani wa kutunga uongo???na kuharibu history na kumsingizia Mzee Mwinyi kitu sio cha kweli??
Mimi sijaleta hii taarifa, pia kila anayeleta taarifa humu haimaanishi yeye ndio mwandishi, wakati mwingine ameikuta mahali akaikopi na kuja kui paste humu Lengo ni kuhabarisha na kama unavyojua tena hii mitandao ya kijamii kila mtu anatamani awe wa kwanza kuhabarisha wengine.
Nadhani kama mleta habari Hana taarifa sahihi, Wewe ulikuwa na jukumu la kutoa izo taarifa sahihi kuliko kumshambulia yeye
 
Mgeni rasmi katika mechi ya Simba na Stella alikua Rais Ally Hassan Mwinyi na hapo kabla Alisha waomba mashabiki wa Yanga kama watakuja uwanjani basi wasishangilie wapinzani wa Simba ni Bora wakae kimya maana ata yeye amekuja uwanjani kuwa sapoti Simba.
Yanga wali sisitizwa watangulize uzalendo.
Mpaka kipindi chakwanza kina kwisha Simba alikua kapasuka bao mmoja na Yanga walikua watulivu.

Kipindi chapili kilipo changanya Simba wakapasuka bao la pili ndipo mashabiki wa Yanga walipo lipuka kwa kuimba uzalendo umetushinda.
Nikweli Rais Mwinyi alitoa kauli iyo ya Tanzania ni kichwa Cha mwendawazimu baada ya matokeo ayo ya kuhuzunisha.
 
Timu iliyofika fainali CAF ndiyo isababishe taifa kuitwa kichwa cha mwendawazimu?
Je , timu ambayo haijawahi kuvuka hata makundi nchi iitweje?

Acha kupotosha watu wewe utopolo . Chanzo cha hilo jina ni kufungwa kwa taifa stars kila ilipokuwa inashiriki mashindano ya kila aina
 
Sasa mtu atapotosha vipi wakati Kuna mamilioni ya watu waliona/sikia wakati kauli inatolewa na muhusika !!! Inawezekana wewe na baadhi ya watu hawakubahatika kuona/kusikia ila haiondoi ukweli uliopo.
 
Mkuu, utaumiza kichwa kuwaelewesha hawa "HAMNAZO"! Hawajui, bahati mbaya, hawajui kama hawajui, na cha kusikitisha, hawapo tayari kujua!
 
Mbweha wewe
 
Sawa kichwa Cha mwendawazimu
 
Wapi ufahamu wangu umetoka mkuu? Mbona bandiko liko wazi, wewe hutaki vijana wa kizazi hiki wajue maana halisi ya huu msemo na wapi chimbuko lake?
Umepotosha..kichwa cha Mwenda wazimu ilitumika au ilianza kutumika kwa timu ya Taifa na siyo klabu..
Maneno hayo yalitamkwa na Mhe Alli Hassan Mwinyi akiielezea timu ya Taifa ambayo ilikuwa inafungwa mara kwa mara.
Kabla hujazema kitu fanya utafiti Utopolo wewee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…