Je, wajua kuwa Simba ndio ilisababisha Tanzania kuitwa kichwa cha Mwendawazimu?

Je, wajua kuwa Simba ndio ilisababisha Tanzania kuitwa kichwa cha Mwendawazimu?

Ingawa huu usemi umetamalaki kwenye sekta mbalimbali hasa za michezo hapa Tanzania, ila kama ulikuwa hujui basi chukua hii Leo.

Mwaka 1993 klabu ya Simba ilifika fainali ya michuano iliyoitwa Caf cup dhidi ya Stella Abidjan ya nchini Ivory coast.
Mchezo wa kwanza ulipigwa nchini Ivory Coast uliisha kwa suluhu, hivyo mechi ya marudia ilikuwa lazima mshindi apatikane

Simba walijiandaa vizuri na mchezo huu wa marudia na hamasa ilikuwa kubwa kiasi cha kumwalika rais wa nchi wa wakati huo ndugu Ally Hassan Mwinyi kuwa mgeni rasmi siku hiyo.
Pia Aliyekuwa mfadhili wa Simba wakati huo ndugu Azim Dewji aliwaahidi wachezaji wote kuwanunulia magari aina ya Toyota KIA endapo wangeshinda mchezo huo.

Siku ya mchezo ilifika na Uwanja wa taifa wa wakati huo( Uwanja wa Uhuru) ulijaa pomoni kuisapoti timu ya nyumbani simba

Stella Abidjan walipiga mpira mwingi sana na kuichabanga Simba 2-0 magoli yote yakiwekwa kimiani na Mshambuliaji wao hatari BoLi Zozo

Ndipo baada ya mchezo huo, raisi Ali Hassan Mwinyi akitoka jukwaa kuu huku akiwa amelowa kwa aibu kubwa baada ya kuona timu ya nyumbani inafungwa mbele yake na kombe linachukuliwa kwenye ardhi ya nyumbani alitoa kauli hii" TANZANIA NI KICHWA CHA MWENDAWAZIMU" maneno haya alikuwa akiwalenga Simba waliokubali kufungwa uwanja wa nyumban mbele ya rais wa nchi Yao.
Sio kweli, umesema uongo.
 
  • Thanks
Reactions: BRN
Mwaka 1994 Tanzania ilifanikiwa kuchukua kumbe la cecafa liliofanyika Kenya...fainali ilikuwa Tz na Uganda...
Timu ilipofika nchini ikafanyiwa sherehe ndogo ...ambapo Rais Mwinyi ndo alihutubia kuwapongeza ...na akasema Hongereni Kwa kukataa kuwa kichwa cha mwendawazimu ...ambapo kila kinyozi anajifunzia kunyoa ..ndo chanzo cha huo msemo..

Kama hujui uliza ueleimishwe...

Mods rekebisheni hii thread inamtaja Rais Mwinyi kwenye uwongo...
Maxence Melo Cookie
 
Mwaka 1994 Tanzania ilifanikiwa kuchukua kumbe la cecafa liliofanyika Kenya...fainali ilikuwa Tz na Uganda...
Timu ilipofika nchini ikafanyiwa sherehe ndogo ...ambapo Rais Mwinyi ndo alihutubia kuwapongeza ...na akasema Hongereni Kwa kukataa kuwa kichwa cha mwendawazimu ...ambapo kila kinyozi anajifunzia kunyoa ..ndo chanzo cha huo msemo..

Kama hujui uliza ueleimishwe...

Mods rekebisheni hii thread inamtaja Rais Mwinyi kwenye uwongo...
Maxence Melo Cookie
Humu watu wako kwenye utani wa jadi we unashupaza shingo utafikiri umechukuliwa mke wako? Ebooh? Huna majukumu ya msingi ya kufanya paka unakimbilia kushtaki? Relax maisha hayapo hivi, au hili jambo limekugusa Moja Kwa Moja? Sio Kwa kupanic kiasi hichi
 
Humu watu wako kwenye utani wa jadi we unashupaza shingo utafikiri umechukuliwa mke wako? Ebooh? Huna majukumu ya msingi ya kufanya paka unakimbilia kushtaki? Relax maisha hayapo hivi, au hili jambo limekugusa Moja Kwa Moja? Sio Kwa kupanic kiasi hichi
Wewe hujui humu watoto Wengi umri kuanzia miaka 24..mwaka 1994 Wengi hawajazaliwa...why ulete utani wa kutunga uongo???na kuharibu history na kumsingizia Mzee Mwinyi kitu sio cha kweli??
 
Wewe hujui humu watoto Wengi umri kuanzia miaka 24..mwaka 1994 Wengi hawajazaliwa...why ulete utani wa kutunga uongo???na kuharibu history na kumsingizia Mzee Mwinyi kitu sio cha kweli??
Mimi sijaleta hii taarifa, pia kila anayeleta taarifa humu haimaanishi yeye ndio mwandishi, wakati mwingine ameikuta mahali akaikopi na kuja kui paste humu Lengo ni kuhabarisha na kama unavyojua tena hii mitandao ya kijamii kila mtu anatamani awe wa kwanza kuhabarisha wengine.
Nadhani kama mleta habari Hana taarifa sahihi, Wewe ulikuwa na jukumu la kutoa izo taarifa sahihi kuliko kumshambulia yeye
 
Mgeni rasmi katika mechi ya Simba na Stella alikua Rais Ally Hassan Mwinyi na hapo kabla Alisha waomba mashabiki wa Yanga kama watakuja uwanjani basi wasishangilie wapinzani wa Simba ni Bora wakae kimya maana ata yeye amekuja uwanjani kuwa sapoti Simba.
Yanga wali sisitizwa watangulize uzalendo.
Mpaka kipindi chakwanza kina kwisha Simba alikua kapasuka bao mmoja na Yanga walikua watulivu.

Kipindi chapili kilipo changanya Simba wakapasuka bao la pili ndipo mashabiki wa Yanga walipo lipuka kwa kuimba uzalendo umetushinda.
Nikweli Rais Mwinyi alitoa kauli iyo ya Tanzania ni kichwa Cha mwendawazimu baada ya matokeo ayo ya kuhuzunisha.
 
Timu iliyofika fainali CAF ndiyo isababishe taifa kuitwa kichwa cha mwendawazimu?
Je , timu ambayo haijawahi kuvuka hata makundi nchi iitweje?

Acha kupotosha watu wewe utopolo . Chanzo cha hilo jina ni kufungwa kwa taifa stars kila ilipokuwa inashiriki mashindano ya kila aina
 
Timu iliyofika fainali CAF ndiyo isababishe taifa kuitwa kichwa cha mwendawazimu?
Je , timu ambayo haijawahi kuvuka hata makundi nchi iitweje?

Acha kupotosha watu wewe utopolo . Chanzo cha hilo jina ni kufungwa kwa taifa stars kila ilipokuwa inashiriki mashindano ya kila aina
Sasa mtu atapotosha vipi wakati Kuna mamilioni ya watu waliona/sikia wakati kauli inatolewa na muhusika !!! Inawezekana wewe na baadhi ya watu hawakubahatika kuona/kusikia ila haiondoi ukweli uliopo.
 
Timu iliyofika fainali CAF ndiyo isababishe taifa kuitwa kichwa cha mwendawazimu?
Je , timu ambayo haijawahi kuvuka hata makundi nchi iitweje?

Acha kupotosha watu wewe utopolo . Chanzo cha hilo jina ni kufungwa kwa taifa stars kila ilipokuwa inashiriki mashindano ya kila aina
Mkuu, utaumiza kichwa kuwaelewesha hawa "HAMNAZO"! Hawajui, bahati mbaya, hawajui kama hawajui, na cha kusikitisha, hawapo tayari kujua!
 
Ingawa huu usemi umetamalaki kwenye sekta mbalimbali hasa za michezo hapa Tanzania, ila kama ulikuwa hujui basi chukua hii Leo.

Mwaka 1993 klabu ya Simba ilifika fainali ya michuano iliyoitwa Caf cup dhidi ya Stella Abidjan ya nchini Ivory coast.
Mchezo wa kwanza ulipigwa nchini Ivory Coast uliisha kwa suluhu, hivyo mechi ya marudia ilikuwa lazima mshindi apatikane

Simba walijiandaa vizuri na mchezo huu wa marudia na hamasa ilikuwa kubwa ambapo aliyekuwa mfadhili wa Simba wakati huo ndugu Azim Dewji aliwaahidi wachezaji wote kuwanunulia magari aina ya Toyota KIA endapo wangeshinda mchezo huo.

Siku ya mchezo ilifika na Uwanja wa taifa wa wakati huo( Uwanja wa Uhuru) ulijaa pomoni kuisapoti timu ya nyumbani simba

Stella Abidjan walipiga mpira mwingi sana na kuichabanga Simba 2-0 magoli yote yakiwekwa kimiani na Mshambuliaji wao hatari BOLIZOZO

Ndipo baada ya mchezo huo, mgeni rasmi akitoka jukwaa kuu huku akiwa amelowa kwa aibu kubwa baada ya kuona timu ya nyumbani inafungwa mbele yake na kombe linachukuliwa kwenye ardhi ya nyumbani alitoa kauli hii" TANZANIA NI KICHWA CHA MWENDAWAZIMU" maneno haya alikuwa akiwalenga Simba waliokubali kufungwa uwanja wa nyumban Tena mbele ya mashabiki wao.
Mbweha wewe
 
Hii haifuti ukweli kwamba simba anahistoria kubwa kimataifa kuliko utopolo. Usione leo hii simba anaenda kushiriki super cup ukafikiri ni kwa sababu ilya kujaza mashabiki uwanjani ndio kigezo. Mizizi ya simba imejikita mbali sana kimataifa ikiwemo kupitia aibu na misukosuko mingi.
Sawa kichwa Cha mwendawazimu
 
Wapi ufahamu wangu umetoka mkuu? Mbona bandiko liko wazi, wewe hutaki vijana wa kizazi hiki wajue maana halisi ya huu msemo na wapi chimbuko lake?
Umepotosha..kichwa cha Mwenda wazimu ilitumika au ilianza kutumika kwa timu ya Taifa na siyo klabu..
Maneno hayo yalitamkwa na Mhe Alli Hassan Mwinyi akiielezea timu ya Taifa ambayo ilikuwa inafungwa mara kwa mara.
Kabla hujazema kitu fanya utafiti Utopolo wewee
 
Back
Top Bottom